Utajiri wa gesi umepotelea wapi?

Utajiri wa gesi umepotelea wapi?

SONGOKA

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
1,836
Reaction score
1,845
Miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya gesi asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatuambia sasa umasikini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua uchumi wa gesi, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umasikini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof. Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka Polisi na Jeshi kudhibiti watu kule Kusini ili uchimbaji wa gesi ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na Urusi ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gesi.

Cha kushangaza, hakuna tena anayeongelea kuhusu uchumi wa gesi wala kuuaga umasikini kupitia uchumi wa gesi.

Huu utajiri wa gesi umepotelea wapi hivi?
 
miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya GAS asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatwambia sasa umaskini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua UCHUMI WA GAS, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umaskini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka POLIS na JESHI kudhibiti watu kule kusini ili uchimbaji wa GAS ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na URUSI ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gas

CHA KUSHANGAZA, hakuna tena anayeongelea kuhusu UCHUMI WA GAS wala kuuaga umaskini kupitia UCHUMI WA GAS.
HUU UTAJILI WA GAS umepotelea wapi hivi??

Kama nadharia inaitwa Resources Curse au "The Paradox of Plenty"!!! Isome inaweza kukusaidia kujibu hii hoja yako
 
miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya GAS asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatwambia sasa umaskini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua UCHUMI WA GAS, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umaskini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka POLIS na JESHI kudhibiti watu kule kusini ili uchimbaji wa GAS ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na URUSI ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gas

CHA KUSHANGAZA, hakuna tena anayeongelea kuhusu UCHUMI WA GAS wala kuuaga umaskini kupitia UCHUMI WA GAS.
HUU UTAJILI WA GAS umepotelea wapi hivi??
Nawe umeanzisha thread?????? Utajiri unataka uwe unatangazwa kwenye kipindi gani ndiyo uridhike?
 
Serikali laghai huwa hazina mipango madhubuti inayoeleweka zaidi ya blah blah zenye kulaghai wananchi wake kwenye majukwaa ya kisiasa
Mleta uzi anasahau mswaada ulipitishwa usiku wa manane, wapinzani hawahawa wakiwa wamefukuzwa ukumbini na spika. Ile ilikuwa kuiuza gas hiyo kwa mikataba sawa na ya madini mengine. WaTz hatuna wa kumlaumu tujilaumu wenyewe kwa kuendekeza uongozi huu wa CCM.
 
yawezekana hufuatilii masuala ya nchi yako, ila umeendekeza siasa. gesi haijaanza kuchimbwa, ila mchakato unaendelea na sasa mazungumzo ya kujenga NLG plant mkoani lindi kwa makampun washirika na serikali unaendelea. mchakato wa gesi is not an overnight event, it is a process, inapitia procedures mbalimbali. ges inayotumika sasa ni ya mda mrefu kutoka msimbati na songosongo, na ndio inayosafirishwa kwa bomba hadi dar es salaam. kama hujui jambo ni vema ukatafuta taarifa sahihi kuliko kubwabwaja tu mitandaoni
 
Back
Top Bottom