Uswazi na misosi!

Uswazi na misosi!

Kaka umenikumbusha enzi zangu nilipokuwa naishi Tandale kwa Mkunduge

huku ukidai.....
529116_325109044247852_1985267626_n.jpg
 
muhimu sana hiyo maana tunaoishi uswahilini wageni zetu huwa wanavizia mida ya lunch.

Heheheheheh umenikumbusha enZi hizo bwana

Kuna wageni fulani (family friends) wao muda wa kutembelea ni karibia na msosi, sasa mkiwa mnakula wanapita kuchukua nyama tu hahahahah mwenyewe unaiwejea uile mwisho mgeni anaichukua

Hehehe unaishia kula mchuzi
 
Hahahahah hii thread imenikumbusha mbal jaman,nlishawah mchoma my brodah na ugal jichoni kisa kanìibia nyama!lol utoto raha jaman,cku hyo nlichapwa sana na my dady hahah!
 
Mkuu siku ukialikwa ikulu ukakutana na nyama "shazi" utakula mwishoni hizo nyama?

Kuna siku nilijikuta humo ndani kikazi. Wageni walipoondoka kilibaki chakula cha Kumwaga. Nikaona hapa leo wali Utanisamehe. Ilikua ni kuchapa nyama pori,vyuku,samaki,mbuzi,swala,bata yaani mpk unachemsha. Mule ndani jamaa wanafaidi bana.
 
Mi nilikuwa mtaalamu wa kwenda kula ubwabwa kwenye Maulid za watu mtaani.

Mida kama ya saa tano tano hivi unaanza kusikilizia harufu ya pilau.

Ile sinia linapelekwa na wewe huyo tayari ushasogea.

Halafu sasa kabla hata halijawekwa chini watu washaanza kudaka matonge ya nyama.

Mpaka linafika chini nyama zishaisha kilichobaki vifupa tu.

Mwananyamala Visiwani kuna vituko sana aisee.

Kaka nawe ulikulia pande zile? Nilikuwa napanda hadi kwa alimaua na kijitonyama kule kufuata mnuso, hadi ikawa msosi wa home hauna ladha ukilinganisha na wa kugombea kwenye shughuli
 
Mie enzi zangu basi likiletwa sinia la wali yani kabla halijawekwa mezani naanza kuangalia wapi kuna nyama kubwa yani likifika tu naidaka ile nyama kubwa then ndo naendelea kula
 
Mie enzi zangu basi likiletwa sinia la wali yani kabla halijawekwa mezani naanza kuangalia wapi kuna nyama kubwa yani likifika tu naidaka ile nyama kubwa then ndo naendelea kula

Hahhhahhhahha kama mimi aiseee lol
 
Nyama haijawahi kuwa priority yangu kwenye chakula, i just dont like it.

Firigisi nadhani ndo my best nyama
 
Back
Top Bottom