Usithubutu kukopa pesa Platinum au Bayport matapeli hawa

Usithubutu kukopa pesa Platinum au Bayport matapeli hawa

Ndugu wana jf hizi kampuni za kukopesha fedha zina usumbufu sana riba yao kubwa kudai loan balance wasumbufu, ukitaka kufuta deni hawakubali.

Ndugu wana jf nawashauri acheni kukopa kwa hawa majamaa ni matapeli sana kuwa makini
Kwani hukosoma vigezo vyao?
Wewe uli default mkopo tu ukapambana na makucha yao
 
Ndugu wana jf hizi kampuni za kukopesha fedha zina usumbufu sana riba yao kubwa kudai loan balance wasumbufu, ukitaka kufuta deni hawakubali.

Ndugu wana jf nawashauri acheni kukopa kwa hawa majamaa ni matapeli sana kuwa makini
Usipoeleza umepigwaje uzi wako unabaki kuwa majungu tu.
 
Nyie nao watanzania mna utapeli tapeli katika masuala ya Mkopo, hamna nidhamu na fedha, unakopa kwa kicheko ukidaiwa kurejesha unaanza vita, na ndio maana mtoa mada hajawah kuelezea kiudani nini shida za hao jamaa.

Najua baadhi wana changamoto kweli ila na watanzania ni changamoto zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Crdb, nmb, nbc hamuzionagi au hao KWAKUA hua wanawafata maofisini mwenu kiwagonga saundi
 
Nakuelewa mleta uzi.
Kulikuwa na manz flan nilikuwa napiga akaenda kukopa milion 4 kwa dhamana ya gari. Kwanza picha inaanza wakaanzisha makato wakati hela hawajaingiza kwenye account Kufika muda wa kumaliza mkopo(ulibaki milioni 2 akataka kumaliza wote atemane nao)

Ajabu walianza visa kwa kuleta balance isiyo sahihi na ile waliokuwa wanampa kwenye statement tukagombana wee mpk wakakubali ikafika muda wa kubadili kadi ya gari watoe title yao pale

Asee napo muziki ulikuwa mkubwa kama mwezi mzima wanasema system yao inasumbua kuondoa title hadi waite IT sijui nin huko.

Siku yule manzi aliniita nikamsaidie nikamwambia poa nipitie muda wa mchana tukaenda ofisi zao pale morocco nikamchukua na jamaa yangu mwanasheria tulienda kuwasha moto balaa pale tukawapa siku 3 tunafungua kesi mbona walibadili chap tu.

Ndio nikaona jamaa ni wababaishaji tu na waongo waongo.
 
Nimeona baadhi yenu mnajifanya kuuliza shida yao ni nini mnawatetea 😅 tunajua nyie ni mawakala wao uchwara, ila ngoja niwatajie shida zao...
1. Hawatak uwalipe mkopo wao ukipata cash
2. Hawatak kutoa loan statement, wanajionaga wajanja kumbe mapunga
3. Hawatak kuruhusu bank nyingine inunue mkopo wako kwao, ni wapuuzi
4. Wakikubari kukupa loan statement wanakubambikizia deni kubwa ili ughairi ubaki nao, maboga tu hawa
5. Hawatak kukuonyesha mikataba yao na watakulazimisha ujazie ofisini kwao hio mikataba, vilaza sana
6. Kabla hawajakupa mkopo wanaanza kukukata mshahara, ukiwauliza mbona hamjanipa mkopo bado wanakujibu usihofu system tu imewah, hwana akili
7. Mkopo wao haushi mfano kama mkopo wao unaishia mwezi August wataendelea kukukata tu hadi ugombane nao, lengo lao ukate tamaa ushawishike kukopa tena Wasenge sana
8. Mkopo wako ukibak miez michache kuisha watakusumbua kukupigia cm kukushawish ukope tena, maanina zao
9. Ukipata mkopo watakupigia cm kukuomba hela ya soda eti wamekumbambania umepata mkopo.

MIMI WAKIJA OFISINI HUWA NAWAFUKUZA NA HAWAPAT NAFAS YA KUONGEA HATA NA MTU, NA BAHAT NZURI HUWA NATEMBELEA WADAU WILAYANI NA MIKOANI NAWAELIMISHA KUHUSU UTAPELI WAO, CHA KWANZA NIKIKAA KIKAO NA WADAU WANGU NAWAPIGA MARUFUKU KUKOPA KWENYE TAASIS ZA KIPUUZI KITAPELI KAMA BAYPORT, PLATINUM, BARCLAYS, NA VITAASISI/VIBENKI UCHWARA...

Watu wengi sana wametapeliwa na hao watu, bahat nzuri sijawah kukopa kwao, hayo niliyo andika ni malalamiko ya wateja wao kutoka maeneo tofaut tofaut...
 
Back
Top Bottom