Uwanja wa ndege wa DSM(JNIA) washushwa viwango vya ubora kimataifa,Waziri Mbarawa chukua hatua upesi

Mkuu usifurahie hilo jambo. Kama ulikuwa haujui basi ktk mashirika ya umma yanayokusanya pesa za kigeni na kuichangia bajeti ya serikali ni TCAA ambayo hukusanya tozo/ushuru toka kwa kila ndege inayotua hapo JNIA. Sasa hauoni athari zake zitamgusa hadi bibi maskini wa kule kijijini anaetegemea huduma ya matibabu bure au mtoto wa mkulima anaetegemea elimu bure? Mfano mwingine ni kuwa unaweza kuugua ukapata rufaa ya matibabu nje kwa kupitia fedha za serikali sasa kama ndege kubwa hizo hazitui hauni itakuwa ngumu kusafirishwa kwenda nje kwa matibabu. Sijui kama ulikuwa unawaza hivi nilivyokutolea mfano. Tuache ubinafsi na tuipende nchi yetu nayo itulee.

NIMEKUOLEWA MDAU
 
Aibu !
Nikiwa na jamaa zangu kutoka nchi nyingine, tunaposafiri safari ndefu na kutua hapa na pele tukiwa wenye furaha, aibu yangu ni pale tunapotangaziwa sasa tunatua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA. Kwa jinsi Tanzania ilivyo nchi nzuri huwa wananiambia 'let's see the beauty of Tanzania'

Kwa anayesema tunakosoa bila kushauri hajielewi kabisa, wajibu wetu tumetimiza kwa kulipa kodi na kuchagua viongozi, hao viongozi ni kazi yao kuufanya uwanja wetu wa Ndege uendane na hadhi ya nchi,
 
Pia naunga mkono TAA imeoza kbs,management ya utawala ibadilishwe kbs kuna uozo mkubwa sana pale,kuna mwaka fulani waliwahi waita watu kufanya interview kwenye tangazo lao kiwango cha mshahara kilikuwa cha juu,kuja kusign mikataba wakasema eti tangazo lilikosewa kama ni watu makini kwan nin hawakuwambia watu mapema wakajijua?Tatizo ni umimi tuu ndo ulioja pale.
 
Awamu hii ya tano na bado...kila kukicha hata kilichokuwa kizuri kinakuwa kichafu sijui kuna nini awamu hii.....huu utawala nikama hauna baraka, maana jitihada zinaonekana kama.zinafanyika lakini matokeo ndio haya.
Nimeupenda huu uzi

Aibu tupu kwa kweli!!!!

Ha haaaa walifikiri wana akili wakaacha na jina la Kilimanjaro..., kweli hawa wamezoea kudanganya bila akili... na sasa hakuna cha rushwa kuanzia ngazi za juu.

Nashangaa hiyo CAT9 ilikuwaje ikapewa lazima walidanganya... kiwanja hicho kinatia aibu nchi yetu katika mengi sana.
 
Mimi nawaza tu hiyo speed ya gari la KIA usiku usiku...hahahaaa dereva wake alitamani liruke kama ndege kuja ku counter attack ujio wa ICAO
Naelewa nachokiongea mkuu Salary Slip
Ni kweli serikali kuanzia mwaka wa fedha,imepeleka mapato yote hazina na kuziondolew hizi mamalaka uwezo wa kujiamulia mambo wenyewe hasa yale ya harakaharaka yanayohitaji pesa
Lakini haiondoi ukweli kuwa,hizi Mgt za taasisi kama TAA zilikuwa na uwezo wa kuweka katika bajeti zao za ndani vifungu vya manunuzi ili kuendana na hitaji la kimataifa la zimamoto.Ila sbb ya mazoea na ujanjaujanja mqmbo haya hayafanyiki
Tukiingiza tu siasa za kuushambulia uongozi wa juu sbb za itikadi,tutashindwa kuona chanzo cha tatizo.Ndio
 
Ametokea wapi kabla ya kupata cheo hiki? Kwa nini anasubiri amri kutoka juu, atakuwa hana uwezo huyo ama kabebwa tu!!
Mkuu ndie alie muweka hapo na ni yeye anaesema anajua nani akae wapi kwa wakati gani, na amri zisizokwisha lazima mapungufu yatokee..
 
Asante saana ndugu kwa taarifa.
Ss wengine tunasikia habari ya terminal 3 kushindana na ya kenya, sasa kama kiwanja chenyewe kinashushwa grade kweli kitaweza kushindana na cha kenya.
 
Kwa kweli wamechelewa kutoa hayo maamuzi. ..Viongozi wetu ndio wengi wanaongoza kwa kusafiri lakini hawajifunzi toka kwa wenzetu na kutamani kuiga vizuri.

Embu sasa wahusike wachukulie hii kama changamoto muhimu sana ya kuwabadilisha ikibidi wavuke hata madaraja manne ya ushindi. ....

Mabadiliko ni lazima
 
Aibu !
Nikiwa na jamaa zangu kutoka nchi nyingine, tunaposafiri safari ndefu na kutua hapa na pele tukiwa wenye furaha, aibu yangu ni pale tunapotangaziwa sasa tunatua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA. Kwa jinsi Tanzania ilivyo nchi nzuri huwa wananiambia 'let's see the beauty of Tanzania'

Kwa anayesema tunakosoa bila kushauri hajielewi kabisa, wajibu wetu tumetimiza kwa kulipa kodi na kuchagua viongozi, hao viongozi ni kazi yao kuufanya uwanja wetu wa Ndege uendane na hadhi ya nchi,

Kiukweli wakosoaji katika nchi hii ndio Wazalendo na wenye msaada kuliko haya majamaa yasiojielewa... kiukweli hata ukiwa angani tu ukaangalia mji kwa juu utajua unatua kwenye nchi ya namna gani..
 
Kwa kweli wamechelewa kutoa hayo maamuzi. ..Viongozi wetu ndio wengi wanaongoza kwa kusafiri lakini hawajifunzi toka kwa wenzetu na kutamani kuiga vizuri.

Embu sasa wahusike wachukulie hii kama changamoto muhimu sana ya kuwabadilisha ikibidi wavuke hata madaraja manne ya ushindi. ....

Mabadiliko ni lazima
Na kila mara wamekuwa wakisafiri kwenda nchi za watu!!Sijui huko huwa wanajifunza nini cha maana?ni aibu sana
 
Back
Top Bottom