Utoaji wa Huduma za Afya Umezinduliwa Kwenye Hospitali Kuu ya Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,898
942

UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA UMEZINDULIWA KWENYE HOSPITAL KUU YA MUSOMA VIJIJINI

Leo, Jumanne, tarehe 9.8.2023, Mkuu wa Wilaya wa Musoma (DC), Dkt Khalifan Haule amezindua utoaji wa Huduma mbalimbali za Afya kwenye Hospitali ya Halmashauri yetu ya Wilaya ya Musoma (Musoma DC)

Hospitali imejengwa katikati ya Halmashauri yetu, kwenye Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti.

Hospitali hii yenye kutoa huduma za Afya kwa kiwango cha hadhi ya Hospitali ya Wilaya, hadi sasa Serikali imeishatoa Tsh bilioni 3.49 kwa ajili ya ujenzi, na Tsh milioni 600 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa.

Majengo muhimu tisa (9) yamekamilika, na majengo mengine sita (6) yanaendelea kujengwa likiwemo jengo la kufulia (laundry)

Hospitali ina vifaa vya kisasa, vikimemo: Digital X-ray, Ultrasound na Mitambo ya kutengeneza Oxygen ambayo inapelekwa sehemu ya matibabu kupitia mtandao wa paipu.

Mitungi ya Oxygen ipo ikiwa ni kwa matumizi ya dharura au kusaidia mahitaji ya hospitali nyingine, vituo vya afya na zahanati.

Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wamehudhuria uzinduzi huo. Chama kiliongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha CCM Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Denis Ekwabi. Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo alishiriki kwenye uzinduzi huo.

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa kutoka kwenye tukio la uzinduzi wa huduma za Afya kwenye Hospitali kuu ya Musoma Vijijini.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumanne, 9.8.2023
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2023-08-10 at 06.16.35.mp4
    19.6 MB
Back
Top Bottom