USHUHUDA: Nilizaliwa na Virusi vya UKIMWI

USHUHUDA: Nilizaliwa na Virusi vya UKIMWI

Kwa hiyo mkuu katika kipindi chote hicho unatumia nini mpaka umeweza kukaa miaka yote hiyo mkuu.

Ni arv au nifafanulie kiongozi.

Hongera sana.
Usijali mkuu,sikuwahi kutumia Arv miaka ya nyuma,Arv nimeanza kutumia mwaka jana tena baada ya kulazimishwa sana na Daktari wangu ambaye ni rafiki yangu so kuanzia mwaka jana mwezi wa tisa ndio nimeanza kutumia ARV
 
Dogo, YOU ARE ONE IN A MILLION. Hongera sana. Nimependa maamuzi yako na msimamo wako wa kijasiri na kishujaa sana.

Pole kwa kumpoteza mama ukiwa mdogo sana, ila usimlaumu kwa sababu hujui nae ilikuwaje mpk akaupata. Muombee sana huko aliko. TO ERR IS HUMAN...!!
 
Mara ya kwanza kupima 2007, nikapima 2009, halafu nikapima 2015.

Nyakati zote nilikua uncomfortable kusubiri majibu. Ile moment haizoeleki.

Mleta uzi nakupa hongera kwa attitude yako, samahani sikupi pole unastahili pongezi
Kwa nn umepima kwa kupishana miaka hivyo?
 
Usijali mkuu,sikuwahi kutumia Arv miaka ya nyuma,Arv nimeanza kutumia mwaka jana tena baada ya kulazimishwa sana na Daktari wangu ambaye ni rafiki yangu so kuanzia mwaka jana mwezi wa tisa ndio nimeanza kutumia ARV

Ooh okay.

Naskia ukianza kumeza hutakiwi kuacha au ni maneno ya watu tu...?

Na umeona tofauti gani kabla ya kuanza kumeza na baada ya kumeza kuna utofauti wowote katika mwili wako mkuu...?

Hongera.
 
Ooh okay.

Naskia ukianza kumeza hutakiwi kuacha au ni maneno ya watu tu...?

Na umeona tofauti gani kabla ya kuanza kumeza na baada ya kumeza kuna utofauti wowote katika mwili wako mkuu...?

Hongera.
Ahsante,Tofauti ipo kwanza ukitumia ARV sometimes unachoka kabisa kama hujala,kuhusu kuacha Arv,kuna kipindi nilienda vijijini na akiba ya dawa iliisha na huko hakukuwa na hospitali wala zahanati hivyo nilikaa wiki tatu bila kutumia Arv, sikupata madhara ila ukianza kutumia sio vizuri kuacha kwani kuna madhara utayapata ,kikubwa ni kuzingatia mlo kamili na dawa,
 
Hongera Rafiki. Bora ww ulipata bila ya Zinaa ukimwomba MUNGU kwa Amani na kuamini unaweza pona kabisa tofauti na sie wengine tunaosumbuliwa na Uzinzi maana hata tukipata unajiuliza MUNGU utamuanza anza je kumueleza Shida yako. Pole sana Rafiki.na Hongera sana kwa uwazi wako. MUNGU akupe maisha marefu. Ukimwi sio kufa wanakufa wazima wagonjwa wanadunda. Kikubwa tuombeane majaribu ni Mengi
 
Kwa nn umepima kwa kupishana miaka hivyo?
Nilikua sipangi kwenda kupima, yaani ilikua labda natembea sehemu nikikuta wanafanya hiyo kitu ndiyo napima.

Mfano hapo kuna kile kipindi ch Tanzania Bila Ukimwi inawezekana, Kuna sherehe za Saba Saba Dar es Salaam, na Nane Nane Mbeya
 
Hongera Rafiki. Bora ww ulipata bila ya Zinaa ukimwomba MUNGU kwa Amani na kuamini unaweza pona kabisa tofauti na sie wengine tunaosumbuliwa na Uzinzi maana hata tukipata unajiuliza MUNGU utamuanza anza je kumueleza Shida yako. Pole sana Rafiki.na Hongera sana kwa uwazi wako. MUNGU akupe maisha marefu. Ukimwi sio kufa wanakufa wazima wagonjwa wanadunda. Kikubwa tuombeane majaribu ni Mengi
Ameeeen kaka,ubarikiwe sana kuwa na ukimwi sio mwisho wa maisha
 
Back
Top Bottom