''Usimuone vile Kambarage ana Kibega'' Dossa Aziz

''Usimuone vile Kambarage ana Kibega'' Dossa Aziz

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,494
Reaction score
33,052
1750131889430.jpeg

Mwalimu Nyerere akisukuma gari pamoja na watu wengine

"USIMUONE VILE KAMBARAGE ANA KIBEGA"
Dossa Aziz


Picha hiyo hapo juu inanikumbusha Jumapili moja miaka mingi iliyopita tumekaa barazani nyumbani kwa Dossa Aziz Mlandizi.

Miaka mingi Dossa Aziz na Ally Sykes walikuwa hawajaonana.
Niliona jinsi Dossa alivyomlaki Ally Sykes kwa bashasha.

Dossa Aziz alikuwa anasikiliza radio asubuhi ile kama saa nne amefungua BBC World Service.

Dossa Aziz anaagiza achinjwe mbuzi.
Hakika alikuwa amefurahi kupita kiasi.

Siku hii Ally Sykes alikuwa amenipeleka nyumbani kwa Dossa nikamhoji kuhusu historia ya TANU.

Ally Sykes alikuwa na mgeni wake mwanamke Mmarekani Mweusi kutoka gazeti maarufu Washington Post.

Mbele ya nyumba yake kulikuwa na mabaki ya Land Rover.

Katikati ya mazungumzo Dossa Aziz akanyoosha kidole kuelekeza ile Land Rover akaniambia, ''Nimesafiri kwingi na Kambarage katika gari hii wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika."

Akanyamaza kidogo.
"Wakati mwingine gari inakwama njia mbovu.

Kambarage anashuka kwenye gari tunasukuma gari pamoja na watu wengine.

Usimuone vile Kambarage ana kibega."
Kibega maana yake nguvu.

1750132150872.jpeg

Dossa Aziz katika siku zake za uzeeni akiishi Mlandizi
 
Kuna mambo Dossa Aziz akikuhadithia kuhusu Julius Nyerere
utabakia mdomo wazi.

Nasikitika Mwalimu hakunyanyua kalamu kuandika historia hii.
Ugonjwa uliomsababishia kifo umempata akiwa kwenye mchakato wa kuandika historia yake.

Nakumbuka alimshirikisha Haroub toka Unguja na wengine toka Tanganyika.

Unfortunately, the project died with him.
 
Kina...
Kitabu cha Abdul Sykes kimeeleza mengi sana kuhusu Julius Nyerere ingawa hayo yangetoka kinywani mwake ingekuwa bora zaidi.
 
Nyerere angewekeza nguvu zakd zote kuijenga Tanganyika, kuachana na sera yake ya Ujamaa pekee! Na badala yake angechanganya Ujamaa na Ubepari kama walivyofanya China!

Angeachana na mchakato wake wa kuzisaidia nchi nyingine za Kiafrika kwenye kupigania uhuru! (Na kama angezisaidia basi kungekuwa na makubaliano ya kufidiana baada uhuru wa hizo nchi), Kuachana na Muungano wa kinyonyaji na Zanzibar! nk

Nina uhakika Tanganyika ingekuwa sehemu nzuri zaidi kiuchumi kuliko ilivyo sasa. Kimsingi alikuwa ni Mzalendo asiye na chembe ya shaka kwa nchi yake. Na kamwe huwezi kumlinganisha na hawa akina Chifu Mangungo wetu wa sasa.
 
Kitabu kinauzwa Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro, Manyema, Mtambani na Kichangani bei elfu kumi tu.

Mkuki na Nyota Samora Avenue pia kipo.
Hakuna uwezekano wa kununua soft copy? Maana nipo nje ya Dar
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom