Uswazi na misosi!

Uswazi na misosi!

Aaa mie nilikuwa nikilishwa hadi namaliza shule ya msingi!
article-2535141-1A77CBF800000578-179_634x404.jpg

hahahahaha heri yako wewe mimi nimeanza kula mwenyewe na mwaka mmoja tu
ila mwanangu nahisi nitamlea kiyai yai
 
kwa kweli namshukuru sana baba yangu, Mungu amlaze mahala pema peponi..sisi hatukuwa matajiri lakini nyama ilikuwa inapikwa nyumbani kwetu kila siku iendayo kwa Mungu..yani mimi hadi niliichukia nkawa sili nyama..kitu nilikuwa napenda bila kukinai ilikuwa samaki wa kuakaanga kulumangia na maziwa mgando hapo ugali utaenda..
 
Hahaaaa sinia moja mikono ishirini!

Watu wanafinyanga matonge, wanalamba mikono, wanarudi tena kufinyanga.

Ni uchafu lakini kuna raha yake. Leo hii siwezi hata kula ugali na watu halafu wote tuwe tunachovya kwenye bakuli moja.

ila unajua bana ile collabo nzuri sana yani mnapokula kwa umoja kuna connection fulan inakuwepo. I miss that life dah
 
Halafu nani humu keshawahi kunya pombe chafu? Basi bana, mi nshawahi. Kuna mshikaji wangu mmoja anaitwa Eriki, mama yake alikuwa anazipika na kuziuza hizo pombe chafu.

Alianza na kutengeneza ulanzi, akaja akawa anatengeneza kangala, baadaye akawa anatengeneza wanzuki. Kuna kipindi wanzuki ilibamba sana.

Basi bana hapo nyumbani kwa kina Eriki kwa nyuma kule wakapafanya klabu ya pombe. Mtu kama hujawahi kwenda kwenye klabu ya pombe chafu jaribu tu siku moja ukajionee. Nakwambia hata kama una sonona kiasi gani ukienda itaisha tu maana kuna vituko kushinda maelezo.

Mida ya jioni jioni ndo huwa bomba zaidi. Panachanganya sana maana wabeba zege, wauza mkaa, wasukuma mikokoteni na wengineo wa sampuli hizo ndo wanakuwa wanapitia kuzimua kabla hawajaenda makwao.

Ila usafi ndo hivyo tena. Enzi hizo walikuwa wanatumia makopo ya Tan Bond kunywea. Halafu walikuwa wanashea sasa. Likopo lile linajazwa, linazungushwa raundi na kila mtu anapiga sip.

Binafsi sikuzipenda hizo pombe. Zilikuwa chungu chungu hivi. Ila niliipenda sana pombe ya Kibuku. Ila sina hakika kama na hii ni pombe chafu maana ilikuwa inatengenezwa kiwandani pale Ubungo.

Nshanunua sana mimi hiyo pombe. Halafu ukiiwekea sukari ndo ilikuwa inakuwa bomba zaidi. Hata kilevi chake kilikuwa si cha juu kivile. Nashukuru tu sikuoza meno na kutoka mapengo.
 
Mi nilikuwa mtaalamu wa kwenda kula ubwabwa kwenye Maulid za watu mtaani.

Mida kama ya saa tano tano hivi unaanza kusikilizia harufu ya pilau.

Ile sinia linapelekwa na wewe huyo tayari ushasogea.

Halafu sasa kabla hata halijawekwa chini watu washaanza kudaka matonge ya nyama.

Mpaka linafika chini nyama zishaisha kilichobaki vifupa tu.

Mwananyamala Visiwani kuna vituko sana aisee.

Heeh!!, kumbe ndio ww tulikuwa tunakuita chopeko na mnofu enzi zile duh,,ulikuwa na master ya ubunifu na Phd ya hiyo kitu maana sinia ilikuwa haifikichini nyama zimeshakamatwa juu kwa juu utadhani unasumaku.

Kweli ile Mwananyamala visiwani ulikuwa unatisha aisee.
 
Sijui umewaza nini? lol

Nimetoka kwa mama ntilie muda huu na nimekumbuka hii kitu baada ya kumuona jamaa mmoja anafanya hivyo nikamuuliza nae ilibidi acheke sana!
 
Heeh!!, kumbe ndio ww tulikuwa tunakuita chopeko na mnofu enzi zile duh,,ulikuwa na master ya ubunifu na Phd ya hiyo kitu maana sinia ilikuwa haifikichini nyama zimeshakamatwa juu kwa juu utadhani unasumaku.

Kweli ile Mwananyamala visiwani ulikuwa unatisha aisee.

Wacha kabisa! Mwananyamala Kisiwani nna historia ndefu. Jaribu kwenda pale Mwembekona kwa mzee Mapinduzi umwulizie Diego au Bwanyenye watakwambia.....
 
Nyama yaliwa mwisho coz we always spare the best for last...lkn mi naenda viceversa nyama kwanza niishibe kisha ndo naendelea na msosi ha ha haa
 
Kuna watu wanatiririka hadi raha....

Halafu kuna mtindo wa uswazi ambapo watu wote wananawa mikono kwenye bakuli moja (maji kiduchu) ....hadi maji yote yanakuwa brown/chorcolate....

Kisha msosi unapigwa... with good manners, hutakiwi kuvusha mkono juu ya msosi...unakula upande wako!!
 
Mi nilikuwa mtaalamu wa kwenda kula ubwabwa kwenye Maulid za watu mtaani.

Mida kama ya saa tano tano hivi unaanza kusikilizia harufu ya pilau.

Ile sinia linapelekwa na wewe huyo tayari ushasogea.

Halafu sasa kabla hata halijawekwa chini watu washaanza kudaka matonge ya nyama.

Mpaka linafika chini nyama zishaisha kilichobaki vifupa tu.

Mwananyamala Visiwani kuna vituko sana aisee.

Mkuu umenikumbusha jamaa mmoja alikuwa ni mtaala sana wa kujua ilipo misiba,hitma,ubarikio,ubatizo,40 n.k

Huyu jamaa ni noma,alikuwa anakibaraghashia na alikua anaweka ndizi mbivu na pilipili
Ikitokea shughuli yeye anakua yupo kamili ....lol!!!!!!!!!!!!!
 
Halafu kulikuwa na madogo wenye tabia mbaya...

Anaficha finyango zake na wengine wote mkimaliza yeye ndoa naanza kula kwa madaha kama paka aliyeshiba panya... Anawakera kiasi kwamba kama hana ubavu mnamvamia na kumpora....

Mkuu hapa kama ulikua huna ubavu ulikua unamaliza nyama zako mapema maana kama hukua unaweza kupigana basi lazima unyang'anywe na kichapo juu!
 
Back
Top Bottom