Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Baada ya Gazeti la Jamhuri kujaribu kumtakasa mtuhumiwa wa utekaji nyara wa Dr. Ulimboka, ACP Ahmed Msangi,
- Tunaomba serikali itoe maelezo kwa nini mtuhumiwa mkuu ashiriki kwenye tume ya uchunguzi katika tuhuma zinazomkabili
- Huyu mtu ana tuhuma nzito ndani ya jeshi la polisi na viongozi wakuu akiwemo IGP wanalifahamu hilo iweje apewe mamlaka ya kutafuta wahalifu wakati yeye ni mhalifu namba moja (nasema mhalifu kwa maana waraka unaonyesha alikubali kwamba yeye ni mhalifu na akaomba msamaha)
- Tunaiomba serikali itoe maelezo kuhusu hizi nyaraka ambazo wakuu wa polisi na usalama wa taifa wanazo zinazomshutumu Ahmed Msangi kuwa mhalifu tena wa ujambazi
- Tunaomba serikali itupe maelezo ya usalama wa raia wake kwani mtu anatekwa, kwa kusudi la kumuua, washukiwa wanatajwa lakini hatua zozote hazichukuliwi dhidi ya washukiwa. Wiki inaisha serikali kimya. Tunaomba majibu
- Tafadhali msifumbie macho haya maswala ya msingi kwani yana uzito. hizi siyo uzushi ni malalamiko ya kweli ya raia waliowengi. Tunaomba msiwashinikize MODs kuondoa hii thread. Kwani raia na sisi wana CCM tunaomba majibu yatolewe