cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Juzi nilifika Mkoani Mara hasa wilaya ya Tarime maeneo ya vijijini karibu na mpakani mwa Tanzania na Kenya
Nilifika vijiji vya Gwitiryo,Pemba,Borega na kwingineko na nilicho baini katika vijiji hivi,mambo yanayofanyika hapa ni hatari kwa usalama wa Taifa kwa sasa na baadae
Jamii ya wakurya wanaokaa hapa wameanzisha utamaduni wa kuoa wanawake kutoka nchini Kenya ambao tayari wana watoto zaidi ya watatu na kuendelea
Yaani wanaume wa vijiji vya mpakani wanaenda Kenya wanachukua wanawake waliokwisha zaa huko Kenya na watoto wao na kuwahamishia upande wa Tanzania na hao watoto huhesabiwa kama watoto wa Mwita Chacha wa Tanzania na hupewa majina ya ukoo kwa upande wa Tanzania, watoto hawa wengine huwa wana umri mkubwa
Mmoja wa mwanakijiji niliyekutana katika kijiji cha Nyabitocho alinisimulia kuwa watoto walio olewa pamoja na mama zao ni wengi tu,na isitoshe tunawafahamu na wengine ni wajumbe wa serikali ya kijiji na wengine ni viongozi kwenye vyama vya siasa wanawafahamu lakini wananyamaza tu na ukifuatilia hawana vibali vya kuishi Tanzania
Mwingine aliniambia kipindi anasoma chuo kikuu Dodoma wamesoma na kijana ambaye waliolewa na mama yake huku Tanzania lakini baadae akili ilipo pevuka akarudi Kisii Kenya kwa ndugu zake hata hivyo kupitia elimu ya Tanzania alisoma hadi chuo kikuu na mkopo akapata ila cha ajabu likizo alikuwa anaenda kisii Kenya na alipinga yeye kuolewa na mama yake ila anashukuru kupata mwanya wa kusoma Tanzania hadi chuo kikuu kupitia mama yake
Nikataka kujua kama kuna watanzania wanaolewa Kenya na watoto wao,walisema upande wa Kenya hakuna kitu kama hicho,Kenya wanasheria kali kuhusu wahamiaji ,hakuna mtanzania anaweza kujiita mkenya ila wakenya wengi wanajiita Watanzania
Nimebaini kuwa kwa miaka kadhaa ijayo usalama wa Taifa la Tanzania utakuwa hatarini,je hao wanawake wanao olewa kutoka Kenya na watoto wao wakija Tanzania wanasoma na kuanza kutambulika kama Watanzania Idara ya uhamiaji inalijua hilo? Na wamechukua hatua gani? Viongozi wa vijiji wapo tu hawachukui hatua
Hizi familia zinazo olewa kutoka Kenya ni hatari kwa usalama wa Taifa ,kuna siku usalama wa Taifa tutawakabidhi wakenya nionavyo miaka ijayo
Wakurya acheni kuoa wanawake wa Kenya na familia zao,mnahatarisha usalama wa Taifa
Nilifika vijiji vya Gwitiryo,Pemba,Borega na kwingineko na nilicho baini katika vijiji hivi,mambo yanayofanyika hapa ni hatari kwa usalama wa Taifa kwa sasa na baadae
Jamii ya wakurya wanaokaa hapa wameanzisha utamaduni wa kuoa wanawake kutoka nchini Kenya ambao tayari wana watoto zaidi ya watatu na kuendelea
Yaani wanaume wa vijiji vya mpakani wanaenda Kenya wanachukua wanawake waliokwisha zaa huko Kenya na watoto wao na kuwahamishia upande wa Tanzania na hao watoto huhesabiwa kama watoto wa Mwita Chacha wa Tanzania na hupewa majina ya ukoo kwa upande wa Tanzania, watoto hawa wengine huwa wana umri mkubwa
Mmoja wa mwanakijiji niliyekutana katika kijiji cha Nyabitocho alinisimulia kuwa watoto walio olewa pamoja na mama zao ni wengi tu,na isitoshe tunawafahamu na wengine ni wajumbe wa serikali ya kijiji na wengine ni viongozi kwenye vyama vya siasa wanawafahamu lakini wananyamaza tu na ukifuatilia hawana vibali vya kuishi Tanzania
Mwingine aliniambia kipindi anasoma chuo kikuu Dodoma wamesoma na kijana ambaye waliolewa na mama yake huku Tanzania lakini baadae akili ilipo pevuka akarudi Kisii Kenya kwa ndugu zake hata hivyo kupitia elimu ya Tanzania alisoma hadi chuo kikuu na mkopo akapata ila cha ajabu likizo alikuwa anaenda kisii Kenya na alipinga yeye kuolewa na mama yake ila anashukuru kupata mwanya wa kusoma Tanzania hadi chuo kikuu kupitia mama yake
Nikataka kujua kama kuna watanzania wanaolewa Kenya na watoto wao,walisema upande wa Kenya hakuna kitu kama hicho,Kenya wanasheria kali kuhusu wahamiaji ,hakuna mtanzania anaweza kujiita mkenya ila wakenya wengi wanajiita Watanzania
Nimebaini kuwa kwa miaka kadhaa ijayo usalama wa Taifa la Tanzania utakuwa hatarini,je hao wanawake wanao olewa kutoka Kenya na watoto wao wakija Tanzania wanasoma na kuanza kutambulika kama Watanzania Idara ya uhamiaji inalijua hilo? Na wamechukua hatua gani? Viongozi wa vijiji wapo tu hawachukui hatua
Hizi familia zinazo olewa kutoka Kenya ni hatari kwa usalama wa Taifa ,kuna siku usalama wa Taifa tutawakabidhi wakenya nionavyo miaka ijayo
Wakurya acheni kuoa wanawake wa Kenya na familia zao,mnahatarisha usalama wa Taifa