Utumwa mpya ndani ya Kanisa

Utumwa mpya ndani ya Kanisa

Ukiwa na namna yako ya pekee ya mtindo wa maisha hapa duniani ni ngumu sana kueleweka na walimwengu wote hata kama yana mafanikio makubwa .

Wewe IGA yule anayefuatwa na watu wengi wa ulimwengu huu hata kama ni mdhambi!! hapo sasa ndivyo utakavyo kubalika na kueleweka vizuri na walimwengu wa dunia na ulimwengu huu.
 
Teh heheheee! Kutwa kucha unahangaika na uwepo wa Mungu, kila nyuzi inayotaja Mungu upo halafu unawadanganya eti hayakusumbui. Unasumbukaje? Kwa sababu moyoni mwako ukweli unaujua na ndio unaokusumbua!
Wewe huangaiki? hebu toa hoja! Siyo kashfa na maneno machafu ambayo mnadai Mungu hapendi.
 
Nimeituma kama nami livyoikuta namani itawagusa wengi an ndio hali halisi iliyipi kwa sasa.

UTUMWA MPYA NDANI YA KANISA

Pale udadisi unapokwenda likizo (reasoning)
Ndani ya Kanisani,watu kwa kukosa maarifa wanaibiwa. Kwa bahati mbaya hatujifunzi kutoka kwa Wabeloya, hawa walikuwa wadadisi.

Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonike. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.

Watu Wanaibiwa kwa kupitia magonjwa yao , wanaibiwa kwa kupitia umaskini wao, wanaibiwa kwa kupitia kukata tamaa kwao , wanaibiwa kwa kupitia kutokujua kwao.

Wengi wao shida zao haziondoshwi ingawa mtumishi wa bwana (The man of God ) anaendelea kuneemeka.

Wanaibiwa kwa kutumi jina la yule ambaye alipotakiwa kulipa kodi ilibidi amtume mfuasi wake kupata hela kwenye kinywa cha Samaki.

Wanaibiwa kwa kutumia jina la yule ambaye alikuwa hana mahali pa kulaza ubavu wake .

Huu ninauita wizi wa bila kutumia nguvu.

Wizi huu unatokea sana Africa nzima ambapo waumini kiupofu wanafuata na kutimiza maagizo ya uongozi.

Kwa uaminifu mkubwa wanapanga foleni kununua miujiza kwa njia ya mafuta, maji , chumvi, vitamba nk. Kwa mtu yeyote anayejiita Mtumishi wa Mungu (The man of God).
Wengi wao wakihubiriwa kuwa kuna laana ya ukoo au kizazi ili hali maandiko yanatufundisha kuwa laana zote zilimalizwa pale msalabani .
Changamoto nyingi walizo nazo wakristo wengi Barani Africa kama umaskini na baadhi ya magonjwa,sio za kiroho,bali ni Ujinga.Mafundisho mengi kwa waumini ni juu ya laana ya kizazi au Ukoo (Generational curse) ingawa Mambo mengi ni ujinga wa kizazi au ukoo (Generational ignorance)

Katika Makala yake iliyochapishwa na jarida la Modern Ghana , toleo no.215 la April 2019 Mwandishi Kay Musonda ansema!

Afrika kwa sasa inashuhudia aina mpya ya utumwa kupitia Ukristo (ulokole). Aina hii ya utumwa wa imani imewafanya watu wengi kuwa wavivu wa kufikiri na uwezo wa kutafakari mambo umedumazwa.

Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu. Wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa. Wanajituza wao zaidi kuliko kumtukuza yule wanayemhubiri.

Wachungaji wa aina hii hawawezi kuongelea mafanikio ya watu weusi kama Barack Obama, Serena Williums, na Usain Bolt. Hawawezi kuongelea wagunduzi waliosaidia kutransform dunia kama akina Albert Einstein, Steve Jobs na wengine. Hawawezi kuongelea Wanasayansi waliodedicate maisha yao na wengine kufia maabara wakitafuta dawa za kutibu magonjwa mbalimbali yanayoisumbua Afrika.

Hawawezi kuongea kuhusu wanafasihi vijana kama Chimamanda Ngozi na Ben Okri, au wakongwe kama Chinua Achebe na Ngugi wa Thiong'o.

Kila pembe ya dunia kuna watu waliofanikiwa kutokana na maarifa, bidii, ubunifu, na weledi. Wapo wafanyabiashara, wanasiasa, wanafasihi na hata wanasayansi wanaofanya mambo makubwa ya kuisaidia dunia yetu. Lakini wachungaji wa Afrika hawatawaongelea watu wa aina hii.

Wao wataongelea mtu aliyepata kazi kimiujiza licha ya kukosa sifa za kupata kazi hiyo, kwa sababu tu aliombewa na kupewa mafuta ya upako siku ya interview ya kazi.

Wataongelea kuhusu kijana aliyetoa mshahara wake wote kwa miezi mitatu mfululizo kwa Mchungaji wake kama mbegu ya mafanikio, baadae akawa 'Boss' kazini.

Au wataongelea kuhusu kijana aliyefeli sekondari lakini baada ya baba yake kumalizia ukarabati wa nyumba ya Mchungaji, alipokea barua ya kupata 'admision' chuo kikuu bila hata kurudia mitihani.

Wachungaji hawa hutumia 'miujiza na shuhuda feki' kama njia ya kuwafumba akili wafuasi wao. Kule Afrika kusini kuna Mchungaji alidanganya kufufua mtu. Hata alipoomba msamaha bado kuna waumini wanaendelea kumuamini na kumsujudu.

Wachungaji hawa wamegundua haya ndio mahubiri yanayopendwa sana huku Afrika. Hawataki kuhubiri kuhusu Aliko Dangote alivyoanza biashara na magumu aliyopitia.

Wanahubiri kuhusu mama Janeth aliyekua mama Ntilie huko Enugu, lakini alipotumia mtaji wake wote wa shilingi laki 5 kununua mafuta ya upako kwa Nabii fulani, ghafla biashara yake ikakua na sasa anamiliki mahoteli makubwa pande zote za nchi. Yani bila mtaji, bila business plan, bila timeline ghafla tu akamiliki mahoteli. Na waumini watashangia kwa kusema Ameen.

Aina hii ya ukristo imepanda mbegu ya uvivu wa kufikiri kwa vijana wengi wa Afrika ambao wanalazimishwa kumuona Mungu kama Mfadhili wa wavivu, au wasiostahili. Kwamba mwanafunzi hata asiposoma anajua akipewa mafuta ya upako atafaulu tu siku ya mtihani. Mfanyabiashara hata asipokua mbunifu anajua akienda kwa 'baba wa miujiza' biashara yake itapanuka ghafla bin vuu. Mfanyakazi hata asipowajibika kazini anajua akitoa fungu la kumi kwa 'Dokta Upako' atapanda cheo.

Kwa baadhi ya makanisa Africa namna pekee ya kufanikiwa ni kufanya kile wanachokiita kupanda mbegu, kupaka mafuta ya upako au kunyunyuziwa maji ya baraka. Eti wanaofanikiwa haraka ni watu 30 wa mwazo wanaokimbilia mbele ya kanisa kila mmoja akiwa ameshika noti ya dola 100.

Aina hii ya mahubiri inawafanya watu waamini kwamba Mungu hawapendi wanaojituma na kuwa wabunifu katika kazi, badala yake anawapenda zaidi wanaotoa zaka, sadaka, malimbuko na fungu la 10 hata kama ni wavivu. Hii sio sawa hata kidogo kwa sababu Biblia inakataa uvivu kwa nguvu zote ( *Mithali 12:27 Bali mtu mvivu hapiki Mawindo yake; Bali Mwenye bidii anazo mali za thamani).*
_
Watu wanaaminishwa kwamba ukishatoa sadaka kanisani unaweza kuamka kila siku asubuhi ukapayuka 'Mimi ni Milionea' halafu ukavuta shuka na kuendelea kulala fofofo, ukisubiri sadaka uliyotoa ikupe muujiza wa kuokota hela, ili upate mtaji wa biashara unayoiwaza.

Mtu huna kazi, huna biashara wala wazo la biashara, huna ujuzi, huna elimu, lakini kila siku unashinda kanisani kumsikiliza Mchungaji anayesema kesho utakua milionea na wewe unasema "Baba napokea/Dady I receive". Huu ni utani.

Waambieni wanaofanya utani huu kwa kofia za Uchungaji, Uaskofu, Unabii au Utume kwamba wanamkosea Mungu. Waambieni Mungu wetu ni Mungu wa kanuni, na hana kanuni ya kuwabariki wavivu. Tuache kufundisha waumini wetu kwamba uvivu unalipa kupitia miujiza.

Mafanikio ni matokeo ya bidii, ubunifu na weledi. Biblia inazungumzia kuhusu karama. Hebu kila mtu atumie karama alizopewa kwa bidii, ubunifu na weledi aone kama hatafanikiwa. Sio sahihi kuwaambia watu wabweteke tu na kusubiria mafanikio kama kusubiria daladala kituoni kwa sababu tu wamepakwa mafuta ya upako.

Mungu alishatubariki *tangu wakati wa uumbaji wetu. Ni wajibu wetu kujibidisha katika yale tufanyayo ili baraka zake ziambatane nasi ( *Kumb 28:6 Utabarikiwa uingiapo utabarikiwa na utokapo).*

Wazungu na Wachina wanazidi kushindana katika kuitawala dunia kwenye mambo mbalimbali kuanzia viwanda, biashara, sayansi na teknolojia. Sisi tuko 'busy' kununua maji ya upako tukiamini yatatufanya tuwe kama Jack Ma au Bill Gates. Upuuzi.

Tumeumbwa kuitawala hii dunia (Mwanzo 1:28Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini na ndege wa angani, na kila kiumbw chenye uhai kiendacho juu ya nchi). Tutumie vipawa na karama tulizopewa ili kutimiza kusudi hilo la Mungu. Tusiruhusu Askofu, Mchungaji, Nabii, mtume au kiongozi mwingine yeyote wa dini atutawale akili zetu kwa kutuhubiria mafanikio ya miujiza. Wao wanaishi kifahari kwa sadaka za waumini wao, huku waumini wakiendelea kuwa mafukara wa kutupwa.

Biblia inasema kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa ( *Mithali 1:7 Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu).* Tutafute maarifa, tufanye kazi kwa bidii, na tumuabudu Mungu katika Roho na kweli. Kwa kufanya hivyo tutapata MAFANIKIO katika mambo yote tuyafanyayo.

NB: Makala hii inazungumzia baadhi ya makanisa ya kilokole sio yote. Dont generalize. Yapo makanisa ya kilokole yenye misingi bora, lakini mengine yamejaa upotoshaji. Haya ndio yaliyozungumzwa hapa. Tafsiri isiyo rasmi imefanywa
na Malisa GJ.
Tukutane wiki ijayo panapo majaliwa.
wajinga ndio waliwao
 
Am christian, i believe in Jesus and i believe in his miracles na nina amini wako wachungaji na maaskofu ambao kweli wana mcha Mungu na wanapokuombea kweli unapata uponyaji au kufungulia, ila tatizo unaloliona sasahivi kwanza si la kushangaza mana hata kwenye biblia takatifu ilishaandika kwamba nyakati za mwisho manabii wengi wa uongo watakuja na wataangamiza watu wengi sana, na pili the problem isn't them (hao manabii) bali waumini, watu hawamtafuti Mungu bali wanatafuta VITU, wamemgeuza Mungu kama mnganga wa kienyeji mtu anataka aendelee na maisha yake ya dhambi kama kawaida at the same time anatafuta baraka kutoka kwa Mungu ndo hao wanakimbilia kwa hao manabii wanaohubiri magari na nyumba na kuwa milionea sijui laana za ukoo yani wanaishia kudanganywa zaidi na kufanywa mazezeta zaidi. Na ndo mana unakuta mtu anakwambia ameokoka ila matendo yake utabaki mdomo wazi, mtu anakwambia ameokoka alivyovaa tena kanisani achia mbali mtaani hutaamini, ukimwambia anakwambia usimletee ulokole wa kizamani, na wachungaji wao wako kimya tu, sasa huwa najiuliza biblia ya zamani ni ipi na ya sasa ni ipi wanayotumia wao, watu wanazini humo makanisani kama hawana akili nzuri yani hata ile hofu ya Mungu ndani yao hakuna lakini ndo hao hao wanakwambia tumeokoka, hizo nyimbo za sikuhizi sasa ndo uuuuwi sometime unazima hadi radio hizo video ndo kabisaaaaa utachefukwa kiukweli kwenye gospel ni heri usikilize tu audio video nyingi zinakera alafu unaambiwa waimbaji wameokoka. Mungu atusaidie
Kweli kabisa
 
You mess up..!
Hata kama hilo ni kweli, huo ni ushahidi zaidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, kusingekuwa na mess ya aina yoyote.

Kila kitu kingekuwa katika perfect order.
 
Watu wamekuwa wavivu kuisoma biblia ndiyo maana wanapigwa, na waendelee kupigwa mpaka akili iwakae sawa. Watu wanapenda miujiza ya kuombewa, mara maji mara mafuta, mara chumvi nk.

Hakunaga mambo ya kuvunja laana hakuna nabii wala mtume wala mchungaji awezaye kuvunja laana, laana zilivunjwa na Yesu akamaliza kama akuzimaliza Yesu ni mtu gani awezaye kuzivunja?
Sadaka na zani vinapaswa vitolewe mahala sahihi hambapo hakuna ufisadi, ili vifanye kazi ya Mungu, lakini kwa staili hii ya uvivu wa kuyasoma maandiko wacha waendelee kupigwa mpaka akili ziwakae sawa.
 
Hahahah..! Kiranga Kwa akili yako wewe una hisi Mungu anaupande..?

Mungu yupo katikati ya mazuri na mabaya, God has no choice, no good or bad to him..! Alichonifanya kibaya na kizuri kwa binadamu ndicho kipimo cha hukumu zake kwetu.

Kifupi iko hivi hizo maafa na mabaya yote tunayaumba sisi katika maisha yetu si Mungu. Mfano huwa mnaambiwa dhambi mwisho wake ni mauti/kifo, utambue mtenda dhambi ni binadamu si Mungu.

Ukisema Mungu angetuumba na kutunyima utashi tufanye kazi kwa settings/programmed kama computer ata wewe hapo usinge hoji haya maswali yako ya kijinga. By the way Malaika wako programmed na hawa hizo mess zote unazosema kuwepo kwake ni kuthibitisha kutokuwepo kwa Mungu, mfano Malaika hawapatwi na hizo maafa na mabalaha, Lakini usidhani Malaika wanaenjoy/kufurahia uumbwaji wao zaidi ya binadamu.


Wewe jamaa uwezo wako wa reasoning nautilia shaka sana...!
Hata kama hilo ni kweli, huo ni ushahidi zaidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, kusingekuwa na mess ya aina yoyote.

Kila kitu kingekuwa katika perfect order.
 
Hahahah..! Kiranga Kwa akili yako wewe una hisi Mungu anaupande..?

Mungu yupo katikati ya mazuri na mabaya, God has no choice, no good or bad to him..! Alichonifanya kibaya na kizuri kwa binadamu ndicho kipimo cha hukumu zake kwetu.

Kifupi iko hivi hizo maafa na mabaya yote tunayaumba sisi katika maisha yetu si Mungu. Mfano huwa mnaambiwa dhambi mwisho wake ni mauti/kifo, utambue mtenda dhambi ni binadamu si Mungu.

Ukisema Mungu angetuumba na kutunyima utashi tufanye kazi kwa settings/programmed kama computer ata wewe hapo usinge hoji haya maswali yako ya kijinga. By the way Malaika wako programmed na hawa hizo mess zote unazosema kuwepo kwake ni kuthibitisha kutokuwepo kwa Mungu, mfano Malaika hawapatwi na hizo maafa na mabalaha, Lakini usidhani Malaika wanaenjoy/kufurahia uumbwaji wao zaidi ya binadamu.


Wewe jamaa uwezo wako wa reasoning nautilia shaka sana...!
Asipo elewa na hii uyu jamaa atakuwa na pepo anapepo zito (linalompelekea upumbavu ,ujinga pia na ukichaa wakutokuamini uwepo)

Ila naamini MUNGU atakuja kumuonyesha yeye ni nani kwake ikifika wakati
 
Nimeituma kama nami livyoikuta namani itawagusa wengi an ndio hali halisi iliyipi kwa sasa.

UTUMWA MPYA NDANI YA KANISA

Pale udadisi unapokwenda likizo (reasoning)
Ndani ya Kanisani,watu kwa kukosa maarifa wanaibiwa. Kwa bahati mbaya hatujifunzi kutoka kwa Wabeloya, hawa walikuwa wadadisi.

Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonike. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.

Watu Wanaibiwa kwa kupitia magonjwa yao , wanaibiwa kwa kupitia umaskini wao, wanaibiwa kwa kupitia kukata tamaa kwao , wanaibiwa kwa kupitia kutokujua kwao.

Wengi wao shida zao haziondoshwi ingawa mtumishi wa bwana (The man of God ) anaendelea kuneemeka.

Wanaibiwa kwa kutumi jina la yule ambaye alipotakiwa kulipa kodi ilibidi amtume mfuasi wake kupata hela kwenye kinywa cha Samaki.

Wanaibiwa kwa kutumia jina la yule ambaye alikuwa hana mahali pa kulaza ubavu wake .

Huu ninauita wizi wa bila kutumia nguvu.

Wizi huu unatokea sana Africa nzima ambapo waumini kiupofu wanafuata na kutimiza maagizo ya uongozi.

Kwa uaminifu mkubwa wanapanga foleni kununua miujiza kwa njia ya mafuta, maji , chumvi, vitamba nk. Kwa mtu yeyote anayejiita Mtumishi wa Mungu (The man of God).
Wengi wao wakihubiriwa kuwa kuna laana ya ukoo au kizazi ili hali maandiko yanatufundisha kuwa laana zote zilimalizwa pale msalabani .
Changamoto nyingi walizo nazo wakristo wengi Barani Africa kama umaskini na baadhi ya magonjwa,sio za kiroho,bali ni Ujinga.Mafundisho mengi kwa waumini ni juu ya laana ya kizazi au Ukoo (Generational curse) ingawa Mambo mengi ni ujinga wa kizazi au ukoo (Generational ignorance)

Katika Makala yake iliyochapishwa na jarida la Modern Ghana , toleo no.215 la April 2019 Mwandishi Kay Musonda ansema!

Afrika kwa sasa inashuhudia aina mpya ya utumwa kupitia Ukristo (ulokole). Aina hii ya utumwa wa imani imewafanya watu wengi kuwa wavivu wa kufikiri na uwezo wa kutafakari mambo umedumazwa.

Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu. Wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa. Wanajituza wao zaidi kuliko kumtukuza yule wanayemhubiri.

Wachungaji wa aina hii hawawezi kuongelea mafanikio ya watu weusi kama Barack Obama, Serena Williums, na Usain Bolt. Hawawezi kuongelea wagunduzi waliosaidia kutransform dunia kama akina Albert Einstein, Steve Jobs na wengine. Hawawezi kuongelea Wanasayansi waliodedicate maisha yao na wengine kufia maabara wakitafuta dawa za kutibu magonjwa mbalimbali yanayoisumbua Afrika.

Hawawezi kuongea kuhusu wanafasihi vijana kama Chimamanda Ngozi na Ben Okri, au wakongwe kama Chinua Achebe na Ngugi wa Thiong'o.

Kila pembe ya dunia kuna watu waliofanikiwa kutokana na maarifa, bidii, ubunifu, na weledi. Wapo wafanyabiashara, wanasiasa, wanafasihi na hata wanasayansi wanaofanya mambo makubwa ya kuisaidia dunia yetu. Lakini wachungaji wa Afrika hawatawaongelea watu wa aina hii.

Wao wataongelea mtu aliyepata kazi kimiujiza licha ya kukosa sifa za kupata kazi hiyo, kwa sababu tu aliombewa na kupewa mafuta ya upako siku ya interview ya kazi.

Wataongelea kuhusu kijana aliyetoa mshahara wake wote kwa miezi mitatu mfululizo kwa Mchungaji wake kama mbegu ya mafanikio, baadae akawa 'Boss' kazini.

Au wataongelea kuhusu kijana aliyefeli sekondari lakini baada ya baba yake kumalizia ukarabati wa nyumba ya Mchungaji, alipokea barua ya kupata 'admision' chuo kikuu bila hata kurudia mitihani.

Wachungaji hawa hutumia 'miujiza na shuhuda feki' kama njia ya kuwafumba akili wafuasi wao. Kule Afrika kusini kuna Mchungaji alidanganya kufufua mtu. Hata alipoomba msamaha bado kuna waumini wanaendelea kumuamini na kumsujudu.

Wachungaji hawa wamegundua haya ndio mahubiri yanayopendwa sana huku Afrika. Hawataki kuhubiri kuhusu Aliko Dangote alivyoanza biashara na magumu aliyopitia.

Wanahubiri kuhusu mama Janeth aliyekua mama Ntilie huko Enugu, lakini alipotumia mtaji wake wote wa shilingi laki 5 kununua mafuta ya upako kwa Nabii fulani, ghafla biashara yake ikakua na sasa anamiliki mahoteli makubwa pande zote za nchi. Yani bila mtaji, bila business plan, bila timeline ghafla tu akamiliki mahoteli. Na waumini watashangia kwa kusema Ameen.

Aina hii ya ukristo imepanda mbegu ya uvivu wa kufikiri kwa vijana wengi wa Afrika ambao wanalazimishwa kumuona Mungu kama Mfadhili wa wavivu, au wasiostahili. Kwamba mwanafunzi hata asiposoma anajua akipewa mafuta ya upako atafaulu tu siku ya mtihani. Mfanyabiashara hata asipokua mbunifu anajua akienda kwa 'baba wa miujiza' biashara yake itapanuka ghafla bin vuu. Mfanyakazi hata asipowajibika kazini anajua akitoa fungu la kumi kwa 'Dokta Upako' atapanda cheo.

Kwa baadhi ya makanisa Africa namna pekee ya kufanikiwa ni kufanya kile wanachokiita kupanda mbegu, kupaka mafuta ya upako au kunyunyuziwa maji ya baraka. Eti wanaofanikiwa haraka ni watu 30 wa mwazo wanaokimbilia mbele ya kanisa kila mmoja akiwa ameshika noti ya dola 100.

Aina hii ya mahubiri inawafanya watu waamini kwamba Mungu hawapendi wanaojituma na kuwa wabunifu katika kazi, badala yake anawapenda zaidi wanaotoa zaka, sadaka, malimbuko na fungu la 10 hata kama ni wavivu. Hii sio sawa hata kidogo kwa sababu Biblia inakataa uvivu kwa nguvu zote ( *Mithali 12:27 Bali mtu mvivu hapiki Mawindo yake; Bali Mwenye bidii anazo mali za thamani).*
_
Watu wanaaminishwa kwamba ukishatoa sadaka kanisani unaweza kuamka kila siku asubuhi ukapayuka 'Mimi ni Milionea' halafu ukavuta shuka na kuendelea kulala fofofo, ukisubiri sadaka uliyotoa ikupe muujiza wa kuokota hela, ili upate mtaji wa biashara unayoiwaza.

Mtu huna kazi, huna biashara wala wazo la biashara, huna ujuzi, huna elimu, lakini kila siku unashinda kanisani kumsikiliza Mchungaji anayesema kesho utakua milionea na wewe unasema "Baba napokea/Dady I receive". Huu ni utani.

Waambieni wanaofanya utani huu kwa kofia za Uchungaji, Uaskofu, Unabii au Utume kwamba wanamkosea Mungu. Waambieni Mungu wetu ni Mungu wa kanuni, na hana kanuni ya kuwabariki wavivu. Tuache kufundisha waumini wetu kwamba uvivu unalipa kupitia miujiza.

Mafanikio ni matokeo ya bidii, ubunifu na weledi. Biblia inazungumzia kuhusu karama. Hebu kila mtu atumie karama alizopewa kwa bidii, ubunifu na weledi aone kama hatafanikiwa. Sio sahihi kuwaambia watu wabweteke tu na kusubiria mafanikio kama kusubiria daladala kituoni kwa sababu tu wamepakwa mafuta ya upako.

Mungu alishatubariki *tangu wakati wa uumbaji wetu. Ni wajibu wetu kujibidisha katika yale tufanyayo ili baraka zake ziambatane nasi ( *Kumb 28:6 Utabarikiwa uingiapo utabarikiwa na utokapo).*

Wazungu na Wachina wanazidi kushindana katika kuitawala dunia kwenye mambo mbalimbali kuanzia viwanda, biashara, sayansi na teknolojia. Sisi tuko 'busy' kununua maji ya upako tukiamini yatatufanya tuwe kama Jack Ma au Bill Gates. Upuuzi.

Tumeumbwa kuitawala hii dunia (Mwanzo 1:28Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini na ndege wa angani, na kila kiumbw chenye uhai kiendacho juu ya nchi). Tutumie vipawa na karama tulizopewa ili kutimiza kusudi hilo la Mungu. Tusiruhusu Askofu, Mchungaji, Nabii, mtume au kiongozi mwingine yeyote wa dini atutawale akili zetu kwa kutuhubiria mafanikio ya miujiza. Wao wanaishi kifahari kwa sadaka za waumini wao, huku waumini wakiendelea kuwa mafukara wa kutupwa.

Biblia inasema kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa ( *Mithali 1:7 Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu).* Tutafute maarifa, tufanye kazi kwa bidii, na tumuabudu Mungu katika Roho na kweli. Kwa kufanya hivyo tutapata MAFANIKIO katika mambo yote tuyafanyayo.

NB: Makala hii inazungumzia baadhi ya makanisa ya kilokole sio yote. Dont generalize. Yapo makanisa ya kilokole yenye misingi bora, lakini mengine yamejaa upotoshaji. Haya ndio yaliyozungumzwa hapa. Tafsiri isiyo rasmi imefanywa
na Malisa GJ.
Tukutane wiki ijayo panapo majaliwa.
Ni kweli kabisa mtoa mada walokole wa sikuizi wamekuwa kama wajinga au naweza sema misukule hawapo katika uwezo wao kamili au timamu wa kufanikisha au kuratibu mambo yao katika ubongo wao

Toa ubarikiwe!
Hakuna mahali kwenye biblia wameandika toa ubarikiwe lakini kuna mahali for wameandika toa kwa hiari yako na kutoa kwa hiari sio kushinikizwa na kutishwa kwamba usipotoa utalaaniwa huo ni ujanja wa wahuni tunamtolea MUNGU kwasabu ametubariki na sio kwasababu atupe vitu MUNGU sio betting umpe ili akupe vyote ni vyake ata ulivyo navyo pia ni vyake kwaiyo kwa swala la kutoa huangalia moyo wa mtu ambao unatoa shukrani kwa vichache ambavyo MUNGU amempa si kwa kutishwa au kulazimishwa kwa hiari yake mwenyew

2 Wakorintho 8:3 Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;

Watu walitoa kwa hiari na sio kwa kutishwa

Na hili limepelekea ujinga kabisa na watu wamekuw wavivu Yesu alifanya kazi mchana kutwa na bado usiku alikuwa anaenda kuomba
Walokole ujinga uwatoke yaani kazi wanakuwa wavivu ukitegemea miujiza nasema sahau hiyo miujiza maandiko yanasema kila mtu atavuna alicho panda

Kama ulipanda haba utavuna haba afu unaanza MUNGU mbona umeniacha MUNGU hajawai muacha mtu ,mtu ndiye anamuacha MUNGU

Uvivu piga kazi sana kwa nguvu zote kwanza MUNGU huwa hashughuliki na
Wavivu hata sikumoja acha uvivu piga kazi

Wagalatia 6:7 Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.
 
Makanisa mainstream ndio majizi orijino. Katoliki, Lutheran, Anglican na mengineyo... Tena haya ndio kichefuchefu zaidi kwani hupeleka huo mshiko wanaotuchukulia Rumi, Jeremani, Uingereza na kwingineko. Kwa kuwa wote ni wevi huwa nawaunga mkono hawa wajasiria dini wa kisasa kwani wamejiongeza na hukuza uchumi wa humu humu kwetu. Wameamua kuchukua fungu lao linalowaangukia...
Kanisa Katoliki kwa mfano, limewahi kupora, kutesa, kuua walioitwa 'wazushi', kushiriki biashara ya utumwa na zaidi kusaidia mataifa ya Ulaya ya Kikatoliki kueneza ukoloni Afrika, Asia na Amerika ya Kusini huku lenyewe likineemeka pakubwa kwenye 'uwekezaji' huo.
Sijui kama lilishawahi kuomba radhi kwa dhuluma kubwa ambazo limeifanyia ainabinadamu, na hata lijapoomba radhi, bado manufaa ya kiuchumi yaliyotokana na dhuluma hizo ndio msingi ambao kanisa limeegama kwa sasa.
Huu unaouita 'utumwa mpya' ni rasha rasha tu, mapichapicha yenyewe hasa yalikuwa na hadi sasa yako kwenye makanisa makongwe niliyoyataja hapo juu. Anza na hayo kwanza kisha ndio uje kuwashambulia wanangu wa faida walioiona fursa na kuamua kuchukua chao.
 
Chaajabu hata baadhi ya waislam wameanza mambo haya hasa kwa mbinu za nyota zilizo ibwa sijui....

all in all huu ni wizi wa wazi

Mambo ya nyota ni upuzi na ushikirikina. Wenye kuamini hayo watapata hukumu yao. Hakika ya Uislamu ni dini ya haki umejitenga mbali na machafu yote.
 
Back
Top Bottom