Nasubiri 9december kusikia wimbo wa taifa utaimbwaje maana tz haina miaka 50. Sina ugomvi na ndugu zetu wazanzibar,ila linapoja swala utaifa naona kama wanajitenga.Kama uzanzibar basi uwepo UTANGANYIKA. Maana naona wimbo wa tanzania bara na tanzania visini umeshindwa kuimbika.Penye uzanzibar kuwepo UTANGANYIKA.Kwenye tanznia hakuna kitu kinachoitwa zanzibar,kuna tanzania visiwani. Na kwa nini zanzibar kusiwepo TANGANYIKA.Siamini kwenye selikari tatu maana itakua mzigo kwa taifa.Viongozi wetu waaje ghirba maana kwenye huu mungano unawanufaisha wao,ususani viongozi wa zanzibar. Ndiyo maana ukiongelea selikari moja wanaku
a wakali eti zanzibar aiwezwi kumezwa ni nchi kamili.Hivi TANGANYIKA sio inchi kamili? Na vile TANGANYIKA hatuna viongozi,zanzibar wavunja katiba viongozi wa tanzania wako kimya maana wanaogopa kuwanyoshea vidole.Nani kakwambia sultan anyoshewa kidole? Lazima tutambue kwenye wao kuna sisi.Wao wana wimbo wa taifa,sisi hatuna.Wao wana bendera taifa sisi hatuna.Kweli wimbo wa tanzania bara na tanzania visiwani unaimbika?au tumebaki majuha ndiyo tunaitikia,kiitikio bila kujua beti za wimbo zinaimbwaje? Imefika mida tuache unafki wanapozungumzia uzanzibar na UTANGANYIKA sio dhambi kama wanazungumza.Ila nitaendelea kusisitiza siamini kwenye selikari tatu,naana ni mzigo kwa wananchi .Najua kwa selikari moja kwa viongozi wa zanzibar litakua gumu maana hawana masrai nalo.Huu mungano naona ni mzigo kwa kiumbe alioubeba,mzigo unaoneka unakwenda ila mtu alio beba haonekani. Najua huyo kiumbe siku ya kuchoka kubeba huu mzigo wa mungano atajitokeza.''Bandugu heri ya 9december''