Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Pamoja na kumtaja Kibunango, huu ushauri wangu ni kwa wazalendo wote wa Tanzania wanaolipenda na kulitakia mema taifa letu.
- Fikiria baadaye baada ya miaka mingi utakapokuwa umekaa na mjukuu wako ukimsimulia historia mpya ya taifa ilivyoandikwa mwaka 2010.
- Fikiria faraja utakayokuwa nayo kumjuza ukombozi ulivyopatikana mwaka huo na kwamba wewe babu yake ulikuwa sehemu ya hayo mabadiliko muhimu.
- Fikiria heshima atakayokupa mjukuu wako akifahamu wewe ulishiriki kikamilifu katika kulikomboa taifa mikononi mwa wale waliokuwa na nia ya kuliangamiza.
- Fikiria fahari utakayoisikia ukikumbuka kwamba wewe pamoja na wazalendo wengine mliweza kuipiga mweleka chama kilichoididimiza nchi kwa miaka hamsini.
- Fikiria atakavyoweza kutamba mbele ya rafiki zake kuwa babu yake alikuwa moja wa wanaharakati waliowezesha misingi ya utawala bora na maisha bora.
- Fikiria amani utakayokuwa nayo moyoni ukiwaona wajukuu zako wanafurahia maisha bora kwa sababu tu hukukubali kuhadaiwa kwa kanga na kofia kuuza kura yako.
- Fikiria, fikiria, fikiria........
Tumuunge mkono Dr. Slaa na kwa pamoja tuiandike upya historia ya taifa letu.