Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,914
Hebu leo tucheke kidogo kwa kukumbushana pilika za enzi hizo utotoni hasa kwenye msosi
Kuna mambo ambayo ukiyakumbuka yalivyokuwa enzi hizo za utoto basi unaweza kucheka hadi mbavu zikauma hili ninalokwenda kulizungumzia hapa ni kwa wale tuliokulia uswazi na ambao bado tunaishi Uswazi maana wale watoto wa kishua hii hawakuijua kabisa hivyo wanaweza kuona kama ni hadithi tu
Moja kati ya jambo ambalo nikilikumbuka ni pale kwenye msosi unapokuwa umetengwa mezani,kwa zile familia zetu ambazo ailikuwa na uwezo wa chini kidogo kulipokuwa kunapikwa nyama basi siku hiyo kwenye msosi mezani zinaweza kupigwa ngumi kwa kugombea finyango za nyama,kwa kuepusha hilo wazazi walikuwa wanahesabu finyango kwa idadi yetu wote na kabla ya kuanza kula mlikuwa mnaambiwa "mtakula kila mmoja finyango mbilimbili" na baada ya hayo kila mmona alikuwa anatoa finyango zake na kuziweka kwenye bakuli kubwa au sinia ambalo ugali umewekwa na kuanza kuchovya mchuzi na mchika kama utakuwepo
Lakini kuna kitu amcacho nadhani kimetuathiri kutokana na hii kitu ya utotoni,huku ukubwani nimeona watu wengi sana wakiwa wanakula hasa kwetu ambao tunakula kwa mama ntilie,utaona kuwa mtu kama ameagiza wali na nyama au ugali na samaki basi nyama au samaki huachwa na kuja kuliwa mwishoni,sijui hii ni kwasababu gani
Lakini kwa uchunguzi wangu mdogo nimegundua kuwa ile dhana ya utotoni ya kuthamini sana vitoeo kama vile nyama husababisha kuona kama ni vya thamani sana na hupelekea watu kuacha na kuvila mwishoni ili auone utam wake .....lol
Nimeshaona wengi sana kwenye hili lakini kila nikiona huishiakucheka na kukumbuka mbali sana zile enzi za vurugu kwenye msosi
Vipi,wewe ukiwa kwenye msosi unaousisha kitoweo kama kuku,au nyama ya ng'ombe unaacha vile vi finyango hadi mwishoni au unakula bila kuzingatia kuwa kuna finyango?
Hebu tukumbuke kidogo na tufurahi na kucheka hizi enzi zetu za uswazi!!!!!!
Kuna mambo ambayo ukiyakumbuka yalivyokuwa enzi hizo za utoto basi unaweza kucheka hadi mbavu zikauma hili ninalokwenda kulizungumzia hapa ni kwa wale tuliokulia uswazi na ambao bado tunaishi Uswazi maana wale watoto wa kishua hii hawakuijua kabisa hivyo wanaweza kuona kama ni hadithi tu
Moja kati ya jambo ambalo nikilikumbuka ni pale kwenye msosi unapokuwa umetengwa mezani,kwa zile familia zetu ambazo ailikuwa na uwezo wa chini kidogo kulipokuwa kunapikwa nyama basi siku hiyo kwenye msosi mezani zinaweza kupigwa ngumi kwa kugombea finyango za nyama,kwa kuepusha hilo wazazi walikuwa wanahesabu finyango kwa idadi yetu wote na kabla ya kuanza kula mlikuwa mnaambiwa "mtakula kila mmoja finyango mbilimbili" na baada ya hayo kila mmona alikuwa anatoa finyango zake na kuziweka kwenye bakuli kubwa au sinia ambalo ugali umewekwa na kuanza kuchovya mchuzi na mchika kama utakuwepo
Lakini kuna kitu amcacho nadhani kimetuathiri kutokana na hii kitu ya utotoni,huku ukubwani nimeona watu wengi sana wakiwa wanakula hasa kwetu ambao tunakula kwa mama ntilie,utaona kuwa mtu kama ameagiza wali na nyama au ugali na samaki basi nyama au samaki huachwa na kuja kuliwa mwishoni,sijui hii ni kwasababu gani
Lakini kwa uchunguzi wangu mdogo nimegundua kuwa ile dhana ya utotoni ya kuthamini sana vitoeo kama vile nyama husababisha kuona kama ni vya thamani sana na hupelekea watu kuacha na kuvila mwishoni ili auone utam wake .....lol
Nimeshaona wengi sana kwenye hili lakini kila nikiona huishiakucheka na kukumbuka mbali sana zile enzi za vurugu kwenye msosi
Vipi,wewe ukiwa kwenye msosi unaousisha kitoweo kama kuku,au nyama ya ng'ombe unaacha vile vi finyango hadi mwishoni au unakula bila kuzingatia kuwa kuna finyango?
Hebu tukumbuke kidogo na tufurahi na kucheka hizi enzi zetu za uswazi!!!!!!