Usiombe yakukute jamani, daah!!!

Usiombe yakukute jamani, daah!!!

Pole sana rafiki, hapo sasa ndo panaitwa Golgota ya Tanga!!
 
Mtu ana watoto wawili analazimisha awe mkeo? Huyu anaujasiri namna hii ni hatari kwa afya yako na familia yako kwa njia yoyote ile hata ndumba.
 
Mwalimu ndo mke wako halali wa ndoa, huyo unasema sijui unahisia naye atabaki kuwa mchepuko. Na ukitaka LAANA ikufuate maisha yako yote thubutu kumwacha mwalimu wa Singida nakuambia hakuna rangi utaacha kuona chini ya jua.

Ngoja kwanza nikutoe tongotongo kitendo cha huyo wa Tanga kujikata mkono ni dalili mbaya mbele ya maisha yako ukishi naye, pili umesema ana watoto wawili. Je ulishawahi kufuatilia historia ya kuzaa na kuachana na hao wanaume? Huyo mwanamke amekuzidi akili, kitendo cha kuzaa na wewe huku akijua una mkeo ameshakusoma your strength and weakness na akaona huwa akikufanyia XYZ huwezi kubanduka. Mbaya zaidi hata ukimwacha mkeo wa Singidani hayo mapenzi yake ni sawa na nguvu ya Pepsi, yataisha tooo slowly.

Ushuri wa kijinga: Jenga mazingira ya kumwacha silent abaki kuwa mmezaa mtoto na utamlea mwanao, mwanao akikua mchukue akaungane na mkeo Singidani baada ya kutubu hiyo dhambi kwa mkeo mwalimu.

Pili, fanya juu na chini uhame Tanga either uhamie Singida kama mna ofice branch huko au uhamie kwingine jirani na mwalimu
Tatu, kwa kuwa unalia sana swala la hisia wewe uhame au mkea ahamie mkoa mwingine utakao hamia, urudishe mapenzi ya awali kwa mwalimu
Huu ushauri,una mantiki sana nimeukubali Brother Great CHUKUA HUU USHAURI
 
Jambo usilo lijua ni kwamba wanume mara nyingi huoa wanawake wanaohisi hawawapendi sana kama wa huyo jamaa.

Pili wanaume wengi bila shinikizo toka kwa mwanamke wake anajiona hayuko tayari kuoa muda husika. Huwa kuna kusita sita na ndio maana jamaa alipompa mimba ya kwanza mwanamke wa kwanza alijiona hayupo tayari kuwa na mtoto.

Jamaa mke wake ambae atadumu nae bila kero ni yule wa kwanza sababu anaonesha anampenda kwa dhati na mvumilivu.

Huyo wa Tanga akishajihakikishia ndoa na mtoto tayari jamaa atajuta kumfahamu. Hapo mtoto ametumika amemtumia kama blackmail kwa jamaa sababu anahisi mtoto ndio kitu kinachomfanya jamaa amchague mwanamke wa kwanza.
Umeongea ukweli mtupu!!!
 
Hiyo picha imenikata stimu halafu na wewe mtoa mada ni mtu wa ovyo sana ungekuwa ndugu yangu ningesikitika sana ila ingawa sikujui bado nasikitika sana akili yako ni ya kijinga mnoo kwa Maisha unayoishi na ujinga unaofanyiwa na hao wanawake wote wawili.
 
Kwako ThaGreatman . Ndugu yangu hapo unaishi na nyoka. Ni suala la muda tu atakung'ata . Hebu jaribu kujiuliza, kama ameweza kujitendea hivyo yeye mwenyewe siku akili yake itakapomtuma kukudhuru wewe atakufanyaje? Nikipata muda ntakufundisha mbinu zakumfanya mwanamke akuchoke, akuchukie na kukuacha mwenyewe bila kukulaumu wala kujilaumu. Asante kwa leo.
Mkuu naomba utupe angalau mbinu usisahau
Tujinasue maana wengine tumecheza hattrik zote lakin wapi
 
Ndugu zangu,ukisikia njia panda Kali ndiyo hii!!
Mwaka 2010 niliachana na mpnz wangu nliyempenda sanaaa,ktk kipindi hicho cha mpito nilikutana na msichana mmoja mkoani huko,nikamtongoza ki-maskhara sana,(sikuwa serious kwa sababu sikumpenda kwa kweli) akakubali,nikajisemea moyoni huyu nakula then simrudii tena!

Kweli,nikamla msichana yule,(alikuwa mwaka wa kwanza Chuo cha diploma huko Mkoani),kwa uzembe wetu hatukutumia kinga,baada ya miezi kadhaa akaniambia anahisi ni mjamzito,nilishtuka kweli kwa sababu sikutaka kabisa kuwa na mtoto japo sikuchukua tahadhari kuliepuka hilo. Sikuikataa bali nilimshawishi atoe ile mimba,nikamtumia mpaka pesa ya kutolea,akakataa kabisa kuitoa na pesa yangu akanirudishia!(nikamtumia tena imsaidie kwa mambo yake mengine)

Baada ya mwaka mmoja,alijifungua mtoto anafanana na mimi sanaaa,hata kukataa isingewezekana,nikakubali kulea mtoto. Miaka miwili baadaye nikaanzisha mahusiano mengine,hayakudumu kwa sababu ya huyu mama wa mtoto wangu alikuwa karibu sana nami kimawasiliano juu ya maswala ya mtoto,jambo ambalo lilimkera mpnz wangu hiyo,akaamua kuachana na mimi!

Miaka yote hiyo tulikuwa tunakaa mbali mbali na huyo mama wa mtoto wangu,kutokana na upweke nilimuita Hugo mama wa mtoto nikae naye angalau kidogo niweze kutafuta kumpenda,then tuangalie uwezekano wa kuishi pamoja.(tulikaa kama miezi mitatu hivi kwa matazamio)

Ukweli alikuwa msichana mpole asiye na makuu,nikaamua kumtambulisha nyumbani rasmi,na kutambulika kuwa Huyo ndiye mchumba wangu!(akarejea kwao)

Baada ya mwaka mmoja,nikaenda kwa wazazi wake kuomba ridhaa ya kutambulika pia,wakanipa faini ya kumzalisha binti yao,nikatozwa kiasi fulani cha pesa,baada ya hapo ikawa rasmi pande zote mbili,japo nafsi yangu haikuwa imempenda kwa kweli!!

Mwaka 2014 mimi nilipata kazi,mkoani Tanga,yeye akapangwa Singida (yeye ni mwalimu),basi akawa ananitembelea Tanga mara kadhaa na maisha yakawa yanasonga!
Nilipoanzia kazi kuna binti mmoja alihamia akitokea mkoani Dodoma,tukawa tunasaidiana kazi pale ofisini lakini kwa kweli Moyo wangu ulimpenda yule Dada sanaaa!!(nikawa najizuia sana kuwa naye karibu ili nisijihusishe naye kimapenzi) pasipo kujua kumbe na yeye alikuwa ananipenda sana ila sikuwahi kujua!

Nikawa mwepesi sana kumzungumzia mwanamke wangu(mama mtoto wangu wa Singida) mara kwa mara namuweka profile picture kuongea naye japo ukweli sikuwa na hisia naye kabisa!!!

Kumbe yule dada mgeni alikuwa anakuwa disappointed sana kuona vile,akaomba nimsaidie kutafuta nyumba kwani hakuwa mwenyeji Tanga,nikamuunganisha na mzee mwenye nyumba yangu,akapata apartment pacha na yangu,(hapo ndipo matatizo yalipoanzia)

Tukawa watu wa karibu sana,akija mama wa mtoto wangu wanaongea pamoja na kuishi kiundugu kabisa,na baadaye akiondoka mke wangu anamsifia kuwa mke wangu ni mpole sana!

Akaanza kunisaidia kupika then tunakula wote,kwa kipindi cha kama miezi sita hivi,siku moja tukiwa tunaangalia filamu sebuleni,alionekana kuwa mnyonge sana,akanambia anaomba apumzike chumbani kwangu,nikamruhusu,ilikuwa jioni sana kama saa moja hivi,alipoingia chumbani kwangu mimi nikatoka kwenda kutafuta chakula kwa sababu hatukupika siku hiyo!nilikula huko nikarudi kama saa nne usiku,nikamkuta amelala kabisa,amevua blauzia na amevaa chupi na kanga tu!(kwa kweli nilishtuka nikajikuta kama sipo sawa hivi.

Nilimwamsha lakini hakuamka,niakaingia bafuni kuoga niliporudi alikuwa bado kitandani,nikapanda kitandani nikalala,ilipofika saa saba za usiku uvumilivu ulinishinda nikaanza kumshika maziwa,mapaja,na hatimaye tukaanza romance, na kuivunja amri ya sita!(kumbe lilikuwa kosa kubwa sanaaa)

Tukaingia kwenye mahusiano na ukawa mchezo wetu wa kila siku! Akija mama mtoto wangu ana-pretend kama hakuna kinachoendelea baina yetu,mwaka 2015 miezi ya saba nikata kuvunja mahusiano na mama wa mtoto,nilimshirikisha akaniomba aje tuzungumze juu ya maamuzi hayo,akaja mwezi wa 8/2015,alikaa mwezi mmoja,tuliongea kuhusu kuvunja uhusiano,akaongea kwa Huruma sana na mchozi mengi nikaamua kuahirisha maamuzi yangu,akaondoka!

Mwezi mmoja baadaye akaniambia anahisi ni mjamzito,(mtoto wa pili),nilisononeka sana lakini sikuwa na jinsi,ilibidi nikubaliane na uhalisia,baada ya kuondoka mke wangu tukaendelea na mchezo wetu na co-worker,mara akaanza wivu hataki niongee na mama wa mtoto wangu,nikamwambia ni bora tuachane kuliko kunipa masharti ya eti nisiongee na mpnz wangu mbele yake,na nikamwambia kuwa mchumba wangu ana mimba ya pili,hakufurahia kabisa habari hiyo akaniambia anatamani pia azae,(japo aliongea kiutani utani sana!)

Heeh,mwezi January 2016 co-worker akaniambia amenasa,khaaaa!!!!nikajaribu mbinu zangu zote kumwambia atoe,akasema hawezi kutoa kama sitaki mtoto atamlea mwenyewe,(Jamani wanaume wenzangu,usithubutu kukubali kauli hii kutoka kwa mwanamke,utajuta)

Baada ya miezi kwenda nikajikuta dilemma moja mbaya,huyu wa Tanga,nampenda sana,(sijui kama ndo limbwata au mapenzi natural,nampenda sana!) Wote wana watoto,ila wa Singida anao 2 japo simpendi sana,huyu wa Tanga ana mtoto 1 (nampenda sana,lakini kikwazo kwake ni kwamba kumbe kabla ya kuja Tanga alikuwa ameacha watoto wengine 2 huko kwao,japo hakuolewa)
Kutokana na mazingira aliyopo yule mama watoto wangu wa Singida ilibidi nimnunulie jiko la gas na baadhi ya vitu,jamaa yangu alikuwa anaenda huko nikamuomba niondoke naye kwenda Singida then nichangie mafuta!
Mama yanguuuu!huyu wa Tanga ameleta janga,maana amekuwa akinizuia nisiende Singida tangu juzi,na mimi kwa misimamo yangu nikamwambia siwezi kuacha kwenda ile ni familia yangu,akaniambia ukirudi utanikuta maiti hapa ndani kwako,nikampuuza,nimetoka kununua baadhi ya vitu narudi nyumbani nimemkuta chumbani kwangu akiwa anavuja damu nyingi,(naambatanisha picha mnisamehe wenye hisia kali kuona damu)

Amejichinja mshipa mkuu wa mkono wake wa kushoto,nimepata hofu sana kwa sababu sasa nagundua nipo na mtu hatari sana,kitendo alichofanya leo kimefanya nijutie maamuzi yangu ya mwanzo kabisa,kwanini nilikubali kukaa naye karibu na kuanza naye mahusiano!
Kitendo cha kujichinja mwenyewe si kuna siku anaweza kunivizia aniue huyu mwanamke jamaniii,nawezaje kumtoka mtu huyu katika mazingira haya,na kazini tupi pamoja kila siku!!!

Jamani ndugu zangu natamani siku zirudi nyuma nibadili mfumo wa maisha ila ndo siwezi tena,naombeni mawazo yenu ndugu zangu kwa sababu uwezo wangu wa kufikiri umekoma kabisaaa!!!
Daaa pole sana mkuu
 
The greatman ktk ubora wako, kwanza una miaka mingapi? Kifua huna pia wanawake wanakuzidi akili
Mkuu yakikufika utaelewa,lakini kwa sasa ni rahisi sana kuniona dhaifu,japo awali nilikuwa naamini haiwezi kufikia hatua kama hii,kwani niliamini huyu wa ofisini lazima atakuwa na woga wa kibinadamu kwa kujua kwamba mimi na yeye tynaiba tu,lakini kumbe sivyo hata kidogo!!!
 
Hiyo picha imenikata stimu halafu na wewe mtoa mada ni mtu wa ovyo sana ungekuwa ndugu yangu ningesikitika sana ila ingawa sikujui bado nasikitika sana akili yako ni ya kijinga mnoo kwa Maisha unayoishi na ujinga unaofanyiwa na hao wanawake wote wawili.
Mkuu mpaka kufika hatua ya kuleta Uzi hapa,ni kwamba yamenifika shingoni,kwa uzembe au ujinga wangu,inanigharimu sasa,ninachokitafuta zaidi ni namna ya kutoka hapa nilipo kurejea maisha yangu ya kawaida!

Najua nilipotoka kumdhania huyu co-worker kuwa atakuwa na hofu na kuficha mahusiano yetu,kumbe sivyo kabisa!!!
 
Bro
Brother binafsi nimejifunza kitu kutoka kwako ni bora ukawa na mtu mmoja tu tena ambaye una malengo nae hata ikitokea mimba basi najua nitakwenda kumuoa
Kabisaaa,ni hatari sana kuingia kwenye mahusiano na mtu (hasa mfanyakazi mwenzako) huku ukiwa na mahusiano mengine,itakutesa sanaaa!!!
 
Mkuu mpaka kufika hatua ya kuleta Uzi hapa,ni kwamba yamenifika shingoni,kwa uzembe au ujinga wangu,inanigharimu sasa,ninachokitafuta zaidi ni namna ya kutoka hapa nilipo kurejea maisha yangu ya kawaida!

Najua nilipotoka kumdhania huyu co-worker kuwa atakuwa na hofu na kuficha mahusiano yetu,kumbe sivyo kabisa!!!
Hapo hauna ujanja maana umeshachanganya nao damu inabidi upambane na matokeo yatakayotokea mbele yako. Umefanya kosa sana kumzalisha huyo demu wa kwanza watoto wawili bila kumuoa na huyo wa pili umeenda pekupeku tena bila kumchunguza kama alishazaa watoto huko alikotoka.

Ndio maana nashindwa kukuelewa wewe ni mtu wa aina gani mpk umefanya yote hayo bila kujua kuwa unaharibu Maisha yako. Hapo kwa lolote unalolifanya hiyo misala itasafiri na ww
 
Kabisaaa,ni hatari sana kuingia kwenye mahusiano na mtu (hasa mfanyakazi mwenzako) huku ukiwa na mahusiano mengine,itakutesa sanaaa!!!
Kweli pole,Kaka Omba Msamaa kwa Mungu na Fanya jitihada za kumtuliza huyo wa Tanga atulie,baadae Fanya njia za kuama kama inawezekana Mrudie yule wa Singida japo haumkubali na Fanya jitihada za kumshirikisha Mungu kwa Wakati huu Mgumu,mpe Mungu nafasi ataufanya Mzigo huu kuwa Mwepesi kwako,Fanya hivyo Brother hamna jambo linalomshinda Mungu na usijione Mkosaji sana Mbele za Mungu,Bali Wanadamu tuna Mapungufu sana wala mtu asikuhukumu kwa haya kuwa na Amani Moyoni na Mkabidhi Mungu hili jambo Mungu atafanya njia pasipokuwa na njia tafanya maji mahali palipo na Mwamba na kuwa mtulivu kwa sasa
 
Kweli pole,Kaka Omba Msamaa kwa Mungu na Fanya jitihada za kumtuliza huyo wa Tanga atulie,baadae Fanya njia za kuama kama inawezekana Mrudie yule wa Singida japo haumkubali na Fanya jitihada za kumshirikisha Mungu kwa Wakati huu Mgumu,mpe Mungu nafasi ataufanya Mzigo huu kuwa Mwepesi kwako,Fanya hivyo Brother hamna jambo linalomshinda Mungu na usijione Mkosaji sana Mbele za Mungu,Bali Wanadamu tuna Mapungufu sana wala mtu asikuhukumu kwa haya kuwa na Amani Moyoni na Mkabidhi Mungu hili jambo Mungu atafanya njia pasipokuwa na njia tafanya maji mahali palipo na Mwamba na kuwa mtulivu kwa sasa
Ahsante sana!!!
 
Siku utajikuta amekuua na kukuzika kimya kimya.
Ndo malipo yake lakini..
Mkeo ni mpole kwa Hiyo ukachukulia upole wake kumuumiza.
na bado kidogo tu utaumbuka
 
Siku utajikuta amekuua na kukuzika kimya kimya.
Ndo malipo yake lakini..
Mkeo ni mpole kwa Hiyo ukachukulia upole wake kumuumiza.
na bado kidogo tu utaumbuka
Wengi mnanituhumu kwa sababu nimekuwa mkweli,lakini si ajabu hata wewe umeshateleza mara nyingi tu,ila hayajakukuta,linapokuja swala la mapenzi watu tunafanya mambo ya ajabu sana,lakini kwa kuwa ni siri basi tunaziacha mioyoni mwetu,wachache tunaojitokeza na kusema yanayotusibu tunashambuliwa sana kana kwamba washambuliaji wote ni innocent kumbe na wao wana ya kwao ila hawayasemi!!
 
Back
Top Bottom