Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,114
Mwaka 2015 kulikuwa na uchaguzi Mkuu miongoni mwa mambo niliyosikia kutoka kwa baadhi ya watu ni kuwa wameuza kadi zao za kupigia kura kwa koasi cha 5000 mpaka 15000.
Mmoja wa aliyekuwa akinisimulia alidai kuwa wakipita watu mitaani wakiwashawishi wauziwe kadi za kupigia kura.
Kutokana na ugumu wa maisha wa watu walikubali na kuuza kadi hizo ambapo ilikuwa ni sawa na kuuza haki yao ya kikatiba maana hawakuweza kupiga kura.
Hata nilipojaribu kuwauliza hao watu ni kina nani hawakuwa wakiwafahamu, na wala hawakujua lengo la watu hao.
Nikawauliza tena sasa itakuwaje zoezi la kupiga kura likifika wakasema wao kupiga kura si kipaumbele kwani hata wasipopiga au wakipiga bado watashinda wale wenye makali wasiowatemea maana kura wanaona ni kupoteza muda tu.
Nikaondoka na maswali hao watu ni kina nani na wananunua kadi za kupugia kura za kazi gani, mpaka leo majibu ya maswali sijapata.
Usiuze kadi ya mpiga kira kwani ni sawa na kuuza haki yako uliyopewa na katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya kushiriki kumchagua kiongozi unayoona anastahili kukuongoza.
Ni muhimu kutambua kuwa una wajibu wa kuilinda haki yako ya kupiga kura na kuhahakisha haipotei wala kupotezwa na yeyote yule.
Mmoja wa aliyekuwa akinisimulia alidai kuwa wakipita watu mitaani wakiwashawishi wauziwe kadi za kupigia kura.
Kutokana na ugumu wa maisha wa watu walikubali na kuuza kadi hizo ambapo ilikuwa ni sawa na kuuza haki yao ya kikatiba maana hawakuweza kupiga kura.
Hata nilipojaribu kuwauliza hao watu ni kina nani hawakuwa wakiwafahamu, na wala hawakujua lengo la watu hao.
Nikawauliza tena sasa itakuwaje zoezi la kupiga kura likifika wakasema wao kupiga kura si kipaumbele kwani hata wasipopiga au wakipiga bado watashinda wale wenye makali wasiowatemea maana kura wanaona ni kupoteza muda tu.
Nikaondoka na maswali hao watu ni kina nani na wananunua kadi za kupugia kura za kazi gani, mpaka leo majibu ya maswali sijapata.
Usiuze kadi ya mpiga kira kwani ni sawa na kuuza haki yako uliyopewa na katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya kushiriki kumchagua kiongozi unayoona anastahili kukuongoza.
Ni muhimu kutambua kuwa una wajibu wa kuilinda haki yako ya kupiga kura na kuhahakisha haipotei wala kupotezwa na yeyote yule.