Utajiri uliojificha kwenye kilimo cha mbegu za mchicha

Utajiri uliojificha kwenye kilimo cha mbegu za mchicha

Jebel

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2021
Posts
376
Reaction score
2,513
Wasalaam,

Je, umeshawahijiuliza njia rahisi ya kutoka kimaisha kutokana na kilimo? Basi leo nataka nikuletee jibu la swali lako.
Kama wewe ni kijana mwenye ndoto za kutoka kimaisha basi pata mtaji mtamu sana kutoka kwenye kilimo hiki cha mbegu za mchicha. Hiki ni kilimo chenye gharama nafuu sana, kwani hakihitaji dawa ya aina yoyote, palizi moja tu na soko la mazao yake ni la uhakika sana.

Kama ilikuwa hujui mbegu za ule mchicha wa kung’oa baada ya siku 18 tu zinatoka wapi, basi leo ni siri nakuletea.

A. NAMNA YA KULIMA ZAO HILI.

-Andaa shamba lako vema, udongo wa kichanga cheusi yaani wenye rutuba au tifutifu unafaa zaidi.

-Hakikisha shamba lako lina rutuba ya kutosha kama rutuba haitoshi basi ongeza mbolea ya samadi kisha baada ya week 4 au 5 ongeza mbolea ya UREA.

-Kwa ekari moja ya 70/70 mbegu 1Kg inatosha sana. Bei ya kilo moja ya mbegu ni Tsh 6000tu.

-Jitahidi sana upande kwa wakati mwafaka kulingana na msimu wa mvua wa eneo lako mfano mkoa wa Kagera wilaya za Muleba, Bukoba mjini na vijijini, Misenyi na Karagwe yote panda kuanzia tarehe 15/8 wilaya ya Biharamlo na Ngara pande September, Kigoma wilaya zote panda katikati ya September na October mwanzoni. Kwa kifupi msimu wa kupanda mahindi katika eneo lako nawe panda kipindi hicho hicho.

-Zingatia palizi kwa mda mwafaka sana

-MUHIMU zaidi jitahidi sana spacing kati ya mche na mche iwe ya kutosha, hivyo wakati wa palizi jitahidi sana iwepo pruning ya kutosha yaani haya majamaa haitakiwi yasogeleane sana kwa matokeo mazuri zaidi.

-Zao hili ni la mda mfupi sana miezi 3 tu unavuna, hivyo andaa tundubai kwa ajili ya kuvuna. Haya majamaa ni mepesi sana kuvuna kuliko ZAO lolote yaani ni ya kukata kwa kisu unaweka kwenye tundubai, unayapiga na kupata tule tu mbegu, peleka sokoni urudi na pesa.

B. SOKO LAKE.
Kuna uhakika wa soko kwani wakulima wa mchicha ni wengi sana, na wanahitaji mbegu hii lakini pia mbegu hii ina matumizi mengine zaidi ya kupanda.

C. CHANGAMOTO ZAKE
Kilimo chochote usidanganyike kina changamoto tu lakini kwa ZAO hili ukilinganisha na mazao mengine ni chache sana
-Spacing yake, yaani haya majamaa yakibanana sana utavuna kidogo sana ili yaweke matunda mazuri ni vema iwepo nafasi ya kutosha walau 3-6cm kati ya mche na mche. Kuya prune huwa ni changamoto sana
-Kama ardhi haina rutuba utavuna kidogo sana
D. GHARAMA ZA JUMLA KWA EKARI MOJA
- Kodi kwa ekari 50,000Tsh
-Kulima ekari 50,000Tsh
-Kupanda ekari 20,000Tsh
-Palizi na pruning 50,000Tsh
-Kuvuna na kupack 50,000Tsh
-Mbegu 4,000Tsh
-Extra costs 20,000Tsh

JUMLA 250,000Tsh.

E. MAVUNO KWA EKARI MOJA

-Kama shamba lina rutuba nzuri, mvua imeenda vema, umepanda vizuri kuna uhakika wa kuvuna kuanzia 500-800Kg kwa ekari moja

F. SOKO LAKE NA BEI
Kwa maeneo mengi 1Kg utaweza kuuza kwa Tsh 3500-4000. Soko lake ni uhakika sana kwani nchi nzima mchicha unalimwa na kuliwa.

NB. Mwaka huu nimelima ekari 10 tu nimeweka zaidi 13M NMB na gharama niliyotumia ni chini ya 3M. Na hii ni ndani ya miezi 3 tu.

Mwisho achana na kilimo cha mahindi na mpunga utakufa kwa presha.
 
Wasalaam,

Je, umeshawahijiuliza njia rahisi ya kutoka kimaisha kutokana na kilimo? Basi leo nataka nikuletee jibu la swali lako.
Kama wewe ni kijana mwenye ndoto za kutoka kimaisha basi pata mtaji mtamu sana kutoka kwenye kilimo hiki cha mbegu za mchicha. Hiki ni kilimo chenye gharama nafuu sana, kwani hakihitaji dawa ya aina yoyote, palizi moja tu na soko la mazao yake ni la uhakika sana.

Kama ilikuwa hujui mbegu za ule mchicha wa kung’oa baada ya siku 18 tu zinatoka wapi, basi leo ni siri nakuletea.

A. NAMNA YA KULIMA ZAO HILI.

-Andaa shamba lako vema, udongo wa kichanga cheusi yaani wenye rutuba au tifutifu unafaa zaidi.

-Hakikisha shamba lako lina rutuba ya kutosha kama rutuba haitoshi basi ongeza mbolea ya samadi kisha baada ya week 4 au 5 ongeza mbolea ya UREA.

-Kwa ekari moja ya 70/70 mbegu 1Kg inatosha sana. Bei ya kilo moja ya mbegu ni Tsh 6000tu.

-Jitahidi sana upande kwa wakati mwafaka kulingana na msimu wa mvua wa eneo lako mfano mkoa wa Kagera wilaya za Muleba, Bukoba mjini na vijijini, Misenyi na Karagwe yote panda kuanzia tarehe 15/8 wilaya ya Biharamlo na Ngara pande September, Kigoma wilaya zote panda katikati ya September na October mwanzoni. Kwa kifupi msimu wa kupanda mahindi katika eneo lako nawe panda kipindi hicho hicho.

-Zingatia palizi kwa mda mwafaka sana

-MUHIMU zaidi jitahidi sana spacing kati ya mche na mche iwe ya kutosha, hivyo wakati wa palizi jitahidi sana iwepo pruning ya kutosha yaani haya majamaa haitakiwi yasogeleane sana kwa matokeo mazuri zaidi.

-Zao hili ni la mda mfupi sana miezi 3 tu unavuna, hivyo andaa tundubai kwa ajili ya kuvuna. Haya majamaa ni mepesi sana kuvuna kuliko ZAO lolote yaani ni ya kukata kwa kisu unaweka kwenye tundubai, unayapiga na kupata tule tu mbegu, peleka sokoni urudi na pesa.

B. SOKO LAKE.
Kuna uhakika wa soko kwani wakulima wa mchicha ni wengi sana, na wanahitaji mbegu hii lakini pia mbegu hii ina matumizi mengine zaidi ya kupanda.

C. CHANGAMOTO ZAKE
Kilimo chochote usidanganyike kina changamoto tu lakini kwa ZAO hili ukilinganisha na mazao mengine ni chache sana
-Spacing yake, yaani haya majamaa yakibanana sana utavuna kidogo sana ili yaweke matunda mazuri ni vema iwepo nafasi ya kutosha walau 3-6cm kati ya mche na mche. Kuya prune huwa ni changamoto sana
-Kama ardhi haina rutuba utavuna kidogo sana
D. GHARAMA ZA JUMLA KWA EKARI MOJA
- Kodi kwa ekari 50,000Tsh
-Kulima ekari 50,000Tsh
-Kupanda ekari 20,000Tsh
-Palizi na pruning 50,000Tsh
-Kuvuna na kupack 50,000Tsh
-Mbegu 4,000Tsh
-Extra costs 20,000Tsh

JUMLA 250,000Tsh.

E. MAVUNO KWA EKARI MOJA

-Kama shamba lina rutuba nzuri, mvua imeenda vema, umepanda vizuri kuna uhakika wa kuvuna kuanzia 500-800Kg kwa ekari moja

F. SOKO LAKE NA BEI
Kwa maeneo mengi 1Kg utaweza kuuza kwa Tsh 3500-4000. Soko lake ni uhakika sana kwani nchi nzima mchicha unalimwa na kuliwa.

NB. Mwaka huu nimelima ekari 10 tu nimeweka zaidi 13M NMB na gharama niliyotumia ni chini ya 3M. Na hii ni ndani ya miezi 3 tu.

Mwisho achana na kilimo cha mahindi na mpunga utakufa kwa presha.
Utajiri ni siri,hakuna njia ya Utajiri inayowekwa wazi.
Pia Kumiliki 10M au 20M sio Utajiri, Wala Gari.
 
Sikupingi lakini soko ni changamoto kubwa sana unaenda kwa mwenye duka anakuambia anahitaji kg2 nawe una kg100 utazimaliza lini? mwingine anakuambia hahitaji
Unajua kwanini?

Walima mchicha wanalima maeneo madogo hivyo wakitaka mbegu wanaingia mtaani kuna maeneo michicha imejiotea, sasa huko ilokojiotea ikishatoa mbegu watu hawaichumi tena sasa mkulima anapita maeneo hayo anakata vile vimbelewele vyenye mbegu anaenda kukung'utia shambani kwake.
Kama tunavyojua mchicha mmoja unaweza kubeba hata mbegu 1000 hivyo mkulima anaweza kupitia miche michache iliyokomaa huko mtaani akapanda shamba lake bila kwenda dukani...

Wanaoenda kununua dukani ni wachache sana hivyo soko la hii kitu ni ngumu
 
Hata mimi nimeshangaa,eti ekari moja utoe gunia 10 za kg 100,

Mmh!?
Mkuu hii inawezekana kuna ardhi zinarutuba najua wewe upo kanda ya ziwa ni ngumu kukuta gunia hata moja au tatu za ufuta lakini niliwahi kuulima pwani nilitoa gunia 7 japo lilikua zaidi ya heka moja na hapo kuna mahali maji yaliuharibu.

Mto ruvu pale kisarawe kuna baadhi ya maeneo ukilima ukpanda mahindi yaote kisha wiki nzima hujaenda ukifika unakataa kama siyo yenyewe yamekuwa na kurefuka kama yanavutwa na kamba! kwenye shimo moja unaweka mahindi 4 au zaidi na yote yanabeba! sijawahi kuona hii ile kule vizembe kama sijakosea jina pako hivyo!
 
Unajua kwanini?

Walima mchicha wanalima maeneo madogo hivyo wakitaka mbegu wanaingia mtaani kuna maeneo michicha imejiotea, sasa huko ilokojiotea ikishatoa mbegu watu hawaichumi tena sasa mkulima anapita maeneo hayo anakata vile vimbelewele vyenye mbegu anaenda kukung'utia shambani kwake.
Kama tunavyojua mchicha mmoja unaweza kubeba hata mbegu 1000 hivyo mkulima anaweza kupitia miche michache iliyokomaa huko mtaani akapanda shamba lake bila kwenda dukani...

Wanaoenda kununua dukani ni wachache sana hivyo soko la hii kitu ni ngumu
Ni sahihi kabisa soko gumu mno...mimi binafisi nimewahi nunua mara1 tu mbegu ya mchicha tena buku2 nyingi mno sikuimaliza.

Kuna mahali niliwahi soma kuwa ni nzuri sana kwa lishe ya watoto angeegemea huko ninge msapoti
 
Sikupingi lakini soko ni changamoto kubwa sana unaenda kwa mwenye duka anakuambia anahitaji kg2 nawe una kg100 utazimaliza lini? mwingine anakuambia hahitaji
Hujaelewa tu hapa wanatafutwa wateja wa mbegu?
Ukinunua ukafanikwa kuvuna mbegu nyingi shughuli ipo kwenye soko.
Utamuuzia nani labda nawe uanze mbinu za jamaa mitandaoni na kwa ndugu na jamaa zako wa karibu.
 
Sitafuti soko wakuu, sehemu nilipo hutu tudude tunatafutwa sana. Lakini mnaruhusiwa kuwaza vyovyote vile, hii ndiyo typical Tanzanian mentality. Posts za ujinga hakuna anayebeza ila za kusaidia watu kuinuka mnatoa response za ovyo. Ain’t surprised though.
 
Wasalaam,

Je, umeshawahijiuliza njia rahisi ya kutoka kimaisha kutokana na kilimo? Basi leo nataka nikuletee jibu la swali lako.
Kama wewe ni kijana mwenye ndoto za kutoka kimaisha basi pata mtaji mtamu sana kutoka kwenye kilimo hiki cha mbegu za mchicha. Hiki ni kilimo chenye gharama nafuu sana, kwani hakihitaji dawa ya aina yoyote, palizi moja tu na soko la mazao yake ni la uhakika sana.

Kama ilikuwa hujui mbegu za ule mchicha wa kung’oa baada ya siku 18 tu zinatoka wapi, basi leo ni siri nakuletea.

A. NAMNA YA KULIMA ZAO HILI.

-Andaa shamba lako vema, udongo wa kichanga cheusi yaani wenye rutuba au tifutifu unafaa zaidi.

-Hakikisha shamba lako lina rutuba ya kutosha kama rutuba haitoshi basi ongeza mbolea ya samadi kisha baada ya week 4 au 5 ongeza mbolea ya UREA.

-Kwa ekari moja ya 70/70 mbegu 1Kg inatosha sana. Bei ya kilo moja ya mbegu ni Tsh 6000tu.

-Jitahidi sana upande kwa wakati mwafaka kulingana na msimu wa mvua wa eneo lako mfano mkoa wa Kagera wilaya za Muleba, Bukoba mjini na vijijini, Misenyi na Karagwe yote panda kuanzia tarehe 15/8 wilaya ya Biharamlo na Ngara pande September, Kigoma wilaya zote panda katikati ya September na October mwanzoni. Kwa kifupi msimu wa kupanda mahindi katika eneo lako nawe panda kipindi hicho hicho.

-Zingatia palizi kwa mda mwafaka sana

-MUHIMU zaidi jitahidi sana spacing kati ya mche na mche iwe ya kutosha, hivyo wakati wa palizi jitahidi sana iwepo pruning ya kutosha yaani haya majamaa haitakiwi yasogeleane sana kwa matokeo mazuri zaidi.

-Zao hili ni la mda mfupi sana miezi 3 tu unavuna, hivyo andaa tundubai kwa ajili ya kuvuna. Haya majamaa ni mepesi sana kuvuna kuliko ZAO lolote yaani ni ya kukata kwa kisu unaweka kwenye tundubai, unayapiga na kupata tule tu mbegu, peleka sokoni urudi na pesa.

B. SOKO LAKE.
Kuna uhakika wa soko kwani wakulima wa mchicha ni wengi sana, na wanahitaji mbegu hii lakini pia mbegu hii ina matumizi mengine zaidi ya kupanda.

C. CHANGAMOTO ZAKE
Kilimo chochote usidanganyike kina changamoto tu lakini kwa ZAO hili ukilinganisha na mazao mengine ni chache sana
-Spacing yake, yaani haya majamaa yakibanana sana utavuna kidogo sana ili yaweke matunda mazuri ni vema iwepo nafasi ya kutosha walau 3-6cm kati ya mche na mche. Kuya prune huwa ni changamoto sana
-Kama ardhi haina rutuba utavuna kidogo sana
D. GHARAMA ZA JUMLA KWA EKARI MOJA
- Kodi kwa ekari 50,000Tsh
-Kulima ekari 50,000Tsh
-Kupanda ekari 20,000Tsh
-Palizi na pruning 50,000Tsh
-Kuvuna na kupack 50,000Tsh
-Mbegu 4,000Tsh
-Extra costs 20,000Tsh

JUMLA 250,000Tsh.

E. MAVUNO KWA EKARI MOJA

-Kama shamba lina rutuba nzuri, mvua imeenda vema, umepanda vizuri kuna uhakika wa kuvuna kuanzia 500-800Kg kwa ekari moja

F. SOKO LAKE NA BEI
Kwa maeneo mengi 1Kg utaweza kuuza kwa Tsh 3500-4000. Soko lake ni uhakika sana kwani nchi nzima mchicha unalimwa na kuliwa.

NB. Mwaka huu nimelima ekari 10 tu nimeweka zaidi 13M NMB na gharama niliyotumia ni chini ya 3M. Na hii ni ndani ya miezi 3 tu.

Mwisho achana na kilimo cha mahindi na mpunga utakufa kwa presha.
Asante mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom