Shemeji yangu akiwa na rafiki zake anasema mimba aliyonayo ni ya mwanaume mwingine japo sisi anatuambia ya ndugu yetu

knows

JF-Expert Member
Nov 9, 2021
1,403
2,006
Habari wakuu.
Naimani wote wazima God anaendela kutupigania achana niende kwenye point.

Nina ndugu yangu kabsa ambae kimiaka tupo sawa sasa kunachangamoto ambayo imempata nduguyangu baada ya wote tulipo maliza chuo changamoto ambayo ni ndogo ila ninzito.

Mwenzangu alikuwa na mahusiano na demu mmoja ivi (Irene) maisha yakasonga sasa dem alikuja akashika mimba na akaamua kutoa taarifa kwa ndugu yangu.

Sasa tatizo likaja wakawa wanapishana demu ataki kuzaa anataka atoe mimba nduguyangu akaja kunieleza mimi mi nikamwambia unajua lakini kwetu sisi kwanzia kiutamaduni wa ukoo wetu mbaka kidini ni marufuku mwanamke kutoa mimba.

Basi ikabidi swala tulifikishe kwa Mzee(baba) na mzee akakataa kuwa huyo binti astoe mimba bas ikabidi mzee atuchukie mbaka kwa wazazi wa huyo binti kufika kule wazazi wake wakagoma wakasema atutaki bint yetu azae hii mimba lazima itolewe kwani bado kuna mambo anaitajika ayafanye ikiwemo kwenda chuo kusoma.

Basi mzee wetu akasema sawa lakini hilo mtajua wenyew na binti yenu lolote litakalo tokea mstushirikishe si tushawaeleza.
Basi tukaondoka baada ya siku kadhaa yule dem akatuambia mimba kashaitoa bas tuka mwambia baridi powah maisha yakaendelea lakini bado hawakuacha na ndugu yangu mahusiano yalikuwepo ila sio kivile kama mwanzo.

Lakini nduguyangu akapata pisi nyingine(Grace) na akaja kuniambia na kunionyesha nikasema baridi ishi nae sasa kilichotokea yule dem jesca akagoma kuachana na mwana So jamaa akawa anawachanganya izo pisi bila kujua.

Sasa kuna day ishu ikaja kujulikana japokuwa uwakika kuwa izo pisi zinachanganywa walikuwa hawana bhas malayakwanza Mimi kama ndugu na shemeji nikasovu kesi ikaisha.maisha yakaendelea japokuwa kesi zilizidi sana kuwa kila dem analalamika kuwa anachitiwa ikafika stage nikachoka kusovu kesi ikabidi nichukue maamuzi magumu ya kutoboa ishu kumueleza dem mmoja(jesca) kuwa anachanganywa bhas dem ikabidi amuulize mwana kuwa kweli nduguyangu akakili ndio bas dem akapisha pembeni akamuachia mwenzie.

Sikufanya kwa ubaya bali kumtoa mwana kwenye matatizo yasio isha kilasiku na mwana akanishukuru sana coz maugonvi yalipungua akawa na amani. Sasa before mwana kuachana na jesca kumbe walikuwa wanagegedana na dem alimwambia tena mwamba kuwa nina mimba tena daah.

ikumbukwe ile ya mwanzo alitoa sasa hii nyingine lakini taarifa zinakuja huyo jesca kumbe alikuwa na bwana mwingine. Nduguyangu kupata taarifa izo ikabidi akatae mimba kuwa sio yake iyoo na dem anasema yakwake. Sasa utata ukawa hapo nakweli dem anamimba kweli na tumbo linaonyesha kabsa. Ikabidi nianze kufatlia Mimi nikaja kugundua nikweli dem ana jamaa mwingine kumbe.

Sasa ikabidi Mimi kama ndugu nimfate dem kumuweka chini na kuhoji vizuri tena kwa kumkazia lakini dem ananiambia shemeji mimi siwez kuku danganya hii mimba niya ndugu yako na swala mimi kuwa natembea na mtu mwingine nikweli kuna mtu nina mahusiano nae mbali na mwenzio daah nikasema fresh nikasepa.

Sasa kipendele kinakuja marafiki zake na dem minawajua kunasiku nilikutana nao nikawa naongea nao na wakanieleza kuwa ile mimba ya jesca sio ya nduguyako ni ya bwanaake mwingine duuh nikaishiwa nguvu nikasema mbona yeye anasema niya nduguyangu wakasema subili tunampigia na tunamuuliza umsike mwenyew anachosema we kaakimya.

Kweli wakampigia apoapo dem kapokea wakaanza kuongea uku wameweka loudspeaker wakamuuliza kuhusu mimba bwanaa weee dema akakana akasema hiyo mimba sio ya nduguyangu kabsa ni ya jamaa yake mwingine duuh acheni nilichoka kabsa.

Sasa wakuu kinacho changanya nikwamba dem kwetu anasema mimba ya nduguyangu kwa rafikizake anasema mimba ni bwanaake mwingine kabsa kiukwe tupo njia Panda hatuelewi wakuu.

Tunaomba ushauri wenu sana nini lakufanya ndomna tumelifikisha huku. Mungu awabariki sana
 
Habari wakuu.
Naimani wote wazima God anaendela kutupigania achana niende kwenye point.

Nina ndugu yangu kabsa ambae kimiaka tupo sawa sasa kunachangamoto ambayo imempata nduguyangu baada ya wote tulipo maliza chuo changamoto ambayo ni ndogo ila ninzito.
We mwandishi boya kweli!! Badala ya kupambana na mfumuko wa bei ujue unatoboaje kesho yako we upobize na mahusiano ya watu bure kabisa wewe😆😂
 
We mwandishi boya kweli!! Badala ya kupambana na mfumuko wa bei ujue unatoboaje kesho yako we upobize na mahusiano ya watu bure kabisa wewe😆😂
Alafu jamaa falama sana baadala ya kukamatia huyo shemeji ajilie anaishia kucheka cheka....fursa hizi watu hawazitumii vizuri
 
Back
Top Bottom