Mdau Makini
Member
- Sep 18, 2012
- 70
- 10
Mwanajeshi kava raba za "coverse"!
Ikiwa hakuna yeyote katika sisi tunaolalamika atachukua hatua basi hakuna kitakachobadilika na hivyo malalamiko yetu yataishia kuwa "Ugonjwa mpya wa Watanzania wa kulalamika bila kuchukua hatua." Sisi tunaokosoa tushike camera, mouse za kompyuta, taa, microphone, stand, cranes, make ups na tufanye kitu.
Ni kweli kuwa wakosoaji wanatakiwa lakini pia watenda kazi mahiri wanatakiwa pia. Marekani kuna James Cameron, Steven Spielberg, Digital Dmain, ILM etc, hao wakilalamika basi James Cameron anafanyia kazi malalmiko yao, huku nani anafanyia kazi ukosoaji wenu (wetu). Ninyi mliosoma Kompyuta tutengenezeeni effects nzuri tutatoa pesa, ninyi mnaosifu script ya Jack Bauer ama Jason Bourne tuandikieni nzuri basi. Sisi uwezo wetu umeishia hapo.
Tanzania ni masikini..... sawa.
Waigizaji ni vilaza........ sawa.
Yanga haina chochote.. sawa.
Hemed anaringa sana.... sawa.
Titanic ni noma............ sawa.
Waafrika ni masikini....... sawa.
Weusi unatokana melanin nyingi katika ngozi..... sawa.
China ni noma hata Marekani wanawaogopa..... sawa.
Iran ni noma, Israel watakoma.... sawa.
Malawi wanatuchezea hawa..... sawa.
Yule jamaa ni gamba tu.... sawa.
KISHA NINI?
Ni kweli mkuu, nilijizuia nisichangie chochote kwenye mada hii
lakini kutokana na mchango wako ninalazimika kusema machache.
Kiukweli katika wachangiaji wengi, na asilimia kubwa ya wanaojiita
wakosoaji wa filamu wa kiTanzania ni vilaza wa kutupwa kwa
kuwa wanakosoa jambo ambalo wao wenyewe hawalijui na wanaongozwa
na chuki badala ya taaluma. Sidhani kama ni sahihi kujiita wakosoaji,
badala yake wangeitwa wapondaji kwa kuwa mkosoaji siku zote
huonesha njia (namna ya kufanya) badala ya kuishia kuponda
tu bila kuonesha solution. Kwa mtu yeyote makini na anayeijua
tasnia ya filamu hawezi kukosoa sinema ya Kanumba (kwa mfano)
kwa kuilinganisha na sinema ya Denzel Washington, kwa vyovyote
atakuwa na matatizo ya akili. Kuendelea kulalamika au kuponda
bila kuchukua hatua hakutusaidii, sana sana ninachokiona hapa ni
kujaribu kuyahamishia matatizo yetu kwenye mitandao ya jamii
tukidhani kuwa tunatafuta solution...
Mimi sikubaliani na wewe. Mimi sio kilaza na wakiitwa vilaza sitakwenda mbele. Kama wewe ni msomaji mweye kumbu kumbu nzuri, utakumbuka siku za nyumba niliwahi kuuliza Lucy Kihwele anafanya nini kuwasaidia wasanii wa Bongo, kwa nini anaeleka cinema za Bongo MTV zikiwa na poor quality. Tumeshasema sana hapa, kwa nini wasanii wa Bongo wasiwape watu cinema zao wafanye editing, kuona obvious engilish mistakes? Tunaishia kupata aibu kubwa kwenye cinema za Bongo!
Tumeshasema sana, wakina Ray, kwa nini wasiajili watu watakaokuwa wanapitia scripts zao ili kuona kama zina mantiki?
Mkuu, hii thread haijaanzia hapa, soma threads za nyuma uone tumesema nini.
Hatuna jabza wala wivu na Ray, wengine hatutegemei hata siku moja kuingia kwenye hiyo tasinia.
Ila, tunasema kwa sababu tunaona, na hata wewe mwenyewe unaona!
This is true empty (ukweli mtupu)