Uswazi na misosi!

Uswazi na misosi!

Hapo kuna ile mnaacha firigisi, au paja ale baba au mgeni. Kuna siku tunapiga mpunga kwenye sinia mbele yangu limekaa paja. Kwa kweli ilibidi nirefushe mkono kuchukua nyama ya mbali kwa sababu paja ni la wakubwa, ngoma ikaenda karibia na finali hakuna mtu wa kuichukua. Wananiambia mbona hauli nyama huku nasuasua nikachangamkia fursa japo nilijisikia vibaya lakini wote wanaelewa taratibu zetu. Ina maana nilikula nyama zaidi ya mgawanyo wa 2 kwa kila mtu. Ilinitokea kwa family friend!

Hahahahahahaaaaaaaaaaa
Mkuu ulikua hatari wewe!!!!!
 
Sie tulikuwa tunaambiwa na mama mboga za majani ndo zinajenga mwili nankuongeza damu so nyama tulikuwa tunakula kwa nadra sana. Siku ya nyama sasa dah nilikuwa sichezi mbali... nikitumwa nawahi kurudi lol nazengea zengea pale jikoni huku nikimuuliza mama... mama nikuonjee kama imeiva? Lol mam was always so kind alikuwa akinipa nionje kidogo
 
Kwani we wabebz umeanza kuwafukuzia ukiwa na umri gani?
Kwa maelezo yako ya kupotea kwenye mdundiko kwa ajili ya kufukuzia mbebz

Nina uhakika ulikua na miaka mitano, sita au saba

Sasa umri huo sidhani kama ulikua unafukuzia wewe ulikua unalishia kuja kustuka ukajikuta umeshafika sinza, umepotea tayari

Ndio maana nikasema ulikuwa hujapevuka
 
1620679_653706044667093_1406226142_n.jpg
Chezea shaba wewe

Kitu rosti kwa juu, aisee
 
Kunguru wakawafanya muwe mnakula nyama kwanza

Kwanini msitengeneze manati mkuu?
Dah! Walikuwa wanakera mbaya, umejipanga ule kuku then anakulenga! Na nia yako n kuku sio wali! So ikabidi strategy zibadilike!
 
ukimlea kiyai yai dada atamfundisha tu. wangu anamiaka 4 dada keshanisaidia kumfundisha kunawa akijisaidia yeye dada anamwagia maji ananawa mwenyewe tena na sabuni

hahahahaha madada wa hawadekezi ukitoka tu wanafanya yao
 
Ikilikuwa kama una history mbaya kwenye minuso ya kuwahi kukimbilia nyama basi nyumbani wako radhi wafunge vioo then wanakununulia kilo moja ya utumbo unapikiwa kisha unaambiwa ukombe hadi iishe yani kitakachofata hapo utakuwa mbali na nyama kabisa
 
Dah! Walikuwa wanakera mbaya, umejipanga ule kuku then anakulenga! Na nia yako n kuku sio wali! So ikabidi strategy zibadilike!

Dawa yao ni manati tu!!!!
 
Ikilikuwa kama una history mbaya kwenye minuso ya kuwahi kukimbilia nyama basi nyumbani wako radhi wafunge vioo then wanakununulia kilo moja ya utumbo unapikiwa kisha unaambiwa ukombe hadi iishe yani kitakachofata hapo utakuwa mbali na nyama kabisa

Hii inaitwa komesha ...lol!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom