raiswenu
JF-Expert Member
- Apr 20, 2018
- 794
- 1,429
Umeshakuwa mtu mzima sasa unajitambua, harakati za maisha zinaendelea kama kawaida, mara unakuja kugundua kuwa wewe ni abortion survivor, mama yako alitaka kuitoa mimba yako. Na wahusika ni baadhi ya ndugu unao ishi nao. How will you react?
Iko hivi nakumbuka nilikuwa kwenye mahusiano na binti flani, tumuite Irene (siyo jina lake halisi), baada ya miezi kadhaa akawa amebeba ujauzito. Kwa mila na tamaduni zetu za kiafrika mtu mstaarabu inabidi ukajitambulishe kwenye familia husika, hivyo nikamtaarifu kuwa ninampango wa kutuma wazee. Kilichonishangaza sasa, alikataa akaniambia subiri kwanza, nilichukulia poa maana nilikuwa sijui ni nini kinaendelea.
Kumbe bwana huyu mdada alikuwa na mchumba anayefahamika mpaka nyumbani, hivyo mimi kwenda kujitambulisha ulikuwa mtihani kwake. Hiki kitu kilinistress sana, maana sasa sikuwa na uhakika na hiyo mimba ni ya kwangu au ya mchumba? Nihudumie au nisihudumie? Niikatae au niikubali? Duh . ila yeye alibaki na msimamo kuwa mimba ni yangu na huyo mchumba ni kwa sababu nyumbani wanamlazimisha kuolewa nae. Mwisho wa siku niliamua kumhudumia.
Sijui ni kukwepa aibu ama nini! Mama yake alianza kulazimisha mimba itolewe, ilikuwa ni vuta nikuvute, mimi nilimkomalia hakuna kutoa mimba, iwe yangu isiwe yangu hakuna kutoa(mtoto hana makosa). Yule mama alishafanya mpaka mpango kwa daktari mimba itolewe binti akagoma kwenda kutoa. Vidonge vya kutoa mimba vililetwa binti akagoma kumeza.
Kufupisha stori, I am a father of a beautiful daughter….very beautiful & intelligent. Juzi huyu binti (Irene)kanitumia video clip mama yake akifurahia kucheza na mjukuu wake(vicheko kama vyote) wakati alitaka kumuua (unafiki). Mjukuu anafurahia kujitupa kwenye miguu ya bibi yake laiti kama angejua kama she wanted her dead. I hope hakuna atakayemwambia , imagine ungekuwa wewe umetambua hiki kitu. How would you react?
Abortion is evil……..!
Iko hivi nakumbuka nilikuwa kwenye mahusiano na binti flani, tumuite Irene (siyo jina lake halisi), baada ya miezi kadhaa akawa amebeba ujauzito. Kwa mila na tamaduni zetu za kiafrika mtu mstaarabu inabidi ukajitambulishe kwenye familia husika, hivyo nikamtaarifu kuwa ninampango wa kutuma wazee. Kilichonishangaza sasa, alikataa akaniambia subiri kwanza, nilichukulia poa maana nilikuwa sijui ni nini kinaendelea.
Kumbe bwana huyu mdada alikuwa na mchumba anayefahamika mpaka nyumbani, hivyo mimi kwenda kujitambulisha ulikuwa mtihani kwake. Hiki kitu kilinistress sana, maana sasa sikuwa na uhakika na hiyo mimba ni ya kwangu au ya mchumba? Nihudumie au nisihudumie? Niikatae au niikubali? Duh . ila yeye alibaki na msimamo kuwa mimba ni yangu na huyo mchumba ni kwa sababu nyumbani wanamlazimisha kuolewa nae. Mwisho wa siku niliamua kumhudumia.
Sijui ni kukwepa aibu ama nini! Mama yake alianza kulazimisha mimba itolewe, ilikuwa ni vuta nikuvute, mimi nilimkomalia hakuna kutoa mimba, iwe yangu isiwe yangu hakuna kutoa(mtoto hana makosa). Yule mama alishafanya mpaka mpango kwa daktari mimba itolewe binti akagoma kwenda kutoa. Vidonge vya kutoa mimba vililetwa binti akagoma kumeza.
Kufupisha stori, I am a father of a beautiful daughter….very beautiful & intelligent. Juzi huyu binti (Irene)kanitumia video clip mama yake akifurahia kucheza na mjukuu wake(vicheko kama vyote) wakati alitaka kumuua (unafiki). Mjukuu anafurahia kujitupa kwenye miguu ya bibi yake laiti kama angejua kama she wanted her dead. I hope hakuna atakayemwambia , imagine ungekuwa wewe umetambua hiki kitu. How would you react?
Abortion is evil……..!