Usumbufu wa Mashirika ya Ndege Dar es salaam

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Ndugu Wa Tanzania

Tumepokea malalamiko ya watu wa rika mbali mbali toka mwaka jana juu ya mashirika ya ndege hapo Dar es salaam wanavyo wasumbua watanzania wanao taka kusafiri kwenda nchi za nje kwa sababu mbali mbali.

Vijana wanatafuta fursa mbali mbali za halal kabisa za kwenda nje ,kimatembezi wengine kikazi, wanapatiwa visa halali kabisa kutoka balozi za nchi.

Wanapo fika Airport kupatiwa boarding pass hapo ndio shughuli mpya, huwasumbua na kuwakatalia kuwapa ticket kwa kisingizio eti hawatarudi Tanzania, hivi wakirudi au wasirudi wewe kama shirika la ndege ni kazi yako ? Ni maamuzi ya mtu mwenyewe.

Mtu anapo fika nchi kama za ulaya ,America na Canada kuna fursa mbali mbali, kama ni mgeni halali kabisa, fursa za kuishi huko zipo kisheria, Sasa shirika unamnyima Mtanzania boarding pass kwani wewe ni nani ?

Na mbaya zaidi mashirika hupiga simu kwenye balozi wakati mwengine na kuziharibu visa zao wasafiri.

Tunaomba serikali , Uhamiaji na sector nyengine kutupia jicho haya mashirika na wasafiri kwa usumbufu wanao pata hapo Airport.

Rais Samia pamoja na mabalozi wetu wamekuwa wakitu hangaikia ndani na nje ya nchi ili tuweze kupata Ajira, na kukuza uchumi wetu

Ahsante
Diaspora
 
Jana kuna vijana wengi wamerudishwa nyumbani ihali wakiwa na visa halali za kusafiri na shirika la KLM ,sababu zao zisizo na msingi, na jealous tu hakuna kitu chengine. KLM wachukue hatua haraka au tutatuma barua kwa shirika lenyewe nchini uholanzi na pia Tutatuma barua Uhamiaji

Diaspora
Shukran
 
Ndugu Wa Tanzania

Tumepokea malalamiko ya watu wa rika mbali mbali toka mwaka jana juu ya mashirika ya ndege hapo Dar es salaam wanavyo wasumbua watanzania wanao taka kusafiri kwenda nchi za nje kwa sababu mbali mbali.

Vijana wanatafuta fursa mbali mbali za halal kabisa za kwenda nje ,kimatembezi wengine kikazi, wanapatiwa visa halali kabisa kutoka balozi za nchi.

Wanapo fika Airport kupatiwa boarding pass hapo ndio shughuli mpya, huwasumbua na kuwakatalia kuwapa ticket kwa kisingizio eti hawatarudi Tanzania, hivi wakirudi au wasirudi wewe kama shirika la ndege ni kazi yako ? Ni maamuzi ya mtu mwenyewe.

Mtu anapo fika nchi kama za ulaya ,America na Canada kuna fursa mbali mbali, kama ni mgeni halali kabisa, fursa za kuishi huko zipo kisheria, Sasa shirika unamnyima Mtanzania boarding pass kwani wewe ni nani ?

Na mbaya zaidi mashirika hupiga simu kwenye balozi wakati mwengine na kuziharibu visa zao wasafiri.

Tunaomba serikali , Uhamiaji na sector nyengine kutupia jicho haya mashirika na wasafiri kwa usumbufu wanao pata hapo Airport.

Rais Samia pamoja na mabalozi wetu wamekuwa wakitu hangaikia ndani na nje ya nchi ili tuweze kupata Ajira, na kukuza uchumi wetu

Ahsante
Diaspora
watu wana wivu sana aisee
ndo maana tunalogana
 
atlcl wanasumbua sana hasa hizi sehemu wanapeleka tundege tumoja aU TUWILI kwa wiki
wanafunga mfumo wa booking na kuuachia usiku wa manane na kesho yake saa 12 ndo safari inaanza
matokeo yake tunakatiwa tiketi kwa bei kubwa na seat zinabaki bila kujazwa
huu ni uhujumu uchumi
Sitosahau siku nimesafiri kwenda mkoani kutokana na huo upuuzi kwa 687,000/= return,

Nauli kubwa kuliko ata ya DXB 💔
 
Tanzania pana tatizo sana huko bado tunaona ndege ni kitu cha ajabu mno utasikia kusafiri baadhi ya Nchi za Africa hasa SA ambako mpaka usafiri wa Truck upo wanataka uwe na return Ticket ila ukiwa hizi Nchi Malawi,Zambia shirika hilo hilo unakata Ticket moja tuu tena toka zamani sisi tuna ujinga fulani ambao upo kwenye damu..
 
Airport wameajiriwa watu wasio na sifa au hadhi ya huduma kwa wasafiri,
Msafirishaji jukumu lake ni kuhakikisha una 1.passport ya Kusafiria
2. Ticket ya ndege
3. Visa

Lakini airport yetu hawa wanakua tofauti, anakuuliza invitation letter iko wapi? Address ya unaposhukia hiyo nchi unayoenda, booking ya hotel na wanataka ulipie,
Hii yote ni kutaka RUSHWA kwa nguvu ndio maana kukwepa huu usumbufu vijana wadogo under 30 huchagua kwenda kupanda ndege Nairobi.

“PEOPLE LUCK EXPOSURE”

Ni wivu wa hali ya juu kumnyima msafiri boarding pass huku akiwa amekidhi vigezo vyote vya safari, kama unshisi anapoenda atadhurika kuna balozi kwenye hizo nchi itamsaidia.
People need to change aise
 
Back
Top Bottom