Utafiti: Uhusiano unaoanzia mtandaoni huenda ukawa ndio bora zaidi kulinganisha na ule wa kawaida!!!

myplusbee

JF-Expert Member
Jul 8, 2016
3,612
6,153
Hapa nitangulie kusema kwamba, binafsi nimeuelewa sana utafiti uliofanywa na Maprofesa wa Idara ya Sosholojia ya Chuo Kikuu cha Chicago!

Kwa ufupi utafiti huo unasema kwamba uhusiano unaoanzia mtandaoni huenda ukawa ndio bora zaidi kulinganisha na ule wa kawaida!!! Hoja yao ni kwamba, Online Dating inatoa uwanda mpana zaidi wa kuchagua mwenza sahihi kuliko uhusiano unaotokana na njia za asili!

Wanachojaribu kutuambia hapa ni kwamba, ingekuwa mtu anatafuta gari apendalo basi online dating ni sawa na kuingia kwenye mtandao wa nyumbani (local website) unaouza magari huku mtandao huo ukiwa ume-upload magari ya aina na sifa mbalimbali. Hapo mteja anapata fursa ya kuchagua gari apendalo kwa umakini zaidi kutoka kwenye maelefu ya magari yaliyokuwa uploaded kabla hajatembelea yard iliyohifadhi magari hayo na kuchunguza kwa ukaribu zaidi gari alilolipenda mtandaoni hapo kabla!

Kinyume chake, uhusiano kwa njia za asili ni sawa na mtu anayesimama barabarani au kituo cha magari kama vile Ubungo Terminal huku akijaribu kuchagua gari apendalo kutoka kwenye magari kadhaa yaliyo kwenye mwendo au yaliyoegeshwa kabla hajaenda yard kuchunguza gari husika kwa umakini zaidi!!

Je, ni nani miongoni mwa hao ana uwezekano wa kupata gari bora zaidi? Yule ambae kabla hajaenda Yard amelichunguza umakini gari husika mtandaoni au yule aliyetega barabarani?

Aidha, utafiti huo unaendelea kusema kwamba 7.6% ya ndoa za wanandoa waliokutana kwa njia za kawaida zilivunjika ukilinganisha na 6% ya ndoa zilizovunjika kwa wanandoa waliokutana mtandaoni! Kwa maana nyingine, Watafiti hawa wanatuambia risk ya kuvunjika ndoa za wale waliokutana kwa njia za kawaida ni kubwa zaidi ukilinganisha na wale waliokutana mtandaoni!

Unakubali au unakataa?! Kwanini unakubali au kwanini unakataa?

Kuisoma makala hii kwa urefu: Tujadiliane: Je, unadhani mapenzi ya kukutana mtandaoni ni salama kiasi gani?
 
Hapa nitangulie kusema kwamba, binafsi nimeuelewa sana utafiti uliofanywa na Maprofesa wa Idara ya Sosholojia ya Chuo Kikuu cha Chicago! Nawaelewa, na ndio maana sioni taabu kila wakati kuwapatia habari njema za mtandao wa Dating Tanzania unaoweza kujiunga kupitia https://www.dating.co.tz ambao lengo letu ni kukutanisha watu wenye lengo la dhati la kutafuta wenza serious.

Kwa ufupi utafiti huo unasema kwamba uhusiano unaoanzia mtandaoni huenda ukawa ndio bora zaidi kulinganisha na ule wa kawaida!!! Hoja yao ni kwamba, Online Dating inatoa uwanda mpana zaidi wa kuchagua mwenza sahihi kuliko uhusiano unaotokana na njia za asili!

Wanachojaribu kutuambia hapa ni kwamba, ingekuwa mtu anatafuta gari apendalo basi online dating ni sawa na kuingia kwenye mtandao wa nyumbani (local website) unaouza magari huku mtandao huo ukiwa ume-upload magari ya aina na sifa mbalimbali. Hapo mteja anapata fursa ya kuchagua gari apendalo kwa umakini zaidi kutoka kwenye maelefu ya magari yaliyokuwa uploaded kabla hajatembelea yard iliyohifadhi magari hayo na kuchunguza kwa ukaribu zaidi gari alilolipenda mtandaoni hapo kabla!

Kinyume chake, uhusiano kwa njia za asili ni sawa na mtu anayesimama barabarani au kituo cha magari kama vile Ubungo Terminal huku akijaribu kuchagua gari apendalo kutoka kwenye magari kadhaa yaliyo kwenye mwendo au yaliyoegeshwa kabla hajaenda yard kuchunguza gari husika kwa umakini zaidi!!

Je, ni nani miongoni mwa hao ana uwezekano wa kupata gari bora zaidi? Yule ambae kabla hajaenda Yard amelichunguza umakini gari husika mtandaoni au yule aliyetega barabarani?

Aidha, utafiti huo unaendelea kusema kwamba 7.6% ya ndoa za wanandoa waliokutana kwa njia za kawaida zilivunjika ukilinganisha na 6% ya ndoa zilizovunjika kwa wanandoa waliokutana mtandaoni! Kwa maana nyingine, Watafiti hawa wanatuambia risk ya kuvunjika ndoa za wale waliokutana kwa njia za kawaida ni kubwa zaidi ukilinganisha na wale waliokutana mtandaoni!

Unakubali au unakataa?! Kwanini unakubali au kwanini unakataa?

Kuisoma makala hii kwa urefu: Tujadiliane: Je, unadhani mapenzi ya kukutana mtandaoni ni salama kiasi gani?
SAWA NAWE UTAPATA WAKO JF
USIKATE TAMAA
 
Utafiti wa kijinga huo na wa uwongo ingawa utafiti hupingwa kwa utafiti.

Lengo lao ni kuwachochea watu watongozane sana online,hawana lolote
Na wakishatongozana online wao wanapata nini?! Btw, kuna tofauti gani kati ya wale wanaotongozana online na wale wanaotongazana kwenye vituo vya daladala?! Mambo ya Mswahili unaweza kukuta ndo unataka kuwalaumu wazungu hapo kwamba utafiti wao unalenga kuhamasisha ngono!!!
 
Na wakishatongozana online wao wanapata nini?! Btw, kuna tofauti gani kati ya wale wanaotongozana online na wale wanaotongazana kwenye vituo vya daladala?! Mambo ya Mswahili unaweza kukuta ndo unataka kuwalaumu wazungu hapo kwamba utafiti wao unalenga kuhamasisha ngono!!!
Inshort ni kwamba hamna lolote apo..utafiti wao unaweza ukawa ni very constructive kimaanisha Hao lengo lao ni KUHAMASISHA NA KUCHOCHEA NGONO kivip? tafiti zinaonyesha kwamba matumizi ya simu za kisasa na Internent especially kwa East african countries yanakua kwa kasi so imetumika kama fursa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inshort ni kwamba hamna lolote apo..utafiti wao unaweza ukawa ni very constructive kimaanisha Hao lengo lao ni KUHAMASISHA NA KUCHOCHEA NGONO kivip? tafiti zinaonyesha kwamba matumizi ya simu za kisasa na Internent especially kwa East african countries yanakua kwa kasi so imetumika kama fursa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Typical African ambae kila ovu lake lazima atafute wa kumdondoshea jumba bovu! Waafrika mmeanza kuendekeza ngono karne na karne na ndio maana miaka yote magonjwa hatari kwa Afrika ni yale yanayotokana na ngono halafu leo uje usingizie dating sites ambazo hazijafikisha hata miaka 25! Btw, imetumika kama fursa East Africa kivipi? Utafiti umefanyika US na kuchapishwa kwenye majarida ya US! Sasa suala la East Africa linatoka wapi?!
 
Mbona naona kinyume chake ndio sahihi, hivi unaweza ukasema unachagua kwa umakini mchumba kutoka mtandaoni? Unakuwa unachagua nini? Jina au mwandiko maana mtu humuoni, tabia zake huzijui, hujui kama ni mchawi, mchafu, malaya etc
Mtoto mzuri kuliko wote JF hujambo?! Halafu juzi nakuita halafu unaniletea mapozi; nitakuendea kwa bibi ujue! Anyway, wacha niwahi boti halafu nakuja kukujibu!
 
Mtoto mzuri kuliko wote JF hujambo?! Halafu juzi nakuita halafu unaniletea mapozi; nitakuendea kwa bibi ujue! Anyway, wacha niwahi boti halafu nakuja kukujibu!
Jamani wapi uliniita? Sikusikia mpenzi. Anyways ile nyumba umeshalipia? Nimechoka kukaa uswahilini ujue
 
Bahati mbaya sana niliekutana nae jf kaenda daaahh! Akiuona huu uzi hope atanitafuta
 
shetani hajawahi kushindwa mbele ya watu wajinga mungu tusaidie maana kila mpango wanaopanga unatimia kwa asilikia 90 mpaka 100


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom