CCM Itaendelea Kuiba na Kutapanya Pesa ya Wananchi Mpaka Lini?

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,553
41,061
Ni ukweli usiopingika, tangu ofisi ya CAG ianzishwe, hakuna wakati ulipokosekana wizi ndanibya Serikali na taasisi zake. Kinachobadilika ni wizi kuwa mkubwa, mkubwa sana au mkubwa kupindukia.

Awamu pekee ambayo ama hakukuwa na wizi au kulikuwa na wizi mdogo sana, ni awamu ya Mwalimu Nyerere, awamu ya kwanza. Na hilo lilidhihirishwa hata na maisha yake mwalimu Nyerere na familia yake. Wakati wa Mwalimu Nyerere, Urais ulikuwa wa kwake binafsi, lakini siku hizi, Urais unakuwa wa familia nzima, hata marafiki wa familia ya Rais. Ndiyo maana tunashuhudia wanafamilia kuwa sehemu ya misafara ya Rais nje ya nchi.

Awamu ya Mwinyi iligubikwa na wizi wa ajabu kupindukia, ambapo inasemwa kuwa zaidi 60% ya pesa zote za misaada, hazikuwahi hata kufika nchini, watu waliziweka kwenye akaunti zao binafsi huko mataifa ya nje. Wakati wa awamu ya Mkapa, kulikuwa na unafuu, lakini haukukoma. Baada ya hapo, wizi ndani ya Serikali umekuwa kwenye mwendo wa kupaa.

Kwa kuwa wizi unaanzia juu kabisa mpaka chini, hakuna wa kumwajibisha mwingine. Kwa sasa, wizi mpaka umehalaljshwa, ndiyo maana hata wanafamilia wa viongozi wakuu wanakuu matajiri wakubwa hata bila ya kuwa na vyanzo vilivyo wazi vya mapato ya kuwawezesha kuwa matajiri. Wameona hiyo haitoshi, sasa wamefikia mpaka hatua ya kuidhinisha malipo kwa wake wa marais. Na tunavyoenda, siku moja itawekwa rasmi kuwa kuwepo kwa malipo kwa wanafamilia wote wa marais na viongozi wengine wakuu, japo hata sasa wakati sheria hiyo haipo, wanafamilia wamekuwa wakifaidi pesa za wananchi maskini, ni kama vile kuolewa na Rais au kuwa mtoto wa Rais, tayari amefanya kazi kubwa sana kwa Taifa, kiasi cha kustahili kulipwa.

Mjadala wa wizi wa pesa za umma uliofanywa na viongozi na watendaji wakuu wa Serikali na taasisi zake, kupitia report ya CAG, kama ilivyotarajiwa, umeisha na hakuna chochote cha maana kilichoamliwa na bunge bandia (ni bunge bandia kwa sababu ndani humo kuna wabunge wengi bandia kwa kadiri ya hukumu ya mahakama kuu, na kuna wabunge wengune bandia 19 waliomo humo ndani kinyume cha katiba).

Huu wizi wote umeasisiwa, unaendelezwa, na kulindwa na CCM. Hao wevi ni viongozi wakuu kupitia CCM, na wengine ni watendaji wakuu kwenye Serikali na taasisi za serikali, ambao kiuhalisia, kama wewe siyo kada wa CCM huwezi kuteuliwa kuziongoza. Kwa hiyo wizi huu wote wa kila mwaka, kila wizara, kila halmashauri na kila taasisi unafanywa na makada wa CCM, unaendelezwa na CCM, na unalindwa na utawala wa CCM.

Maadam CCM ipo madarakani, wananchi inabidi waukubali na kuuzoeazoea, maana hakuna tegemeo wala mwanga kuwa kuna siku utakoma, au kuna siku wevi watachukuliwa hatua makini, zaidi ya hizi za kiinimacho, kama kupiga kelele sana bungeni, na mishowe kupongezana na kufunga mjadala.
 
Simply mpaka wenye nchi tutakapoamua enough is enough, lakini kinyume na hapo ni kujidanganya tu.

Kila mwaka wanasoma hizo ripoti za CAG, wanachambua, wanatoa mapemdekezo, lakini mwisho wa siku ndio tunazidi kuibiwa, huwezi kumwambia mwizi amkamate mwizi mwenzie, kuamini hivyo ni ujinga.
 
Simply mpaka wenye nchi tutakapoamua enough is enough, lakini kinyume na hapo ni kujidanganya tu.

Kila mwaka wanasoma hizo ripoti za CAG, wanachambua, wanatoa mapemdekezo, lakini mwisho wa siku ndio tunazidi kuibiwa, huwezi kumwambia mwizi amkamate mwizi mwenzie, kuamini hivyo ni ujinga.
Ni kweli. Maana hata huko kwenye mataifa ambayo huwezi kushuhudia huu upuuzi wa hapa kwetu, siyo kwamba viongozi ni malaika, bali wananchi ni wakali hasa, hawawezi kuruhusu pesa ya umma kuchezewa.

Umma ndiyo hutengeneza uongozi inaoutaka, ni kwa kutokubali upuuzi wa aina yoyote.
 
018100094042.JPG
 
Hata miaka ya nyuma ilikuwa ni nidhama aliyoweka mzungu na sio nyerere
Wafanyakazi na wananchi kwa ujumla walikuwa na nidhamu ya hali ya juu
Ukitaka kitu wizarani unaingia unajieleza na unahudumiwa bila ujinga wa kuombwa rushwa
Rushwa ilikuwa haijulikani kabisa miaka hiyo

Tatizo limekuja tulipokabidhiwa nchi na kupeperusha bendera
Baada ya miaka zikaanza bakhshishi ikapelekea rushwa

Leo kila sehemu wizi hupati tenda bila kuhonga
Hela zinapelekwa mahali zinapigwa zote bila huruma

Ajabu sana halafu tunajiita nchi
 
Simply mpaka wenye nchi tutakapoamua enough is enough, lakini kinyume na hapo ni kujidanganya tu.

Kila mwaka wanasoma hizo ripoti za CAG, wanachambua, wanatoa mapemdekezo, lakini mwisho wa siku ndio tunazidi kuibiwa, huwezi kumwambia mwizi amkamate mwizi mwenzie, kuamini hivyo ni ujinga.
Mimi ningetamani maisha yawe magumu mara mia ya yalivyo sasa maana kuna watu bado ni wapumbavu sana. Pamoja na kuwa CCM ni majizi ya kura yaliyokubuhu lakini bado kuna watu wanawaunga mkono. Ripoti za CAG miaka yote ziko hivi hivi chini wa utawala wa CCM lakini wahusika hawachukuliwi hatua na serikali inazidi kuongeza matumizi yake yasiyokuwa ya lazima. Kila mwaka tunaona serikali ikiongeza ukubwa wake kwa kuongeza idadi ya wizara, mikoa na wilaya na majimbo ya uchaguzi na ununuzi wa magari ya kifahari kwa watendaji wake. Ifike wakati hata mataahira wajue kuwa CCM ni janga kwa taifa hili.
 
Hata miaka ya nyuma ilikuwa ni nidhama aliyoweka mzungu na sio nyerere
Wafanyakazi na wananchi kwa ujumla walikuwa na nidhamu ya hali ya juu
Ukitaka kitu wizarani unaingia unajieleza na unahudumiwa bila ujinga wa kuombwa rushwa
Rushwa ilikuwa haijulikani kabisa miaka hiyo

Tatizo limekuja tulipokabidhiwa nchi na kupeperusha bendera
Baada ya miaka zikaanza bakhshishi ikapelekea rushwa

Leo kila sehemu wizi hupati tenda bila kuhonga
Hela zinapelekwa mahali zinapigwa zote bila huruma

Ajabu sana halafu tunajiita nchi

Hakika kwa nchi nyingi za Afrika, uhuru haujawa na msaada wowote. Huenda tulihitaji kupewa tu haki za msingi lakini tukaendelea kuwa chini ya utawala wa wakoloni.

Nakumbuka kuna wakati Serikali ilikuwa na kampuni ya ujenzi iliitwa MECCO. Kampuni hiyo ilikuwa hovyo kabisa, haikuweza kujenga hata barabara moja yenye ubora. Ilipokuja kampuni ya Kajima, ya Japan, baadhi ya wahandisi waliokuwa waajiriwa wa MECCO, na wahandisi wengine Watanzania, ndiyo wakawa sehemu kubwa ya wahandisi wa Kajima. Kajima ilijenga barabara nzuri kabisa tena zenye ubora wa hali ya juu. Shida kubwa ya Tanzania, siyo utaalam bali kuukosa uongozi thabiti.

Naamini, Watanzania wangeweza kufanya mambo makubwa mazuri ya ajabu, chini ya utawala wa mzungu kuliko ilivyo sasa.
 
Mimi ningetamani maisha yawe magumu mara mia ya yalivyo sasa maana kuna watu bado ni wapumbavu sana. Pamoja na kuwa CCM ni majizi ya kura yaliyokubuhu lakini bado kuna watu wanawaunga mkono. Ripoti za CAG miaka yote ziko hivi hivi chini wa utawala wa CCM lakini wahusika hawachukuliwi hatua na serikali inazidi kuongeza matumizi yake yasiyokuwa ya lazima. Kila mwaka tunaona serikali ikiongeza ukubwa wake kwa kuongeza idadi ya wizara, mikoa na wilaya na majimbo ya uchaguzi na ununuzi wa magari ya kifahari kwa watendaji wake. Ifike wakati hata mataahira wajue kuwa CCM ni janga kwa taifa hili.
Hakika umaskini wa Tanzania ni wa kutengenezwa. Na wanaoutengeneza ni CCM.

Kama ulivyonena, rasilimali nyingi zinapelekwa kwenye mambo ya hovyo kabisa. Uwingi wa mikoa na majimbo una msaada gani kwa maendeleo ya nchi zaidi ya kuongeza mikono ya kuiba?
 
Hakika kwa nchi nyingi za Afrika, uhuru haujawa na msaada wowote. Huenda tulihitaji kupewa tu haki za msingi lakini tukaendelea kuwa chini ya utawala wa wakoloni.

Nakumbuka kuna wakati Serikali ilikuwa na kampuni ya ujenzi iliitwa MECCO. Kampuni hiyo ilikuwa hovyo kabisa, haikuweza kujenga hata barabara moja yenye ubora. Ilipokuja kampuni ya Kajima, ya Japan, baadhi ya wahandisi waliokuwa waajiriwa wa MECCO, na wahandisi wengine Watanzania, ndiyo wakawa sehemu kubwa ya wahandisi wa Kajima. Kajima ilijenga barabara nzuri kabisa tena zenye ubora wa hali ya juu. Shida kubwa ya Tanzania, siyo utaalam bali kuukosa uongozi thabiti.

Naamini, Watanzania wangeweza kufanya mambo makubwa mazuri ya ajabu, chini ya utawala wa mzungu kuliko ilivyo sasa.
Nakubaliana na wewe mkuu
Tatizo letu ni kutokufuata sheria na nidhamu kazini
Watanzania sio wajinga kama unavyosema ila tuna tatizo la kutokujikubali
Kila kitu wanaogoapa kufanya

Ukisema fanyeni hivi wanashangaa
Wenzetu wanaendelea kwa uthubutu na uzalendo wanajiamini na kufanya mambo kwa kupenda wasonge mbele

Sisi unaiba hela zinazoenda kufanya maendeleo

Mashirika yalikuwa mashirika kweli
Miaka ya 60 nakumbuka father alinichukua safari akakata ticket ya first class nakumbuka mpaka chakula tulicholetewa chumbani huku waiter akiwa na gloves nyeupe
Supu ilikuwa tamu sana
Nilikuwa mdogo but I still remember, wazungu walikuwepo pia
Train Safi, maji na kioo cha kujitazama yaani nidhamu ya hali ya juu
Nakumbuka waswahili wakulima walikuwa na magari yao kama Peugeot
Leo hii mkulima ana njaa kavaa yebo
 
Simply mpaka wenye nchi tutakapoamua enough is enough, lakini kinyume na hapo ni kujidanganya tu.

Kila mwaka wanasoma hizo ripoti za CAG, wanachambua, wanatoa mapemdekezo, lakini mwisho wa siku ndio tunazidi kuibiwa, huwezi kumwambia mwizi amkamate mwizi mwenzie, kuamini hivyo ni ujinga.
Wizi ulioko ndani ni mkubwa kuliko hata hiyo report ya CAG
 
Simply mpaka wenye nchi tutakapoamua enough is enough, lakini kinyume na hapo ni kujidanganya tu.

Kila mwaka wanasoma hizo ripoti za CAG, wanachambua, wanatoa mapemdekezo, lakini mwisho wa siku ndio tunazidi kuibiwa, huwezi kumwambia mwizi amkamate mwizi mwenzie, kuamini hivyo ni ujinga.
Mwenyekiti Wa Ccm Taifa Atasema Nini Kwenye Hili Jambo Zaidi Kawa Mtazamaji
Baadaye Mtawaulaumu CAG,PCCB, COURT Huku Akijua Mkwamishaji Ni Mmoja Tu
 
Mimi ningetamani maisha yawe magumu mara mia ya yalivyo sasa maana kuna watu bado ni wapumbavu sana. Pamoja na kuwa CCM ni majizi ya kura yaliyokubuhu lakini bado kuna watu wanawaunga mkono. Ripoti za CAG miaka yote ziko hivi hivi chini wa utawala wa CCM lakini wahusika hawachukuliwi hatua na serikali inazidi kuongeza matumizi yake yasiyokuwa ya lazima. Kila mwaka tunaona serikali ikiongeza ukubwa wake kwa kuongeza idadi ya wizara, mikoa na wilaya na majimbo ya uchaguzi na ununuzi wa magari ya kifahari kwa watendaji wake. Ifike wakati hata mataahira wajue kuwa CCM ni janga kwa taifa hili.
Ni kama umeisemea nafsi yangu, shida nchi hii naamini wajinga ni zaidi 80% ndio maana hao jamaa wanaendelea kuwepo maana kwa watu wenye akili timam ata tunayojadili sasa nchi ingeshasimama
 
Ni kama umeisemea nafsi yangu, shida nchi hii naamini wajinga ni zaidi 80% ndio maana hao jamaa wanaendelea kuwepo maana kwa watu wenye akili timam ata tunayojadili sasa nchi ingeshasimama
Kwenye mataifa yaliyoendelea, watawala wanafanya yale ambayo umma unataka. Nchi za hovyo kama hizi zetu, umma unafanya yale ambayo watawala wanataka. Ndiyo maana mnakuwa na viongozi ambao ni mafisadi na wevi, lakini wanasifiwa kila siku. Ni kama wanaambiwa waibe zaidi.
 
Back
Top Bottom