Utapeli kwenye makanisa

hamis77

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,642
19,018
Niliambiwa na ndugu mmoja kanisani kwetu aliyetokea Zambia, kwamba nchini kwao waganga wa kienyeji huacha uchawi vijijini na kwenda kuwa wachungaji wa makanisa katika miji na majiji, nao husema eti unaweza kupata pesa nyingi ukiwa mchungaji mjini kuliko kuwa mganga wa kienyeji kijijini kwa kuwa kule mjini unatumia nguvu zile zile za kichawi kana kwamba ni nguvu za Mungu kufanya miujiza na kuponya au kuokoa!

Matendo ya mitume sura ya 8 inatufundisha kuwa tamaa ya kutumia miujiza ili kupata pesa inatokana na tamaduni za kichawi.

Simoni alikuwa mchawi, lakini mara baada ya kusikia habari njema ikihubiriwa na Filipo, alibatizwa. Lakini alipoona ya kuwa watu wanapokea karama ya Roho Mtakatifu kwa kuombewa na mtume Petro, naye alitamani kupata uwezo huo, ndipo akatoa PESA kumpa Petro akisema, “Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu.” (Matendo 8:19).

Simoni alikuwa bado hajatubu kwa kweli, ule uchawi wake wa zamani. Alikuwa bado anataka kuwa na nguvu za kutenda miujiza ili kuwavutia watu, na kujipatia pesa!

Jibu la Petro ni onyo kwetu sote,

“Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.” (Matendo 8:20).

Maneno haya aliambiwa nani? Aliambiwa mtu yule ambaye aliyekuwa anatenda mambo ya kichawi, na ambaye sasa alikuwa anajaribu kuingiza tamaduni na fikra za kichawi kanisani!

Iwapo muhubiri yeyote yule akijaribu KUKUUZIA wewe chumvi, maji ya upako, au kitambaa, akidai kuwa vitu hivyo ndivyo vitakuletea baraka na uponyaji au mafanikio, basi mtu huyo atakuwa anajiweka yeye mwenyewe kwenye eneo lenye hatari sana. Ikiwa na wewe utalipa pesa zako ili KUNUNUA uongo wa vituko kama hivyo, ndipo na wewe utakuwa umejiweka mwenyewe katika eneo la hatari pia. Biblia inatupatia maonyo yenye kutuokoa na yenye usalama kutokana na mwenendo mbaya huo na mtazamo wa kiuchawi kama huo pale Petro anapomwambia Simoni,

“Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.”

Hebu basi fikiri na ujiulize wewe mwenyewe, NI SEHEMU GANI katika Agano Jipya au hata ndani ya Biblia nzima ambapo alitokea mtu kumlipa mtumishi wa Mungu pesa ili apokee uponyaji au baraka? Jawabu la swali hili ni wazi kwamba hakuna popote pale! Hakuna kitu kama hiki kinachofundishwa na Biblia. Na kwa sababu hiyo basi yakupasa moja kwa moja kukataa fundisho hili na vitendo vyake wanavyofanya!

“Na katika kutamani watajipatia faida (yaani, pesa) kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii.” (2 Petro 2:3).

Tayari wengi wamehamia kwenye kutukuza maji ya upako, mafuta ya upako, sabuni za upako, chumvi ya upako, vitambaa na nguo za upako na kila aina ya vitu vya upako mpaka kanisa linaonekana kama kituo cha waganga wa kienyeji maana mambo ambayo tunaelekezwa kanisani sasa hayana tofauti kabisa na mambo ambayo watu wanaambiwa wakienda kwa waganga wa kienyeji.

Yesu alisema, “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; MMEPATA BURE, TOENI BURE.” (Mathayo 10:8).

Ushuhuda wa Paulo ulikuwa ufuatao:

“SIKUTAMANI FEDHA WALA DHAHABU, WALA MAVAZI YA MTU. Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, NI HERI KUTOA KULIKO KUPOKEA.” (Matendo 20:33,35).

maxresdefault.jpg


download.jpg
 
Niliambiwa na ndugu mmoja kanisani kwetu aliyetokea Zambia, kwamba nchini kwao waganga wa kienyeji huacha uchawi vijijini na kwenda kuwa wachungaji wa makanisa katika miji na majiji, nao husema eti unaweza kupata pesa nyingi ukiwa mchungaji mjini kuliko kuwa mganga wa kienyeji kijijini kwa kuwa kule mjini unatumia nguvu zile zile za kichawi kana kwamba ni nguvu za Mungu kufanya miujiza na kuponya au kuokoa!

Matendo ya mitume sura ya 8 inatufundisha kuwa tamaa ya kutumia miujiza ili kupata pesa inatokana na tamaduni za kichawi.

Simoni alikuwa mchawi, lakini mara baada ya kusikia habari njema ikihubiriwa na Filipo, alibatizwa. Lakini alipoona ya kuwa watu wanapokea karama ya Roho Mtakatifu kwa kuombewa na mtume Petro, naye alitamani kupata uwezo huo, ndipo akatoa PESA kumpa Petro akisema, “Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu.” (Matendo 8:19).

Simoni alikuwa bado hajatubu kwa kweli, ule uchawi wake wa zamani. Alikuwa bado anataka kuwa na nguvu za kutenda miujiza ili kuwavutia watu, na kujipatia pesa!

Jibu la Petro ni onyo kwetu sote,

“Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.” (Matendo 8:20).

Maneno haya aliambiwa nani? Aliambiwa mtu yule ambaye aliyekuwa anatenda mambo ya kichawi, na ambaye sasa alikuwa anajaribu kuingiza tamaduni na fikra za kichawi kanisani!

Iwapo muhubiri yeyote yule akijaribu KUKUUZIA wewe chumvi, maji ya upako, au kitambaa, akidai kuwa vitu hivyo ndivyo vitakuletea baraka na uponyaji au mafanikio, basi mtu huyo atakuwa anajiweka yeye mwenyewe kwenye eneo lenye hatari sana. Ikiwa na wewe utalipa pesa zako ili KUNUNUA uongo wa vituko kama hivyo, ndipo na wewe utakuwa umejiweka mwenyewe katika eneo la hatari pia. Biblia inatupatia maonyo yenye kutuokoa na yenye usalama kutokana na mwenendo mbaya huo na mtazamo wa kiuchawi kama huo pale Petro anapomwambia Simoni,

“Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.”

Hebu basi fikiri na ujiulize wewe mwenyewe, NI SEHEMU GANI katika Agano Jipya au hata ndani ya Biblia nzima ambapo alitokea mtu kumlipa mtumishi wa Mungu pesa ili apokee uponyaji au baraka? Jawabu la swali hili ni wazi kwamba hakuna popote pale! Hakuna kitu kama hiki kinachofundishwa na Biblia. Na kwa sababu hiyo basi yakupasa moja kwa moja kukataa fundisho hili na vitendo vyake wanavyofanya!

“Na katika kutamani watajipatia faida (yaani, pesa) kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii.” (2 Petro 2:3).

Tayari wengi wamehamia kwenye kutukuza maji ya upako, mafuta ya upako, sabuni za upako, chumvi ya upako, vitambaa na nguo za upako na kila aina ya vitu vya upako mpaka kanisa linaonekana kama kituo cha waganga wa kienyeji maana mambo ambayo tunaelekezwa kanisani sasa hayana tofauti kabisa na mambo ambayo watu wanaambiwa wakienda kwa waganga wa kienyeji.

Yesu alisema, “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; MMEPATA BURE, TOENI BURE.” (Mathayo 10:8).

Ushuhuda wa Paulo ulikuwa ufuatao:

“SIKUTAMANI FEDHA WALA DHAHABU, WALA MAVAZI YA MTU. Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, NI HERI KUTOA KULIKO KUPOKEA.” (Matendo 20:33,35).

View attachment 1725065

View attachment 1725066
Hapa nailaumu serikali,hususani wizara ya Elimu,utamaduni na Idara za ustawi wa jamii kwa kuacha mambo maovu kama haya yaendelee,
 
Siku hizi mengi ya haya makanisa yanayojiita ya kiroho yamegeuka biashara za watu, hadi watu wana brand hayo makanisa na huduma majina yao, utasikia mimi nasali kwa mchungaji fulani na fulani, naabudu kwa nabii na mtume fulani. Kwa hiyo utaona hayo makanisa na huduma zimekuwa mali binafsi za watu na siyo mali ya Yesu. Wanapigana vijembe kwa ajili ya kuvuta waumini waondoke kwa huyu kwenda kwa huyu. Ndo maana kwenye huu usanii utakuta wanawake ndo wamejaa maana ni rahisi kuwashikia akili....na wamesababisha kuvuruga ndoa na mahusiano maana mke anamsikiliza zaidi mchungaji kuliko mme wake na anakwapua pesa kwa ajili ya matumizi ya familia kupeleka sadaka kwa mchungaji bila kumtaarifu mume.
 
Siku zote kufuata dini bila elimu ndio madhara yake hayo. Ukristo ni dini isiyo na elimu, hakuna msingi wowote mtu anapaswa asome ili afanye ibada yake ipasavyo. Ndio maana wanaishia kukufuru, kutapeliwa kirahisi kuliko dini/imani zingine ambazo ndani yake kusoma dini na kufanya ibada ni lazima. Alhamdulillah uislamu umetupilia mbali shuhba hizo na hata akijitokeza mjinga akajaribu kudanganya watu basi hupotea haraka maana baatwil haidumu. Karibu katika dini ya haki achaneni ni kufru hizo.
 
Siku zote kufuata dini bila elimu ndio madhara yake hayo. Ukristo ni dini isiyo na elimu, hakuna msingi wowote mtu anapaswa asome ili afanye ibada yake ipasavyo. Ndio maana wanaishia kukufuru, kutapeliwa kirahisi kuliko dini/imani zingine ambazo ndani yake kusoma dini na kufanya ibada ni lazima. Alhamdulillah uislamu umetupilia mbali shuhba hizo na hata akijitokeza mjinga akajaribu kudanganya watu basi hupotea haraka maana baatwil haidumu. Karibu katika dini ya haki achaneni ni kufru hizo.
Mkuu, waislamu wana elimu gani kuzidi wakristo, hapa yanaongelewa makanisa siyo misikiti. Usije ukaharibu huu mjadala mkakimbilia kushika majambia kwamba dini ya mtume imekashfiwa...nafikiri huu mjadala unawahusu zaidi wanaofuata ukristo, ndo maana mleta bandiko amerejea vifungu na maandiko ambayo yamo kwenye biblia takatifu kukazia hoja yake, tafadhali sana..
 
Mkuu, waislamu wana elimu gani kuzidi wakristo, hapa yanaongelewa makanisa siyo misikiti. Usije ukaharibu huu mjadala mkakimbilia kushika majambia kwamba dini ya mtume imekashfiwa...nafikiri huu mjadala unawahusu zaidi wanaofuata ukristo, ndo maana mleta bandiko amerejea vifungu na maandiko ambayo yamo kwenye biblia takatifu kukazia hoja yake, tafadhali sana..
Achana naye huyo. Nashangaa kuwa hata heading hakuisoma! Na huko ndo kutokusoma kwenyewe.
 
Niliambiwa na ndugu mmoja kanisani kwetu aliyetokea Zambia, kwamba nchini kwao waganga wa kienyeji huacha uchawi vijijini na kwenda kuwa wachungaji wa makanisa katika miji na majiji, nao husema eti unaweza kupata pesa nyingi ukiwa mchungaji mjini kuliko kuwa mganga wa kienyeji kijijini kwa kuwa kule mjini unatumia nguvu zile zile za kichawi kana kwamba ni nguvu za Mungu kufanya miujiza na kuponya au kuokoa!

Matendo ya mitume sura ya 8 inatufundisha kuwa tamaa ya kutumia miujiza ili kupata pesa inatokana na tamaduni za kichawi.

Simoni alikuwa mchawi, lakini mara baada ya kusikia habari njema ikihubiriwa na Filipo, alibatizwa. Lakini alipoona ya kuwa watu wanapokea karama ya Roho Mtakatifu kwa kuombewa na mtume Petro, naye alitamani kupata uwezo huo, ndipo akatoa PESA kumpa Petro akisema, “Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu.” (Matendo 8:19).

Simoni alikuwa bado hajatubu kwa kweli, ule uchawi wake wa zamani. Alikuwa bado anataka kuwa na nguvu za kutenda miujiza ili kuwavutia watu, na kujipatia pesa!

Jibu la Petro ni onyo kwetu sote,

“Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.” (Matendo 8:20).

Maneno haya aliambiwa nani? Aliambiwa mtu yule ambaye aliyekuwa anatenda mambo ya kichawi, na ambaye sasa alikuwa anajaribu kuingiza tamaduni na fikra za kichawi kanisani!

Iwapo muhubiri yeyote yule akijaribu KUKUUZIA wewe chumvi, maji ya upako, au kitambaa, akidai kuwa vitu hivyo ndivyo vitakuletea baraka na uponyaji au mafanikio, basi mtu huyo atakuwa anajiweka yeye mwenyewe kwenye eneo lenye hatari sana. Ikiwa na wewe utalipa pesa zako ili KUNUNUA uongo wa vituko kama hivyo, ndipo na wewe utakuwa umejiweka mwenyewe katika eneo la hatari pia. Biblia inatupatia maonyo yenye kutuokoa na yenye usalama kutokana na mwenendo mbaya huo na mtazamo wa kiuchawi kama huo pale Petro anapomwambia Simoni,

“Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.”

Hebu basi fikiri na ujiulize wewe mwenyewe, NI SEHEMU GANI katika Agano Jipya au hata ndani ya Biblia nzima ambapo alitokea mtu kumlipa mtumishi wa Mungu pesa ili apokee uponyaji au baraka? Jawabu la swali hili ni wazi kwamba hakuna popote pale! Hakuna kitu kama hiki kinachofundishwa na Biblia. Na kwa sababu hiyo basi yakupasa moja kwa moja kukataa fundisho hili na vitendo vyake wanavyofanya!

“Na katika kutamani watajipatia faida (yaani, pesa) kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii.” (2 Petro 2:3).

Tayari wengi wamehamia kwenye kutukuza maji ya upako, mafuta ya upako, sabuni za upako, chumvi ya upako, vitambaa na nguo za upako na kila aina ya vitu vya upako mpaka kanisa linaonekana kama kituo cha waganga wa kienyeji maana mambo ambayo tunaelekezwa kanisani sasa hayana tofauti kabisa na mambo ambayo watu wanaambiwa wakienda kwa waganga wa kienyeji.

Yesu alisema, “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; MMEPATA BURE, TOENI BURE.” (Mathayo 10:8).

Ushuhuda wa Paulo ulikuwa ufuatao:

“SIKUTAMANI FEDHA WALA DHAHABU, WALA MAVAZI YA MTU. Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, NI HERI KUTOA KULIKO KUPOKEA.” (Matendo 20:33,35).

View attachment 1725065

View attachment 1725066
Wanakuambia hawauzi. Wameyapa hayo malipo majina ya kuwapumbaza watu wasiojua maandiko. Yanaitwa sadaka, sadaka maalum, sadaka ya ukombozi, maagizo maalum n.k. Ni wizi ulio dhahiri na jwa sababu wamejificha kwenye kichaka cha dini wanaona hakuna wa kuwagusa.
 
Hapa nailaumu serikali,hususani wizara ya Elimu,utamaduni na Idara za ustawi wa jamii kwa kuacha mambo maovu kama haya yaendelee,
Na ndio maana kila kukicha Kuna nabii mpya, mtume mpya au kanisa jipya. Wameshaona wakipiga utapeli kwenye kichaka cha dini hakuna wa kuwagusa
 

1 Timotheo 6:10 SRUV​

Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.
 
Back
Top Bottom