Eli Cohen
JF-Expert Member
- Jun 19, 2023
- 1,311
- 4,019
Pesa, Ardhi na Mapenzi.
Hivi ni vitu vilivyo mwaga damu sana, vilivyo karibisha ushetani, vilvyo vunja utu na vilivyo tengeneza uhasama mkubwa sana.
Lakini bado ni vitu vyenye thamani kuliko vitu vyote.
Unapotafuta kiwanja, inabidi uwekeze zaidi katika umakini na upelelezi.
Kuna sehemu nilipata kiwanja, jamaa akawa tayari kuniuzia, lakini kumbe nyuma ya pazia kile kiwanja ni urithi wa watoto wa kaka yake yani baada ya kaka yao kufariki na barua zipo. Yeye akawa amepewa cha nyuma yake ila yeye anang'ang'ania pote.
Kuna sehemu nilipata kiwanja, jamaa akawa ananihakikishia kabisa kuwa hakuna tabu na hadi majirani zake (kabila moja) pale wakawa wanachochea. Lakini kwa bahati nzuri kuna afisa ardhi anaishi pembeni na anamjua mshikaji wangu niliekuwa nae, akatuita pembeni na kuniambia kuwa hapo pana mgogoro jamaa anaekuuzia alinunua kiwanja cha mtu mwingine kwa hio ni kama anataka arushie mtu janga asepe.
Kuna sehemu tena, jamaa ana burgain bei na mimi bei kumbe kiwanja sio chake, ni cha mdogo wake, baadae baada ya kumchimba eti ndio ananiambia sio chake. Kwa hio ina maana bei aliotaka kupatana na mimi ilikuwa kaeka commission yake juu.
KUWENI MAKINI.
Hivi ni vitu vilivyo mwaga damu sana, vilivyo karibisha ushetani, vilvyo vunja utu na vilivyo tengeneza uhasama mkubwa sana.
Lakini bado ni vitu vyenye thamani kuliko vitu vyote.
Unapotafuta kiwanja, inabidi uwekeze zaidi katika umakini na upelelezi.
Kuna sehemu nilipata kiwanja, jamaa akawa tayari kuniuzia, lakini kumbe nyuma ya pazia kile kiwanja ni urithi wa watoto wa kaka yake yani baada ya kaka yao kufariki na barua zipo. Yeye akawa amepewa cha nyuma yake ila yeye anang'ang'ania pote.
Kuna sehemu nilipata kiwanja, jamaa akawa ananihakikishia kabisa kuwa hakuna tabu na hadi majirani zake (kabila moja) pale wakawa wanachochea. Lakini kwa bahati nzuri kuna afisa ardhi anaishi pembeni na anamjua mshikaji wangu niliekuwa nae, akatuita pembeni na kuniambia kuwa hapo pana mgogoro jamaa anaekuuzia alinunua kiwanja cha mtu mwingine kwa hio ni kama anataka arushie mtu janga asepe.
Kuna sehemu tena, jamaa ana burgain bei na mimi bei kumbe kiwanja sio chake, ni cha mdogo wake, baadae baada ya kumchimba eti ndio ananiambia sio chake. Kwa hio ina maana bei aliotaka kupatana na mimi ilikuwa kaeka commission yake juu.
KUWENI MAKINI.