MPIGA ZEZE
JF-Expert Member
- May 16, 2011
- 2,539
- 2,297
"matusi ya nyerere yanayoishi leo
By Makame
Sijaelewa hapo. Nyerere alimtusi mtu/watu au yeye ndiye alietusiwa? It should be remembered that the late Nyerere was not God. Ingawa kuna mikakati ya kumfanya Saint ili iwe kila alichofanya na alichosema ni kitakatifu. Siasa zina mizengwe sana.
Nyerere
(1) Fought for African Liberalization
(2) Ameleta Muungano
(3) Ameondosha ukabila
Pia
(1) amepigana vita Uganda kwa kutaka amrudishe swahiba wake Obote madarakani
(2) Ameleta azimio la Arusha na operation vijiji - vyote vilifeli
(3) Alisababisha mgao wa sukari na unga, sabuni ilikuwa hakuna, maduka hayana bidhaa.
(4) Ilikuwa hakuna uhuru wa kuongea, vyombo vya habari na uwekezaji.
TUMETOKA MBALI. Uzuri wa binadamu, hawakawii kusahau"
Ndugu Makame mimi nigusie tu (3) na (4). JKN alikuwa mpambanaji. Aliingia katika mvutano na IMF (wakala wa International capitalism for better or for worse, it depends unanufaika vipi na mfumo huu) kwa kutaa masharti yao ambayo kwa maoni yake (yawezekana alikuwa sahahi au hakuwa sahihi - lakini nia ilikuwa ni sahihi) aliona ni kuwaumiza wananchi ambao alikuwa akiwaongoza! IMF nayo ikaamua kutuadhibu na ndiyo hali ya joto tuliyoonja. IMF ikashinda na JKN akajiondokea kiungwana (akang'atuka). Alikuwa muungwana vinginevyo angeng'ang'ania kama Mugabe. Aliona upepo wa mabadiliko ya kidunia (utandawazi) ulivyokuwa unavuma kwa kasi. Ni upepo huo huo ambao unahusiana na hiyo hoja yako namba 4. Kwa hivyo basi ukitaka kufanya uchambuzi makini wa kisiasa ni muhimu ukazingatia suala la wakati (enzi). Ni kweli enzi za JKN hatukuwa na uhuru wa vyombo vya habari kama ilivyo leo (na pengine dunia yote ilikuwa hivyo) lakini tulikuwa na uhakika wa umeme (alitengeneza mitambo yote ya mtera na kidatu na ilitosha mahitaji ya wakati huo). Leo hii tuna uhuru mkubwa wa vyombo vya habari na UWEKEZAJI lakini tuko gizani (hata kile kidogo alichoanzisha nacho kimetoweka). Badala ya kumlaumu JKN mimi ninafikiri tungejiliza kwa nini tumeshindwa kujenga kuta kwenye ile misingi mizuri ya huduma za kijamii aliyojenga? Na ni mingi ndugu yangu hatuwezai kumaliza nafasi ya thread hii kuiorodhesha yote inagusa nyanja zote muhimu ikiwa ni pamoja na elimu na miundombinu. Kikubwa zingatia nyakati katika kuchambua masuala ya kisiasa.
Sijaelewa hapo. Nyerere alimtusi mtu/watu au yeye ndiye alietusiwa? It should be remembered that the late Nyerere was not God. Ingawa kuna mikakati ya kumfanya Saint ili iwe kila alichofanya na alichosema ni kitakatifu. Siasa zina mizengwe sana.
Nyerere
(1) Fought for African Liberalization
(2) Ameleta Muungano
(3) Ameondosha ukabila
Pia
(1) amepigana vita Uganda kwa kutaka amrudishe swahiba wake Obote madarakani
(2) Ameleta azimio la Arusha na operation vijiji - vyote vilifeli
(3) Alisababisha mgao wa sukari na unga, sabuni ilikuwa hakuna, maduka hayana bidhaa.
(4) Ilikuwa hakuna uhuru wa kuongea, vyombo vya habari na uwekezaji.
TUMETOKA MBALI. Uzuri wa binadamu, hawakawii kusahau"
Ndugu Makame mimi nigusie tu (3) na (4). JKN alikuwa mpambanaji. Aliingia katika mvutano na IMF (wakala wa International capitalism for better or for worse, it depends unanufaika vipi na mfumo huu) kwa kutaa masharti yao ambayo kwa maoni yake (yawezekana alikuwa sahahi au hakuwa sahihi - lakini nia ilikuwa ni sahihi) aliona ni kuwaumiza wananchi ambao alikuwa akiwaongoza! IMF nayo ikaamua kutuadhibu na ndiyo hali ya joto tuliyoonja. IMF ikashinda na JKN akajiondokea kiungwana (akang'atuka). Alikuwa muungwana vinginevyo angeng'ang'ania kama Mugabe. Aliona upepo wa mabadiliko ya kidunia (utandawazi) ulivyokuwa unavuma kwa kasi. Ni upepo huo huo ambao unahusiana na hiyo hoja yako namba 4. Kwa hivyo basi ukitaka kufanya uchambuzi makini wa kisiasa ni muhimu ukazingatia suala la wakati (enzi). Ni kweli enzi za JKN hatukuwa na uhuru wa vyombo vya habari kama ilivyo leo (na pengine dunia yote ilikuwa hivyo) lakini tulikuwa na uhakika wa umeme (alitengeneza mitambo yote ya mtera na kidatu na ilitosha mahitaji ya wakati huo). Leo hii tuna uhuru mkubwa wa vyombo vya habari na UWEKEZAJI lakini tuko gizani (hata kile kidogo alichoanzisha nacho kimetoweka). Badala ya kumlaumu JKN mimi ninafikiri tungejiliza kwa nini tumeshindwa kujenga kuta kwenye ile misingi mizuri ya huduma za kijamii aliyojenga? Na ni mingi ndugu yangu hatuwezai kumaliza nafasi ya thread hii kuiorodhesha yote inagusa nyanja zote muhimu ikiwa ni pamoja na elimu na miundombinu. Kikubwa zingatia nyakati katika kuchambua masuala ya kisiasa.