Usililolijua Tabia za Watu Mkoa wa Arusha Soma Hapa

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Wakuu huu naweza kusema ni mtazamo wangu kwakua nimetembea mikoa tofauti hapa Tanzania. katika mkoa huu wa Arusha nimekaa kwa muda mrefu na kuishi na watu wa jiji hili haswa niseme nimebobea katikati ya jiji! Sasa basi hebu fuatilia mtiririko huu hapa chini na wewe utoe experince yako:
  1. Ni mkoa ghali kulingana na maisha tuliyonayo hivi sasa.
  2. Asilimia kubwa ya vijana hawana kazi. (Utakuta vijana wengi wakowako tu).
  3. Kila mtu anajifanya ni dalali (chunga sana unaweza ukauziwa kiwanja hata cha kanisa).
  4. Wanaume ni wambea sana kuliko wanawake.
  5. Mtu akishakua na hela basi hatakosa wapambe wa kumpamba mpaka saa unakwenda kulala.
  6. Mtu akishakua na hela basi majina kama FOGO/KIFARU/MELI ndio majina utakayopewa.
  7. Mtu ukishakua na hela ya kunywa bia zaidi ya tano kaunta basi wewe ni FOGO/KIFARU/MELI. hata kama unakopa.
  8. Kutokana na ukosefu wa ajira vijana wengi wameingiwa na tabia ya kuamka asubuhi na mapema baa au Grosery na kuzimua maarufu kama KUTOA LOCK!
  9. Sio rahisi ukaamka asubuhi mapema katika ya jiji ukakuta maduka yako wazi sana sana ni kuanzia saa 3 asubuhi nakuendelea.
  10. Watu wa hapa hawana haraka sana yaani kwenda na muda, sana sana ukijifanya unaharaka utaambiwa si ungekuja jana au utaambiwa una kiherehere.
  11. Ukisikia mtu alikua Mirerani akaja na kijiwe chake akauza hata 100'000 moja halafu akaiingia baa na akasokota raundi mbili basi wewe sema lile jiwe uliuza shilingi 1000'000'000 wapambe watakupamba sana na hata wanawake hawatakaa mbali na wewe pamoja na madalali wa viwanja na magari.
Jamani kama kuna nililosahau naomba muongeze kwakua naamini hapa JF kuna wakazi wengi wa Arusha. Nawasilisha.
 
Sidhani kama utafiti wako umeufanya kwa makini
Issue ya mtu kuuza mawe na kujifanya ana pesa na kuzungusha round ilikuwa miaka hiyo ya 1990 kwa sasa hakuna limbukeni wa mambo hayo
Vijana wa arusha ni wapambanaji na wanatafuta maisha na wala sio watu wa kuringia kuzungusha round bar wala kuringia bia
Vijana wengi labda ulikutana nao ni wauza madini ambao kazi zao zinahitaji kukaa sehem ambako ni mitaa yao ya biashara na sio kwamba hawana kazi za kufanya
Siwatetei ila ukweli vijana wa arusha ni wahangaikaji mno na wanapambana sana kuyaweka maisha yao kwenye mstari
Ughali wa maisha wa mji wowote unategemea na upatikanaji wa pesa na sidhani kama utafiti huo umeulinganisha na miji mingine ya wapi
Na hapa jua kwamba kuna watu wa UN wako wengi sana hapa mjini na kulingana na hali kama hiyo ni lazima mzunguko wa pesa ni mkubwa na kuwepo kwao ambapo watu kama wale wanapokea mishahara na marupurupu makubwa ni lazima yafanye mji kuwa ghali

Ni mawazo yangu hayo mkuu maana na mimi ni mkaazi wa arusha sana na ni muda mrefu sana
 
asante Mr.rocky
hiyo Na 4 labda unaokuwa nao wewe

Asante sana Black Woman
Anachoongea sijui ni cha kusikia kijiweni
Maana wanaume wa Arusha wanapambana na maisha yao licha ya mji kuwa ghali bado wanamudu kuishi na familia zao
Wanamudu hata kupata za kunywa na kuzimua asubuhi
Maana kama wangekuwa wanakaa vijiweni tuu ni muda upi wangepata hata hizo za kuzimua asubuhi
Na sidhani kama kuna wanaume wa aina ya no 4 uliyoandika hapo may be sample zako zilikuwa kwa marafiki zako wawili watatu ulio nao
Na kama mtu ana pesa zake mwache aitwe majina anayotaka na hata akiitwa meli kama ana pesa zake kuna shida gani
Na ya nini kufuatilia life za watu na kufanya uchunguzi kuwa wanakunywa asubuhi na mapema au wanapongezana bar au kuna mtu ameuza jiwe lake la mererani na anazungusha round bar
huo muda uliupata wapi
 
wanapenda kuvaa jeans, hawana adabu na pesa ,na ukibeba bahasha unaonekana msomi.

Mambo mengine hata sio ya kusema
Kwani kuvaa jeans nako kuna mkoa
maana mtu anavaa kulingana na nature ya kazi yake
Kama anauza duka la spare au la vifaa vya umeme ulitegemea avae suti
Au anafanya kazi godown ulitegemea aulambe mkanda nje
Duh sasa hii ni ushabiki wa ajabu
 
Asante sana Black Woman
Anachoongea sijui ni cha kusikia kijiweni
Maana wanaume wa Arusha wanapambana na maisha yao licha ya mji kuwa ghali bado wanamudu kuishi na familia zao
Wanamudu hata kupata za kunywa na kuzimua asubuhi
Maana kama wangekuwa wanakaa vijiweni tuu ni muda upi wangepata hata hizo za kuzimua asubuhi
Na sidhani kama kuna wanaume wa aina ya no 4 uliyoandika hapo may be sample zako zilikuwa kwa marafiki zako wawili watatu ulio nao
Na kama mtu ana pesa zake mwache aitwe majina anayotaka na hata akiitwa meli kama ana pesa zake kuna shida gani
Na ya nini kufuatilia life za watu na kufanya uchunguzi kuwa wanakunywa asubuhi na mapema au wanapongezana bar au kuna mtu ameuza jiwe lake la mererani na anazungusha round bar
huo muda uliupata wapi

alikuwa anatafuta kupata idadi ya wambeya

nipo huu mkoa miaka mia nane
hayo mambo ya mererani ilikuwa zamani enzi za titus
leo wakipata jiwe wala huwezi jua ki vile kimya kimya
kwa mambo yao kama ni pombe ni za kawaida
kama wanywaji wengine
kuhusu ugumu wa maisha mie naona kawaida
ishi kuendana na kipato chako
 
Mr. Rocky labda unaishi bwawa la Ma****i kule maeneo ya relini njoo huku maeneo ya Clock Tower uone wanaume wenye ndevu lakini hata ukishindia maji na pilipili wanajua!
 
Asante sana Black Woman
Anachoongea sijui ni cha kusikia kijiweni
Maana wanaume wa Arusha wanapambana na maisha yao licha ya mji kuwa ghali bado wanamudu kuishi na familia zao
Wanamudu hata kupata za kunywa na kuzimua asubuhi
Maana kama wangekuwa wanakaa vijiweni tuu ni muda upi wangepata hata hizo za kuzimua asubuhi
Na sidhani kama kuna wanaume wa aina ya no 4 uliyoandika hapo may be sample zako zilikuwa kwa marafiki zako wawili watatu ulio nao
Na kama mtu ana pesa zake mwache aitwe majina anayotaka na hata akiitwa meli kama ana pesa zake kuna shida gani
Na ya nini kufuatilia life za watu na kufanya uchunguzi kuwa wanakunywa asubuhi na mapema au wanapongezana bar au kuna mtu ameuza jiwe lake la mererani na anazungusha round bar
huo muda uliupata wapi

Mr.Rocky wanazimua na viroba vya shilingi 500! Tembea uone wewe!
 
Mr. Rocky labda unaishi bwawa la Ma****i kule maeneo ya relini njoo huku maeneo ya Clock Tower uone wanaume wenye ndevu lakini hata ukishindia maji na pilipili wanajua!

haijalishi ninanokaa wala nini ila utafiti wako kaurudie tena
Hao unaokutana nao ni wale wale wa kila siku ambao hawana deal la maisha
Niko huu mkoa mwaka wa Kumi na moja huu haya mambo sijawahi yaona
Enzi za kuringia na kuzungusha round bar eti umepata jiwe la mererani likuwa miaka ya 90 huko sio sasa
Watu wameelimika na wanajua maisha ni nini
 
Mr.Rocky wanazimua na viroba vya shilingi 500! Tembea uone wewe!

Kama huna kazi hiyo mia tano ya kuzimua kila siku unaipata wapi
Na kodi ya nyumba unayokaa nani anakulipia
na maisha yako unaendeshaji kama hujiwezi
 
alikuwa anatafuta kupata idadi ya wambeya

nipo huu mkoa miaka mia nane
hayo mambo ya mererani ilikuwa zamani enzi za titus
leo wakipata jiwe wala huwezi jua ki vile kimya kimya
kwa mambo yao kama ni pombe ni za kawaida
kama wanywaji wengine
kuhusu ugumu wa maisha mie naona kawaida
ishi kuendana na kipato chako


Black Woman nakubaliana na wewe
Hizi ni story ambazo watu wanasimuliana huko vijiweni na hazina mshiko wowote
 
Unaweza kutujuza umekaa wapi tena zidi ya Arachuga??mimi nipo mwanza maisha ni rahisi ukilinganisha na Arachuga,watu kiuchumi huku wapo hohehahe kwaukweli hata ukimkuta mwenye afadhali pia anafanana tu na ambae hana kwani kujiweka smart inaonekana ni mzozo,ukiwaza maisha Arachuga basi hakuna utakaposhindwa kuishi kwani hata mnaisha ya dar hayalingani na Arusha ,nimeishi mikoa ambayo ukienda kula hotelini unaonekana kama mgeni sehemu hizo,kimavazi ukichomekea unaonekana kama unaenda kanisani jumapili au hospitali au unasafiri.arusha chumba chakupanga ni alfu hamsini bei ya chini,na hakuna chai ya mia tatu ni mia tano kwenda juu,tofauti na huku zoo mpaka sasahivi buku jero kifungua kinywa umemalizi kilakitu supu mpaka chai.jipange kuishi Arusha ndugu.
 
Sidhani kama utafiti wako umeufanya kwa makini
Issue ya mtu kuuza mawe na kujifanya ana pesa na kuzungusha round ilikuwa miaka hiyo ya 1990 kwa sasa hakuna limbukeni wa mambo hayo
Vijana wa arusha ni wapambanaji na wanatafuta maisha na wala sio watu wa kuringia kuzungusha round bar wala kuringia bia
Vijana wengi labda ulikutana nao ni wauza madini ambao kazi zao zinahitaji kukaa sehem ambako ni mitaa yao ya biashara na sio kwamba hawana kazi za kufanya
Siwatetei ila ukweli vijana wa arusha ni wahangaikaji mno na wanapambana sana kuyaweka maisha yao kwenye mstari
Ughali wa maisha wa mji wowote unategemea na upatikanaji wa pesa na sidhani kama utafiti huo umeulinganisha na miji mingine ya wapi
Na hapa jua kwamba kuna watu wa UN wako wengi sana hapa mjini na kulingana na hali kama hiyo ni lazima mzunguko wa pesa ni mkubwa na kuwepo kwao ambapo watu kama wale wanapokea mishahara na marupurupu makubwa ni lazima yafanye mji kuwa ghali

Ni mawazo yangu hayo mkuu maana na mimi ni mkaazi wa arusha sana na ni muda mrefu sana

Mkuu kumbuka UN asilimia kubwa wameondoka mbona bado maisha ni ghali? Kinachofanya mji kuwa ghali ni madalali, huu mji ni wa kitalii si kama Dar, Dar ni mji wa kibiashara sasa mji wa Arusha unapokea wageni wengi kutoka sehemu mbalmbali wageni wanakutana na madalali ili kurahisisha mambo yao...mfano kuna wenye nyumba ukitaka nyumba kwake lazima upelekwe na dalali ndo hapo unakuta mzawa una compite na mgeni halafu ndo unambiwa mambo ya kulipa kwa dola, sasa mzawa utapata wapi dola labda uwe unafanya tourcompany sasa ukipiga hesabu kila kitu kimedhaminishwa kwa dola na si shilingi hata nguo madukani utasikia hii nilinunua dola ....kwa tsh ni... siunaona rate mwenyewe.

Kwa kifupi Utaliii ,United nations, EAC, Madini na Madalali ndo vimefanya mji umekuwa juu kama dola.
 
huyu jamaa analysis yake ni narrow maana watu wa arusha ni watafutaji sana na ukitaka kujua hilo amuka saa kumi na moja asubuhi uone wamama wanavyocharika yaani watu hawasalimiani hiyo asubuhi utazani china! kwa ujumla watu wa arusha ni watafutaji na mchana wanatafuta jioni/weekend ndio wanazitumia!
 
duh .... hii thread ngumi zitarushwa, ngoja tumsubiri PJ atoe verdict
 
Mkuu kumbuka UN asilimia kubwa wameondoka mbona bado maisha ni ghali? Kinachofanya mji kuwa ghali ni madalali, huu mji ni wa kitalii si kama Dar, Dar ni mji wa kibiashara sasa mji wa Arusha unapokea wageni wengi kutoka sehemu mbalmbali wageni wanakutana na madalali ili kurahisisha mambo yao...mfano kuna wenye nyumba ukitaka nyumba kwake lazima upelekwe na dalali ndo hapo unakuta mzawa una compite na mgeni halafu ndo unambiwa mambo ya kulipa kwa dola, sasa mzawa utapata wapi dola labda uwe unafanya tourcompany sasa ukipiga hesabu kila kitu kimedhaminishwa kwa dola na si shilingi hata nguo madukani utasikia hii nilinunua dola ....kwa tsh ni... siunaona rate mwenyewe.

Kwa kifupi Utaliii ,United nations, EAC, Madini na Madalali ndo vimefanya mji umekuwa juu kama dola.

nakubaliana na wewe mkuu na ndo maana nilimpa mfano mmoja tuu wa UN maana bado kuna EAC bado huu ni mji wa kitalii ambao kila kukicha kuna wageni kibao wanaingia na kutoka bado kuna mashirika kibao ya kimataifa yapo hapa
Sasa madai yake kuwa mji huu wanaume ni wambeya au wanaamkia bar kupata za kuzimua sidhani kama ni kweli
 
Unaweza kutujuza umekaa wapi tena zidi ya Arachuga??mimi nipo mwanza maisha ni rahisi ukilinganisha na Arachuga,watu kiuchumi huku wapo hohehahe kwaukweli hata ukimkuta mwenye afadhali pia anafanana tu na ambae hana kwani kujiweka smart inaonekana ni mzozo,ukiwaza maisha Arachuga basi hakuna utakaposhindwa kuishi kwani hata mnaisha ya dar hayalingani na Arusha ,nimeishi mikoa ambayo ukienda kula hotelini unaonekana kama mgeni sehemu hizo,kimavazi ukichomekea unaonekana kama unaenda kanisani jumapili au hospitali au unasafiri.arusha chumba chakupanga ni alfu hamsini bei ya chini,na hakuna chai ya mia tatu ni mia tano kwenda juu,tofauti na huku zoo mpaka sasahivi buku jero kifungua kinywa umemalizi kilakitu supu mpaka chai.jipange kuishi Arusha ndugu.

Mkuu nenda stendi ndogo vijana wangapi wanapiga debe ili tu wapate mia wakusanye siku nzima atakuwa na shilingi ngapi bado hajala ndom mana wanatoa lock kwa mia tano mana kwa hali ilivyo ngumu mtu anaona bora atoe wenge apate nguvu na ujasiri wa kupambana bila hivyo siku haiendi.
Huwezi linganisha maisha ya Arusha na Mbeya au kwingineko, vyakula bei juu, nyumba ndo usiseme Viwanja hatuongei.
 
Back
Top Bottom