Utenzi-nyerere nakulilia

IsangulaKG

JF-Expert Member
Oct 14, 2010
706
386
Source: http://sautizetutz.blogspot.com/2011/10/nyerere-nakulilia.htmlhttps://www.facebook.com/groups/sautizetutz/

NYERERE NAKULILIA!

Nyerere unanisikia?
Machozi nakulilia
Nchi ulopigania
Uhuru Kutuachia.

Nchi ulopigania
Ukajenga Historia
Vigogo ukawachia
Tumebaki tukilia

Ufisadi, umezidia
Na uchafu kupindukia
Mali wajilimbikia
Mafukara tunalia

Mafukara tunalia
Twaililia Tanzania
Nini wanafurahia?
Kama wengi tunalia?

Kwa mbebwe,uongo pia
Bungeni wakaingia
Nini wametufanyia?
Kama vile si raia!

Mikataba kusainia
As if hawana nia
Sisi kutusaidia
Nyerere nakulilia

Kuna Haja Tanzania
Kutafuta zote njia
Fisadi, wababe pia
Kila njia kutumia

Kila njia kutumia
Siyo tu kulialia
Haki yetu kutumia
Kuichange Tanzania!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom