Wanabodi nimefanya kautafiti kadogo cha kuwahoji baadhi ya watu toka Arumeru, Moshi, Baadhi ya waandishi wa habari, Arusha, Dar es salaam kwenye mtandao na face book na kufuatilia mtandao wa JF wameonaje ufunguzi wa Mkapa kampeni ccm je ameweza kuijenga ccm au amezidi kuiporomosha.
Utakumbuka utafiti wangu huu unategemea makala iliyoandikwa na Mwandishi Karugendo kwenye gazeti la Tanzania Daima la wiki iliyopita ambayo niliipost hapa ambayo ilihoji umakini wa ccm kumpa Mkapa mikoba ya ufunguzi wa kampeni ikisema kufanya hivyo itaicha uchi ccm zaidi kuliko kukisaidia.
Hiki ndicho kimetokea zaidi asilimia 87% ya niliongea nao na kunitumia ujumbe wa simu facebook, na wandishi wameonyesha wasiwasi wa umakini wa ccm kuendelea mkuumtumia Mzee mkapa kwani amekibomoa ccm zaidi hasa ukizingatia kejeli na maneno aliyasema kuelekea CDM hayakuwa na tija na si hadhi yake.
Wengine wamesema mkapa anatakiwa kupumzika kadri anavyojitokeza mbele ya watu anawatia hasira kwani kipindi cha utawala wake ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi za uma , ukiukwaji wa haki za binadamu ulishamiri.
Ahadi aliyoitoa ya kupeleka matatizo ya ardhi kwa jk alihali anajua wakati wa utawala wake ndiyo kipindi ubinafshaji na uuzaji wa ardhi ulifanyika Arumeru, hii inaonekana ni kejeli na dharau kwa wameru.
Kuhusu kauli yake ya kutomtambua Vicent Nyerere kama ni mmoja wa wanafamilia wa Nyerere kwa Josephat Nyerere wengine wamesema hawakutegemea mzee kama mkapa anaweza akatoa kauli kama hii haliakijua itawakwaza si Vicent tu bali Familia yote Nyere achilia mbali wananchi wanaoiheshimu familia hii.
"Ikiwa anambeza dogo kama yule ambaye hamkumkashifu mkapa ni sawa na kuidharahu familia ya Nyerere na wananchi wanaiheshimu sana familia hii , ikiwa hamtambui mbunge wa msoma mjini kuwa ni miongoni mwa familia ya nyerere atamfahamu vipi Sioyi ambaye ni mtoto tu wa Marehemu Sumari".
Utakumbuka utafiti wangu huu unategemea makala iliyoandikwa na Mwandishi Karugendo kwenye gazeti la Tanzania Daima la wiki iliyopita ambayo niliipost hapa ambayo ilihoji umakini wa ccm kumpa Mkapa mikoba ya ufunguzi wa kampeni ikisema kufanya hivyo itaicha uchi ccm zaidi kuliko kukisaidia.
Hiki ndicho kimetokea zaidi asilimia 87% ya niliongea nao na kunitumia ujumbe wa simu facebook, na wandishi wameonyesha wasiwasi wa umakini wa ccm kuendelea mkuumtumia Mzee mkapa kwani amekibomoa ccm zaidi hasa ukizingatia kejeli na maneno aliyasema kuelekea CDM hayakuwa na tija na si hadhi yake.
Wengine wamesema mkapa anatakiwa kupumzika kadri anavyojitokeza mbele ya watu anawatia hasira kwani kipindi cha utawala wake ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi za uma , ukiukwaji wa haki za binadamu ulishamiri.
Ahadi aliyoitoa ya kupeleka matatizo ya ardhi kwa jk alihali anajua wakati wa utawala wake ndiyo kipindi ubinafshaji na uuzaji wa ardhi ulifanyika Arumeru, hii inaonekana ni kejeli na dharau kwa wameru.
Kuhusu kauli yake ya kutomtambua Vicent Nyerere kama ni mmoja wa wanafamilia wa Nyerere kwa Josephat Nyerere wengine wamesema hawakutegemea mzee kama mkapa anaweza akatoa kauli kama hii haliakijua itawakwaza si Vicent tu bali Familia yote Nyere achilia mbali wananchi wanaoiheshimu familia hii.
"Ikiwa anambeza dogo kama yule ambaye hamkumkashifu mkapa ni sawa na kuidharahu familia ya Nyerere na wananchi wanaiheshimu sana familia hii , ikiwa hamtambui mbunge wa msoma mjini kuwa ni miongoni mwa familia ya nyerere atamfahamu vipi Sioyi ambaye ni mtoto tu wa Marehemu Sumari".