Usiyoyajua kuhusu Che Guevera

Usiyoyajua kuhusu Che Guevera

Kosa kubwa alifanya ni kuruhusu kukamatwa.
 
Haya
Aisee kuna baadhi ya binadamu wanaumea kwa sababu ya maisha duni wanayoishi wengine

kuna watu wanaandika majina yao vizuri kama CHE GUEVARA na wengine wanaandika majina yao vibaya kama HITLER
Haya makinikia ya kwetu wanapenda tu kuweka majina yao kwenye vitu vikubwa vikubwa ambavyo hata hawajafika kusaidia kwa lolote. STUPID IDIOTS!!!!
 
Mkuu ongezea na hili,

Jina alilotumia Che kuingia Congo kwa mara hiyo ya pili lilikuwa Ramon Benetiz.
Baada ya Che kujifunza Kiswahili kidogo, alijipa yeye mwenyewe na wenzake hao wawili majina ambayo ingekuwa rahisi kwa Wacongo kuwaita. Dreke, aliyekuwa wa pili baada ya Che, akaitwa Moja, Papi akaitwa Mbili na Che akajiita Tatu.
Aprili 20, siku moja tu baada ya kuwasili, Che na watu wengine 14 wakaondoka Dar es Salaam kwa gari kuelekea Kigoma. Barabara ilikuwa mbaya wakati huo na safari yenyewe ilichukua siku mbili. Kwa mujibu wa maelezo ya kwenye Pasajes, Che na wenzake walipanda boti kupitia Ziwa Tanganyika na kwenda Congo.
Che alikaa katika mapambano ya kumsaidia Kabila dhidi ya majeshi ya Joseph Kasavubu na baadaye Mobutu Sese Seko kwa muda wa miezi saba. Wacuba waliokuwa na Che hawakufanikiwa katika azma yao.
Katika kitabu cha Anderson kuhusu Che nilichokieleza kabla, yaliandikwa mengi kuhusu namna Che alivyoshindwa kutimiza azma yake. Mosi, ni aina ya viongozi ambao aliwakuta Congo ambao hawakuwa wakifanana kitabia na mtu kama Castro.
Wakati akina Castro walipambana katika eneo la milima la Sierra Maestra kila siku bila kutoka, Kabila alionekana kwenye uwanja wa mapambano mara moja tu katika wakati wote ambapo Che alikuwa vitani.
Mara zote Kabila na wenzake walikuwa na udhuru wa kutokuwepo vitani. Wanamapinduzi wa aina ya Kabila walikuwa wakifanya siasa zao kwenye viwanja vya ndege, hoteli za kitalii na majiji makubwa duniani.
Che aliporudi Dar kutoka Congo alilalamika kuhusu wapiganaji wa Kabila. Alisema alivunjika moyo nao kwa vile hawakuwa na maana na kwamba mara nyingi wakivuta bangi tu.
Kama walivyo wanamapinduzi wengine mahiri, Che Guevara pia alikiri makosa yake binafsi kwenye vita hiyo ya Congo ambayo ilishindwa kupata matokeo yaliyotarajiwa.Akiandika katika kitabu chake hicho cha Pasajes de la Guerra Revolucionaria (Congo), Che aliandika.
“Kuna mambo kadhaa ambayo pengine sikuyafanya vizuri kwenye mapambano yale. Labda nilikuwa mkali sana kwa askari wangu. Nilikuwa nikitumia mbinu za adhabu ambazo wakati mwingine si za kawaida kwa askari kama vile kuwashindisha njaa.
“Pili, nilikuwa na uhusiano mzuri na wananchi masikini na askari wa chini kuliko wale wa ngazi za juu. Kasoro ninayoijutia ni kwamba sikujifunza vya kutosha lugha ya Kiswahili na hili lilininyima fursa ya kuwasiliana vizuri na watu wengi zaidi.
“Nimejifunza mengi Congo; yakiwamo makosa ambayo sitaraji kuyarudia. Labda yatakuwepo mengine ambayo nitayarudia na mengine mapya nitakayoyafanya. Sasa nimeamini zaidi kuhusu mapambano haya ya msituni dhidi ya ubeberu kuliko ilivyokuwa kabla.Sitasahau kuhusu kushindwa kwangu huku na mafunzo haya niliyojifunza Congo.
Jina lake linatamkwa vipi?
 
Hio ya kuuliwa na mwanajeshi mlevi sijaipata vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
Mario Terán wakati huo alikua ni Mwanajeshi (Sajenti) wa miaka 27 aliyekuwa na tabia ya ulevi (Alcoholic). Alijitolea kumuua Guevara kwa nia ya kulipiza kisasa baada ya wanajeshi wenzake watatu aliokuwa nao kwenye COMBANIA moja (B-Company) (wote waliitwa "Mario") kuuwawa na jeshi lililokuwa likiongozwa na Guevara.
 
Mario Terán wakati huo alikua ni Mwanajeshi (Sajenti) wa miaka 27 aliyekuwa na tabia ya ulevi (Alcoholic). Alijitolea kumuua Guevara kwa nia ya kulipiza kisasa baada ya wanajeshi wenzake watatu aliokuwa nao kwenye COMBANIA moja (B-Company) (wote waliitwa "Mario") kuuwawa na jeshi lililokuwa likiongozwa na Guevara.
Samahani mkUu Alikua Ni mwanajeshi wa nchi Gani ???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ongezea na hili,

Jina alilotumia Che kuingia Congo kwa mara hiyo ya pili lilikuwa Ramon Benetiz.
Baada ya Che kujifunza Kiswahili kidogo, alijipa yeye mwenyewe na wenzake hao wawili majina ambayo ingekuwa rahisi kwa Wacongo kuwaita. Dreke, aliyekuwa wa pili baada ya Che, akaitwa Moja, Papi akaitwa Mbili na Che akajiita Tatu.
Aprili 20, siku moja tu baada ya kuwasili, Che na watu wengine 14 wakaondoka Dar es Salaam kwa gari kuelekea Kigoma. Barabara ilikuwa mbaya wakati huo na safari yenyewe ilichukua siku mbili. Kwa mujibu wa maelezo ya kwenye Pasajes, Che na wenzake walipanda boti kupitia Ziwa Tanganyika na kwenda Congo.
Che alikaa katika mapambano ya kumsaidia Kabila dhidi ya majeshi ya Joseph Kasavubu na baadaye Mobutu Sese Seko kwa muda wa miezi saba. Wacuba waliokuwa na Che hawakufanikiwa katika azma yao.
Katika kitabu cha Anderson kuhusu Che nilichokieleza kabla, yaliandikwa mengi kuhusu namna Che alivyoshindwa kutimiza azma yake. Mosi, ni aina ya viongozi ambao aliwakuta Congo ambao hawakuwa wakifanana kitabia na mtu kama Castro.
Wakati akina Castro walipambana katika eneo la milima la Sierra Maestra kila siku bila kutoka, Kabila alionekana kwenye uwanja wa mapambano mara moja tu katika wakati wote ambapo Che alikuwa vitani.
Mara zote Kabila na wenzake walikuwa na udhuru wa kutokuwepo vitani. Wanamapinduzi wa aina ya Kabila walikuwa wakifanya siasa zao kwenye viwanja vya ndege, hoteli za kitalii na majiji makubwa duniani.
Che aliporudi Dar kutoka Congo alilalamika kuhusu wapiganaji wa Kabila. Alisema alivunjika moyo nao kwa vile hawakuwa na maana na kwamba mara nyingi wakivuta bangi tu.
Kama walivyo wanamapinduzi wengine mahiri, Che Guevara pia alikiri makosa yake binafsi kwenye vita hiyo ya Congo ambayo ilishindwa kupata matokeo yaliyotarajiwa.Akiandika katika kitabu chake hicho cha Pasajes de la Guerra Revolucionaria (Congo), Che aliandika.
“Kuna mambo kadhaa ambayo pengine sikuyafanya vizuri kwenye mapambano yale. Labda nilikuwa mkali sana kwa askari wangu. Nilikuwa nikitumia mbinu za adhabu ambazo wakati mwingine si za kawaida kwa askari kama vile kuwashindisha njaa.
“Pili, nilikuwa na uhusiano mzuri na wananchi masikini na askari wa chini kuliko wale wa ngazi za juu. Kasoro ninayoijutia ni kwamba sikujifunza vya kutosha lugha ya Kiswahili na hili lilininyima fursa ya kuwasiliana vizuri na watu wengi zaidi.
“Nimejifunza mengi Congo; yakiwamo makosa ambayo sitaraji kuyarudia. Labda yatakuwepo mengine ambayo nitayarudia na mengine mapya nitakayoyafanya. Sasa nimeamini zaidi kuhusu mapambano haya ya msituni dhidi ya ubeberu kuliko ilivyokuwa kabla.Sitasahau kuhusu kushindwa kwangu huku na mafunzo haya niliyojifunza Congo.

Kingine kilichomkwaza ni ile tabia ya watu kula watu. Unakamata mateka kisha unamla nyama. Alisema hayo si mapinduzi.
 
Aha ... kwasababu Kuna habari moja niliisoma kuhusu huyu jamaa Nikaona CIA walihusika sana katika mauaji ya huyu mtu

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiasi flani CIA walijaribu kumtafuta ila pia Historia inasema hakuna Mtu aliyekuwa anaogopwa na CIA kama Ernesto Guevara. Philip Agee ambaye alikuwa CIA agent (1957-1968) anasema "There was no person more feared by the company (CIA) than Che Guevara because he had the capacity and charisma necessary to direct the struggle against the political repression of the traditional hierarchies in power in the countries of Latin America"
 
Kiasi flani CIA walijaribu kumtafuta ila pia Historia inasema hakuna Mtu aliyekuwa anaogopwa na CIA kama Ernesto Guevara. Philip Agee ambaye alikuwa CIA agent (1957-1968) anasema "There was no person more feared by the company (CIA) than Che Guevara because he had the capacity and charisma necessary to direct the struggle against the political repression of the traditional hierarchies in power in the countries of Latin America"
Shukrani sana nimekuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliambiwa huyu jamaa alitoroka jela ya katika bahari na akaogerea hadi nchi kavu...

Source; katika kijiwe chetu cha kahawa
 
Back
Top Bottom