Yabesi Consult Co Ltd
Member
- Jan 13, 2018
- 38
- 60
Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo, Kmb 8:18
Watu wengi wanasema Mungu hatoi utajiri, huo ni Uongo. Mungu anatoa utajiri, tena watumishi wengi wa Mungu walikuwa ni matajiri.
Umesoma habari za Ibrahim jinsi alivyokuwa Tajiri wa Mali, Mwz 22:18.
Je, umasoma habari za Isaka na Yakobo jinsi walivyokuwa matajiri? Haukusoma habari ya Ayubu jinsi Mungu alivyomtajirisha?
Utajiri na heshima ziko kwangu, naam, utajiri udumuo, na haki pia,
Mithali 8:18.
Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake, 2Kor 8:9.
Kwanini watu wengi wa Mungu hawana utajiri;
Mosi, wengi wanadhani kuwa utajiri ni dhambi au mtu tajiri hana Imani, hayo ndio mafundisho potofu.
Pili, watu wengi wanaomba kupewa utajiri kwa ajili ya manufaa binafsi na sio Mungu kutukuzwa katika huo utajiri, Mungu anataka ukiwa Tajiri ushiriki katika kusaidia kusukuma mbele injili, kutunza watumishi wake na kuimarisha angano lake kwa sadaka.
Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu, Yk 4:3.
Mungu atusaidie tunapopewa utajiri tuweze kuutumia kwa mapenzi yake. Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha.
Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo, 1 Timotheo 6:17-18.
Watu wengi wanasema Mungu hatoi utajiri, huo ni Uongo. Mungu anatoa utajiri, tena watumishi wengi wa Mungu walikuwa ni matajiri.
Umesoma habari za Ibrahim jinsi alivyokuwa Tajiri wa Mali, Mwz 22:18.
Je, umasoma habari za Isaka na Yakobo jinsi walivyokuwa matajiri? Haukusoma habari ya Ayubu jinsi Mungu alivyomtajirisha?
Utajiri na heshima ziko kwangu, naam, utajiri udumuo, na haki pia,
Mithali 8:18.
Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake, 2Kor 8:9.
Kwanini watu wengi wa Mungu hawana utajiri;
Mosi, wengi wanadhani kuwa utajiri ni dhambi au mtu tajiri hana Imani, hayo ndio mafundisho potofu.
Pili, watu wengi wanaomba kupewa utajiri kwa ajili ya manufaa binafsi na sio Mungu kutukuzwa katika huo utajiri, Mungu anataka ukiwa Tajiri ushiriki katika kusaidia kusukuma mbele injili, kutunza watumishi wake na kuimarisha angano lake kwa sadaka.
Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu, Yk 4:3.
Mungu atusaidie tunapopewa utajiri tuweze kuutumia kwa mapenzi yake. Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha.
Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo, 1 Timotheo 6:17-18.