Heshima kwako Hussein Bashe.
Kwanza naomba kukupongeza kwa kuja jamvini na kujibu baadhi ya hoja na kutoa ufafanuzi katika masuala mbali mbali.Nikiri umejitahidi kujenga hoja lakini pia nikiri lugha unayotumia haifai kabisa ndani ya jamii iliyostaharabika,imejaa dharau,kiburi na zaidi ya yote inakatisha tamaa.
Umekiri mwenyewe umechezewa rafu kibao ndani ya chama chako baya zaidi umeonyesha dhahiri wewe ni mtu wa visasi na vinyongo.Vipi mambo uliyotendewa miaka mingi nyuma hutaki kusahau ? Labda imani na asili yako imekufunza hivyo,ukitendewa jambo baya siku zote ni lazima ujifunze kusamehee na kusahau.Ni uzushi na ubazazi kusema umesamee jambo fulani lakini huwezi kusahau.
Unakiri Lowassa akigombea urais utamuunga mkono hakika kati ya mambo ya kipumbavu uliyowahi kukiri hadharani hakuna kama hili na ikiwa msimamo wako ni huu hakika waliokunyima nafasi ya kugombea ubunge hawakufanya kosa kabisa walikuwa sahihi na ikiwa watakufanyia tena mwaka 2015 watakuwa wamelitendea taifa letu changa jambo jema.
Nikiri mwamzoni nilidhani Bashe ni miongoni mwa vijana wanaoweza kulisaidia taifa lakini baada ya kupitia andiko lako nimegundua hufai hata kurejeshewa uraia wa Tanzania.Vijana wa aina yako ndio wameifikisha Somalia hapo ilipo sasa [kukumbatia magaidi na wezi wa mali za umma]
Mwisho Mungu hawezi kuibarikia Tanzania wala Afrika kama tutawatukuza wezi na mafisadi.
Naomba kuwasilisha.
SHALOOOM JAMVINI
Sikupanga kuchangia bali hii Hoja ya NGONGO imenivutia HUWEZI KUBARIKI AFRIKA KWA KUKUMBATIA MAFISADI NA WEZI.
Hoja ya Bashe ni kwamba LOWASA AKITEULIWA NA CHAMA ATAMUUNGA MKONO,kwani hana mashaka juu ya uwezo wa lowasa kufanya kazi,nakubaliana na Bashe kabisa LOWASA ni mchapa kazi,hoja hapa ni kwamba kama lowasa ni mwizi kwanini yupo uraiani?BASHE amewatega wengi amesema akiteuliwa na chama tujiulize je CCM (MAGAMBA) huteua wezi?majambazi?ninachofahamu kila mtu anauhuru wa kusema lakini haki ya kuhumu ni ya mahakama kama el hajafikishwa mahakamani kwa wizi basi hana kosa.
Taifa letu tukufu tanzania limekumbwa na wimbi la kuhukumiana,juzi tumemsikia VUVUZELA akisema DR WA UKWELI ni FISADI eti analipwa hela nyingi au MBOWE KAMANDA MKUU walipoibua zengwe la ufisadi wa NSSF ,je tuwakatae dokta kwa kuwa katuhumiwa na magazeti ya UHURU na Mzalendo na jambo leo yameandika? kama ni wezi wapelekwe mahakamani wahukumiwe hapo tuwakatae sio tuhuma za kisiasa, Ninachokiona hapa kama EL anatuhumiwa kwa kosa la RICHMOND watanzania tusiwe wavivu wa kufikiri je maamuzi yale ni LOWASA NA MAMA REGINA?nani aliamua ? jibu tunajua ni serekali kupitia baraza la mawaziri,nani alikua kiongozi mkuu wa hiyo serekali?tunamjua,nani alikuwa mweneykiti wa kikao hicho?tunamjua mnakumbuka dk mwakiembe alisema wameficha mengine kulinda mamlaka ya URAIS, tumejinga utamaduni wa kupenda kujibu mambo kirahisi na kupelekea kutotatua tatizo la msingi maamuzi ya kifisadi mengi yamefanyika kupita baraza la mawaziri lakini wandugu tumekuwa wakwanza kutuhumu tunawataka na kusahau msingi wa tatizo.
Rada,tunamtuhumu chenge,kwani aliamua kununua rada yeye na mke wake? Richmond tunamtuhumu lowasa kwani aliamua yeye na mke wake? EPA na KAGODA tunawatuhumu kina maranda,rostam,jitu,na wengine kwani mmesahau balali alisema pesa zile zilienda CCM na sisi wote 2005 tukapewa kanga na tshirt na kuimba nyimbo zao na kutoa asilimia zaidi ya 80%
Dogo huyu wa magamba ameongea mambo ya msingi sana lakini nafahamu CCM hawachelewi kumdhibiti muda si mrefu utasikia kapigwa barua ya onyo na hako kacheo walikompa watakakwapua shauri yake CDM tu ndio uhuru wa kutoa maoni unapatikana,mimi sijaona kosa lake kusema anamuunga mkono lowasa ikiwa magamba watampitisha kama wakati huo atakua segerea basi BASHE atatuambia anamuunga mkono nani.ILA UKWELI MSINGI WA HOJA YAKE KUMUUNGA MKONO EL NI UWEZO WA KUFANYA KAZI NA HILO KULE MAGAMBA WAPO WAWILI EL NA MZEE WA MAKILOMITA NA MABARABARA wengine porojo tuuuuuuuuuuuuuuu