Kuna jambo huwa najiuliza sana kila wakati nikwa natafakari hili tukio.Mke wa rais aliwezaje kukurupuka na kulifuata fuvu la mumewe nyuma ya gari wakati mumewe amepigwa risasi?
Hebu fikiria tu hili tukio lilivyotokea kwa haraka halafu mtu aweze kurukia kipande cha fuvu la mumewe ilhali kukiwa na taharuki na pengine katika mazingira ya kawaida usingeweza kujua kilichotokea maana ni matukio ya haraka sana na katika hali ya kawaida tu ni lazima mshangao na mshtuko ungechukua nafasi kabla ya kujua kuwa mtu ameshambuliwa....
Halafu aliyefanya hivi ni mwanamke......
Ni jambo gumu sana kutokea hili na nachelea kusema kuwa kulikuwa na jambo zito kuliko hata tunaloliona kwenye nyaraka mbali mbali za tukio hili....
Nimefuatilia jambo hili sana tu na pamoja na nyaraka nilizowahi kuziona bado naziona zimepunguwa sana tena sana tu ili kuelezea tukio hili maana ni vigumu sana mambo mengi kutokea....
Mpiga picha ya video aliwezaje kuwaona polisi wakikimbilia eneo alilolitaja halafu hapo hapo aendelee kurekodi tukio hili? Kuna mambo ni magumu sana kuyaelewa...
Pamoja na yote hayo,ninajua [siyo kuamini] kuwa wote hao waliouawa na maafisa wa serikali wanajuwa kilichokuwa kinatokea....
Nashindwa kuamini kuwa Zhapruder pekee ndiyr aliyekuwa na kamera eneo hilo,kuna mengi zaidi na tukio hili ni miongoni mwa matukio tata zaidi kuwahi kutokea....
The bold ,kwa mara nyingine hongera sana kwa kuwajulisha wengine wasiokuwa wakielewa juu ya mengi kuhusu jambo hili.....
Pamoja sana mkuu.....