Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,494
- 33,052
Mwalimu Nyerere akisukuma gari pamoja na watu wengine
"USIMUONE VILE KAMBARAGE ANA KIBEGA"
Dossa Aziz
Picha hiyo hapo juu inanikumbusha Jumapili moja miaka mingi iliyopita tumekaa barazani nyumbani kwa Dossa Aziz Mlandizi.
Miaka mingi Dossa Aziz na Ally Sykes walikuwa hawajaonana.
Niliona jinsi Dossa alivyomlaki Ally Sykes kwa bashasha.
Dossa Aziz alikuwa anasikiliza radio asubuhi ile kama saa nne amefungua BBC World Service.
Dossa Aziz anaagiza achinjwe mbuzi.
Hakika alikuwa amefurahi kupita kiasi.
Siku hii Ally Sykes alikuwa amenipeleka nyumbani kwa Dossa nikamhoji kuhusu historia ya TANU.
Ally Sykes alikuwa na mgeni wake mwanamke Mmarekani Mweusi kutoka gazeti maarufu Washington Post.
Mbele ya nyumba yake kulikuwa na mabaki ya Land Rover.
Katikati ya mazungumzo Dossa Aziz akanyoosha kidole kuelekeza ile Land Rover akaniambia, ''Nimesafiri kwingi na Kambarage katika gari hii wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika."
Akanyamaza kidogo.
"Wakati mwingine gari inakwama njia mbovu.
Kambarage anashuka kwenye gari tunasukuma gari pamoja na watu wengine.
Usimuone vile Kambarage ana kibega."
Kibega maana yake nguvu.
Dossa Aziz katika siku zake za uzeeni akiishi Mlandizi