Usithubutu kukopa pesa Platinum au Bayport matapeli hawa

Usithubutu kukopa pesa Platinum au Bayport matapeli hawa

Hawa jamaa ipo siku watafilisika na kulala mbele hawafai
 
Jamaa ipo siku watakosa wateja na kampuni zao zinakwenda kufa na kufilisika ..muda utaongea
Hilo sahau maana kila siku wajinga wanaendelea tu kuongezeka, huku hizo kampuni zikitumia kila aina ya mbinu kuwashawishi!!

Tamaa ya mkopo wa chap chap, ahadi hewa, ujinga na kukurupuka! Havijawahi kuwaacha salama baadhi ya wafanyakazi, na hasa wale wa serikali.
 
Wanatozaga riba kwa mwezi ni 5%
Kwahiyo 5%×12=60% apr!
Maana yake ukikopa 10m riba kwa mwezi ni laki 5, mwaka ni 6m!
Serikali iko wapi watu wake wanaumizwa hivi? Lazima kuna mkono wa mtu humo.

Huu ni wizi wa mchana "daylight robbery". Lakini tusiwalaumu wakopaji kwamba wote ni wajinga, wengine hupata shida kama ada ya shule, kuuguliwa, kesi mahakamani nk. na kulazimika kulipa, ni utmuwa.

Serikali inayowajali wanyonge isingeruhusu mikopo ya aina hii.

Hata sheria ya kima cha chini cha mshahara lengo lake ni kumlinda mfanyakazi asinyanyaswe na mwajiri kwa malipo duni, lakini bongoland serikali ndiyo ya kwanza kumlinda tajiri kwa kisingizio cha kuvutia wawekezaji.

Hawaelewi kwamba mwekezaji wa kwaza nchini ni mwananchi, mlipakodi namba moja! Hao wengine kuna siku watakosekana au waliopo wataondoka kwenda mahali pengine kwenye maslahi bora zaidi, lakini mwananchi yupo siku zote na ukimwezesha (ukimlinda asiporwe fedha na hawa maharamia) atakulipa kodi zaidi.


Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
Hilo sahau maana kila siku wajinga wanaendelea tu kuongezeka, huku hizo kampuni zikitumia kila aina ya mbinu kuwashawishi!!

Tamaa ya mkopo wa chap chap, ahadi hewa, ujinga na kukurupuka! Havijawahi kuwaacha salama baadhi ya wafanyakazi, na hasa wale wa serikali.
... na hasa Walimu..
 
nimekopa mil moja kwa mwaka nimerudisha 1.2mil halafu pesa hyo nilipewa aslimia 99.9 kwene ac yang wanakata asilimia moja tu ya mkopo wanaokuwekea,,ex 1mil ni elfu 10
Wanatozaga riba kwa mwezi ni 5%
 
nimekopa mil moja kwa mwaka nimerudisha 1.2mil halafu pesa hyo nilipewa aslimia 99.9 kwene ac yang wanakata asilimia moja tu ya mkopo wanaokuwekea,,ex 1mil ni elfu 10
Watu hatupendi rudisha pesa mkuu
 
kukopa tunapenda ila kurudsha inakuwa maneno ila kwa beiport na platnum hata mm shaid na matapel kinoma maden yao hayaish mkuu..
Sijui mkuu, sitetei mtu. Ila kama unakopa muhimu uwe na record za kiasi ulichopewa na utunze kumbu kumbu, wakupe mfumo wa marejesho uweke record. then lipa with ushaihidi mkuu.. ukimaliza deni lao na ushidi unao zipo sehemu za kuwapeleka.. kuliko kulia lia bila ushihid unaonkena kama umeishindwa lipa deni
 
nimekopa mil moja kwa mwaka nimerudisha 1.2mil halafu pesa hyo nilipewa aslimia 99.9 kwene ac yang wanakata asilimia moja tu ya mkopo wanaokuwekea,,ex 1mil ni elfu 10
Acha uwongo wa mchana kweupe,

Weka hapa mkataba wa huo mkopo wako.
 
hahaha huamini mkuu mteja mzur sana wa maboto ntakuja nikupe ushahid mkuu
Sio utakuja kuweka,
Weka hapa ushahidi sahv

Sio kwamba Wote wanaolalamika humu page zaidi ya 300 Ni wapuuz au wanaongelea vitu vya kufikirika.

Hao jamaa Ni majambaz,
Unapinga Hilo lete ushahidi na SIO stories.

Vinginevyo
utwaambie na wewe Kuna namna flan unafaidika na huu uhuni wao.

Hivyo unawasafisha ili mambo yako yakunyokee.
 
Back
Top Bottom