Utata wa dini kongwe na jinai mbaya ya utumwa. Je, Mungu ameonyesha ishara zake kupitia Uislam?

Watu wa mfano wa Bwana Kiranga hata kama laiti Mungu angeliumba ulimwengu anayeutaka bwana Kiranga basi yeye na mfano wa watu wa kama yeye wangelimpinga Mungu wazi wazi kabisa. Kwa sababu tungelikuwa hatuna mapungufu, tungelijiona tumekamilika. Rejelea watu wa Qaumu Aad, walimwambiaje Mtume wao Hud a.s walivyopewa uwezo unaofanana anaoutaka bwana Kiranga.

Walimwambia Hud a.s " Man ash' shaddu minna quwa" Ni nani mwenye nguvu kuliko sisi? Tumekamilika sisi Hud, utatuambia nini? Kuhusu Mungu? Fanya unayotaka kuyafanya wewe pamoja na huyo Mungu wako. Lakini usichoke kumpa darasa, inawezekana akabadilika na akawa anapendeza zaidi kwa Mungu kuliko sisi wenyewe.


yeye yupo kinyume na 'mungu kuumba ulimwengu' kwaio kama unataka kutolea mfano uelewa wake uanze kwa kusema galaxy yetu ni kichembe kati ya zaidi ya galaxy bilioni 200,ambamo ndani ya hicho kichembe kilicho galaxy yetu kuna nyota zaidi ya bilioni 200 ambazo zina mvutano na vitu vingine vinavyo zizunguka kama jua letu, na kwaio kuna sayari infinite numbers abazo hatujaweza fanya research kama kuna kiumbe hai sababu technolojia ya sasa kutofikia huo uwezo, hivyo, huyo mungu unaemsema kakuumba anaesikiliza shida za kichembe ndani ya kichembe ndani ya kichembe cha sehemu ya ulimwengu usio na mwisho na unaoleta mantiki kwa kutumia principles forces za physics
kwamba mungu nisaidie kesho nipate chakula,sijui unilinde, bla bla blaa hayupo. ukianza kwa kutambua hilo ndipo unaweza weka hoja yako kuhusu mungu
 
Mfano mmoja wapo kuna hili la uwepo
wa hawa watoto wa
ajabu ambao huitwa SHARIF. Binafsi nimekua na nimeweza
kushuhudia mmoja wa
watoto hawa wa ajabu.
Akina Sharif huwa ni watoto wa ajabu ambao
huzaliwa na karama ya kujua
mambo mengi ya kidunia na kidini ktk namna ya
ajabu kabisa. Na wengi
kama si wote huzaliwa ktk familia za kikristo na
hulia sana
wakiongozona na wazazi wao kuelekea kanisani. Nukta hii hunifikirisha sana.
HAWA WATOTO WAPO ILA NI WATOTO TU AMBAO WANAZALIWA NA UWEZO MKUBWA WA AKILI...KWA AKILI ZILE WAKIELEKEZWA POPOTE WANAFIT....yaani endapo akielekezwa kwenye masomo ya shule atafit na alielekezwa kwenye dini pia atafiti...

tatizo la hawa watoto ni kwa hawa wanaojiita wahadhiri wanawafanya kama dili na ndio maana watoto hao wanaishia kwenye kuuza maji kwa udanganyifu..

ilipaswa watoto hao wachukuliwe na wafundishwe dini kisawa sawa pamoja na sekula believe me tunaweza kuwa na mashekh makini saana tofauti na hawa wazugaji zugaji 2
 
Kuhusu aina hii ya watoto ipo tofauti kidogo mdugu. Hawa si kuwa ni jitihada za mzazi HAPANA. Huzaliwa wakiwa wenye kuhubiri na kuijua Quran bila hata ya kufundishwa.

hii kitu sio kweeli kabisa kwa mujibu wa dini ya kiislamu ( uislamu ni dini ya asili dini ya kimaumbile) katika nature binaadamu lazima afundishwe ndo ajue..ingekuwa hivyoo muhammad angekuwa wa aina hiyo..ila muhammad alifundishwa na aliminywa hasa pindi alipokuwa anafundishwa kwa mara ya kwanza.
 
Mleta Mada unaamini katka kuona Maajabu. na vituko, unajuaje hayo yametoka kwa MUNGU? Quran haisemi muamini maajabu!! km kifungu kipo weka hapa tuone!

ONgea na Mungu Akupe kilicho sahihi, siyo kuona au kusikia Majaabu, mimi ni muislamu, niliwahi ona Adhana inapigwa Mwezini wakati wataalamu wameenda huko na wakairekodi!!! Niliwahi kuona kuku ana anatamka Bismilah! nilimkomesha na hakurudia tena, nilimkomeshaje hiyo ni story nyingine!
 
Mkuu edwayne. Mimi nimeyashuhudia maajabu haya kwa macho yangu. Kama pia unamjua yule anayeitwa Said John aliyezaliwa Arusha. Fuatilia kisa chake na utaona mambo mengi yenye kushangaza.
Hiko kitu hakiwezekani.. Sasa ataongea lugha ipi
 
Ndugu yangu kumbe bado upo gizani kabisa na haujui jinsi mambo ambavyo yanavyo endeshwa duniani pole sana dahhh

Nimetamani uijue dunia jinsi inavyo endeshwa but itoshe tu kukueleza kwamba hao watoto masharifu uliowataja hawapo ile Ni Hoax tu ...Ili nimipango ya upigaji najua sasa hivi haiwezi kunielewa lakini chunguza vyema utabaini hilo
 
Mkuu edwayne. Mimi nimeyashuhudia maajabu haya kwa macho yangu. Kama pia unamjua yule anayeitwa Said John aliyezaliwa Arusha. Fuatilia kisa chake na utaona mambo mengi yenye kushangaza.
Wale wote Ni scam .. hakuna shekhe sharifu Kama namna ambavyo jamii huwa inaaminishwa ile Ni michezo jombaa
 
Mleta mada unasukumwa na hisia ! Hili la Mosjhi lilivuma mie niko huko lakini ilikuwa ni uvumi mtupu usio na kweli kabisa!
Hawa vijana unaosema wanaitwa 'masharifu' mbona huwa wanafanya shughuli za uganga na uuguzi hadi ramli?
Endelea kuamini ktk dini yako bali achana na mambo ya uvumi!
 
Habari wanajamvi,

Kwa muda mrefu nimekua nikitatizwa na jambo la
imani kwa upande wa
dini hizi mbili za uislam na ukristo. Awali ya yote
ningependa
kueleweka kuwa nimezaliwa ktk familia ya kiislam.
Ningependa ku-stress
hapo kuwa sote tumejikuta ktk imani tulizonazo
baada ya kuzaliwa na
wazazi wenye imani husika.

Nirudi ktk lengo langu la uandishi. Binafsi, kuna
wakati niliwahi
kutatizwa na uwepo wa Mungu. Lakini kwa sasa
niweke wazi nakiri Mungu
yupo na ninaamini ana adhabu zake kwa wale
wanaowafanyia wengine
mabaya hapa ulimwenguni(nadhani hili linajibu hoja
ya wengi kwanini
Mungu atuadhibu anafaidika na nini?)

Utata wangu uliobaki kwa sasa ni juu ya ipi ni imani
ya kweli kati ya
UISLAM na UKRISTO dini ambazo zote zimekua
binafsi zikinitatiza hasa
ninapofanya kunasabaisha na historia mbaya ya mtu
mweusi hapa duniani.
Ni wazi dini hizi mbili zina historia mbaya au zina
nasaba ya moja kwa
moja na jinai mbaya tuliyowahi kufanyiwa waafrika
ya utumwa. Ni wazi
wamisionari walichangia pakubwa ktk kudhibiti na
kufanikisha ukoloni
kwa watu weusi hali ya kuwa wakijua kufanya hivyo
ni kumkosea Mungu na
watu weusi. Hivyohivyo mathalani tumewahi kusikia
mfano wa kikundi
kinachoitwa JANJAWEED cha waislam waarab wa
Sudan ambao wamekua wakiua
waislam
weusi kwa mrengo wa kibaguzi dhidi ya watu weusi.
Na mbaya zaidi jinai
hizi wamekua wakifanya kwa kujumuisha kuchoma
kitabu cha Qur'an
ambacho wao pia hukiamini na kukitumia. (Refer
Darfur Genocide for
clarifications)

Lakini hapo hapo huwa natatizwa na jambo moja
ambalo ndio hasa
ningependa tulijadili wanajamvi. Binafsi nimekua na
imani kubwa juu ya
uislam kuliko ukristo kwa kuangalia nukta kadhaa
ambazo zimekua
zikinifikirisha. Huwa ninaona kuna mambo mengi
ambayo Mungu amekua
akidhihirisha kupitia uislam na kufanya akili kufikiri
zaidi.
Mambo hayo yamejikita ktk maajabu ambayo
naamini wengi wenu mmewahi
kusikia na kushuhudia pengine. Nitaenda haraka haraka.

Mfano mmoja wapo kuna hili la uwepo
wa hawa watoto wa
ajabu ambao huitwa SHARIF. Binafsi nimekua na nimeweza
kushuhudia mmoja wa
watoto hawa wa ajabu.
Akina Sharif huwa ni watoto wa ajabu ambao
huzaliwa na karama ya kujua
mambo mengi ya kidunia na kidini ktk namna ya
ajabu kabisa. Na wengi
kama si wote huzaliwa ktk familia za kikristo na
hulia sana
wakiongozona na wazazi wao kuelekea kanisani. Nukta hii hunifikirisha sana.

Watoto aina hii
hufurahi na kulilia
kwenda msikitini. Maajabu ni mengi juu ya watoto
wa namna hii. Nimeorodhesha ajabu moja kati ya mengi.
Maajabu mengine nakumbuka zamani kidogo
niliwahi kusoma kwenye gazeti
la Alasiri juu ya binti aliyegeuka mnyama wa ajabu
kabisa baada ya
kupiga teke Quran aliokua anaisoma
mama yake. Licha ya juhudi za kumuombea yule
binti hakubadilika,
nafikiri picha za huyo binti mpaka hivi leo zipo.

Kisa kingine ni cha mbuzi aliyezaliwa na maandishi
ya aya za Quran
ubavuni huko Moshi. Pia kuna mtoto alizaliwa Urusi
kama sijakosea
ambaye alikua na maandishi ya Quran mwili mzima.

Kiukweli ni maajabu
mengi kati ya haya machache ambayo binafsi
yamekua yakinifikirisha
kiukweli na kujiuliza maswali mengi sana.

Kwanza najaribu kumuangalia mtu mweusi na
historia yake hapa
ulimwenguni dhidi ya dini hizi mbili kongwe. Kisha
natazama maajabu
haya yanayotokea yakiakisi dini ya Uislam na kubaki
na maswali yasiyo
na majibu. Naomba tujadili juu ya hili la maajabu ya
Mungu kwa kutoa
ishara hizi. Je, ni kweli Mungu anatoa ishara kudhihirisha Uislam kuwa njia ya kweli? Wewe binafsi mchangiaji una nini la kuongeza au una mtazamo gani juu ya haya machache niliyoandika?

Naomba waungwana tujadili kwa fikra huru bila
matusi wala kejeli. Kama huamini uwepo wa Mungu ni vema kuacha kuchangia chochote bali kutazama mjadala.

Huenda kama kuna litakalotuponza na kutupa adhabu kubwa mbele za Mungu ni kejeli na matusi dhidi ya imani za wengine kwa
kuona imani yako ni
bora kuliko ya mwengine na wakati huohuo kumtolea
hukumu mtu mwingine kwa sababu tu ya tofauti zenu za kiimani. Nimejaribu kuandika kwa mjumuisho lakini bila shaka maudhui ni yenye kueleweka.


Nawasilisha.

Mimi ninachoona Makala yako wala haivutii zaidi ya kuonesha ni jinsi gani bado Upo kwenye CAGE.

Kila ulichoandika hapo ni CLAIMS, wala hakuna kitu hapo ambacho I can check to verify what you have just put forth.

Hey, what about that public servant ( Mtumishi wa Umma) aloyekojolea Quran JPM akaamrisha Afukuzwe kazi .

Hivi unahabari kwa sasa yule kijana ni Senior Officer katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro?

Sasa punguza fantasy basi uishike imani yako vyema; usitumie muda wako kuonesha imani yako ina make sense Na za wengine hazi make sense. Ni ukosefu wa Maturity.

Sijui kama unajua Duniani kuna Imani zaid ya Uislam Na Ukristo.
 
Back
Top Bottom