Utapeli wa Mtandaoni kwa kisingizio cha mapenzi

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
20210225_110553_0000.png


Matapeli huko mtandaoni hutengeneza wasifu bandia kwenye tovuti halali za kutafuta wachumba. Wanatumia profaili hizi kujaribu kuingia kwenye uhusiano na mtu ili waweze kupata pesa zake na maelezo binafsi.

Tapeli atakuwa na uhusiano mzuri na mtu huyo wakishazoeana ataanza kuombe pesa ili kusaidia kulipia gharama zinazohusiana na ugonjwa, kuumia, kusafiri au shida ya familia.

Matapeli huwa wanachanganya kihisia kwa kuvuta moyo wa mtu. Wakati mwingine huwa wanatumia mda mrefu sana ili kumjengea mtu uaminifu na wakishajiridhisha kuwa wameshamteka na anawaamini ndipo wanafanya utapeli na kuondoka.

Hivyo ni vyema ukawa makini unapowasiliana na mtu usiyemjua. Usimtumie pesa mpaka uwe umekutana naye ana kwa ana na kumuelewa vizuri.
 
Wengi wao ngoma sawa, unajikuta unamtapeli tapeli😅😅😅😅😅
 
Hii inatokana na changamoto ya kichwa Cha juu kuelemewa na kichwa Cha chini.
 
Mtoa mada umeenda mbali,
Hata uku mitaani tunatapeliwa Sana TU kwa kisingizio Cha Mahusiano.

Sema wengi hawasemi, au hawajui Kama wanatapeliwa.

Mwanaume unakua na binti kwny mahusiano anakugeuza mzazi wake na shida zake zote anakubwagia wewe.

Mwanamke hakuingizii hata mia.
unamgaharamia kuanzia malazi,mavazi, maradhi mpaka starehe zake.

Ukiangalia yeye anacho ofa kwenye mahusiano Ayo Ni PAPUCHI yake tu.

Afu kwa sababu zisizo na msingi, kesho kutwa anakuacha na kwenda kwa mwingine.

Nasema
Huo nao Ni utapeli mwingine Kama utapeli mwingine.

Hapa
Serikali inapaswa iingilie kati,
ikiwezekana siku mwanamke akitamka TUACHANE, Basi mwanaume arudishiwe gharama zao.

Kiukweli,
Hali Ikiachwa iendelee, inakua Ni sawa na kesi ya kujipatia Mali kwa njia za udanganyifu.

Na Kama taifa, hasa kipind hiki Cha UCHUMI wa KATI.
Tutakua tunatengeza TAIFA la ovyo kabisa la matapeli na wapiga dili.
 
  • Thanks
Reactions: Atn
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom