Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Wakuu huu naweza kusema ni mtazamo wangu kwakua nimetembea mikoa tofauti hapa Tanzania. katika mkoa huu wa Arusha nimekaa kwa muda mrefu na kuishi na watu wa jiji hili haswa niseme nimebobea katikati ya jiji! Sasa basi hebu fuatilia mtiririko huu hapa chini na wewe utoe experince yako:
- Ni mkoa ghali kulingana na maisha tuliyonayo hivi sasa.
- Asilimia kubwa ya vijana hawana kazi. (Utakuta vijana wengi wakowako tu).
- Kila mtu anajifanya ni dalali (chunga sana unaweza ukauziwa kiwanja hata cha kanisa).
- Wanaume ni wambea sana kuliko wanawake.
- Mtu akishakua na hela basi hatakosa wapambe wa kumpamba mpaka saa unakwenda kulala.
- Mtu akishakua na hela basi majina kama FOGO/KIFARU/MELI ndio majina utakayopewa.
- Mtu ukishakua na hela ya kunywa bia zaidi ya tano kaunta basi wewe ni FOGO/KIFARU/MELI. hata kama unakopa.
- Kutokana na ukosefu wa ajira vijana wengi wameingiwa na tabia ya kuamka asubuhi na mapema baa au Grosery na kuzimua maarufu kama KUTOA LOCK!
- Sio rahisi ukaamka asubuhi mapema katika ya jiji ukakuta maduka yako wazi sana sana ni kuanzia saa 3 asubuhi nakuendelea.
- Watu wa hapa hawana haraka sana yaani kwenda na muda, sana sana ukijifanya unaharaka utaambiwa si ungekuja jana au utaambiwa una kiherehere.
- Ukisikia mtu alikua Mirerani akaja na kijiwe chake akauza hata 100'000 moja halafu akaiingia baa na akasokota raundi mbili basi wewe sema lile jiwe uliuza shilingi 1000'000'000 wapambe watakupamba sana na hata wanawake hawatakaa mbali na wewe pamoja na madalali wa viwanja na magari.