batmanwafez
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 882
- 1,363
Kiukweli Tz haki hakuna kabisaaa...saa hiv ni kuanza kutembea na pesa feki tu...wakikumata na wew unawashikisha hizo noti feki wakafe nazo huko
Ulikuwa na kosa gani?kuna askari mmoja bonge pale Ostabay nikiwa abiria wa boda alitukamata pale karibu na ulipo ubalozi wa Urusi ,Boda akachukuwa hela mimi akanilaza mahabusu mpaka kesho yake na ulikuwa mwezi wa ramadhani na alikuwa analalamika swaumu kali na akadai rushwa !! ndo nitoke na nilimpa 50 elfuMungu amchomee na moto wa jahanam milele
Hiyo ndiyo Cicem bro... achana na hiyo kitu utabaki maskini,kila siku utachotea maji kwenye gunia.SEHEMU YA KWANZA.
Mimi nafanya shughuli zangu city centre.. Natumia usafiri wa pikipiki kuendesha shughuli zangu mjini ili kufika sehemu kwa wakati.
Kuna order iliwahi kutolewa na mkuu wa Mkoa Mh Paul Makonda kutoingia mjini bila kibali. Ili kutii agizo hilo huwa nakata kibali kila baada ya miezi 6 ili niweze kuendelea na shughuli zangu bila bughudha.
Picha linaanza mwezi september kwa kukamatwa nikiwa nimesimama kwenye mataa ya mnazi mmoja nikisubiri taa ziruhusu magari ,mara paap nadandiwa na mtu aliyevalia kiraia na kuchomoa ufunguo ghfla. Namuuliza kulikoni? Najibiwa leta pikipiki pembeni. Baada ya kusogea pembeni naambia achia pikipiki nauliza kwa nini? Naulizwa una bei gani nikuachie?
Duuu nikajua tapeli huyu,nikamjibu nikupe pesa kwa kosa gani? Nikaambiwa sina Leseni, nikaonesha leseni. Baada ya dakika kadhaa za mabishano anaingia mwingine ananiamuru niachie pikipiki, tukaanza kuvutana wakanizidi nguvu. Pikipiki ikachukuliwa nikaambiwa nikae nyuma. Kweli, kumbe ni askari akanipeleka hadi central , kufika tu yule aliyenikamata akasema "afandeeee huyu kosa lake mwendo kasiiii" shabashiiiii nataka kuongea nikambiwa kaa kimya unajifanya jeuri, kaa chini nyosha miguuu, duuuu nikatii sheria bila shuruti. Walikuepowengine wengiwaliokaa chini wanachukuliwa maelezo.
Baada ya muda zamu yangu ikafika nikaanza kuhojiwa. Nikaulizwa kosa nikasema sina kosa. Askari akaniambia usinipotezee muda mimi sijakukamata. Akaniambia chagua kosa niandike Mwendokasi au wrong parking, duuuh nimebisha pale mwisho a picha nikaandikiwa Wrong parking.
Baadae tukapekuliwatuakawekwa ndani wote. Tulikuwa kama 20. Tukiwa ndani tukawa tunabadilishana mawazo na madereva wenzangu. Wengi ni Bodaboda. Nikaambiwa hapa kesho asubuhi unatakiwa uandae wadhamini 2waje na barua za serikali za mitaa. Kweli kesho yake akaanza kutoka mmoja baada ya mwingine. Zamu yangu ilipofika nilidhaminiwa na mtu mmoja. Nikaachiwa kama saa 6 mchana. Nikaambiwa kesho saa 4(siku iliyofuata) nije na LESENI, KADI YA PIKIPIKI, BIMA, SUMATRANA RISITI.
Kesho nikaenda navyo vyote. Tumekaa pale asubuhi hadi mchana hakuna kinachoendelea ila naona wenzangu(wazoefu wa kukamatwa mjini) wanachukua pikipiki wanaondoka. Ikabidi na mimi nijiongeze nikamuuliza aliyetoka na pikipiki,utaratibu wa pikipiki ukoje?mbona nimeshakaguliwa lakini sioni nikiachiwa? Akaniambia Bro hapa huwa hawataki maneno wanataka pesa au uende mahakamani ukajitetee? Duuhh kusikia mahakamani nikapagawa.
Nikamuuliza wanataka kiasi gani? Nikaambiwa laki na nusu (150,000/=). Baada ya kukaa muda ikabidi na mimi niende ofisini pale kwa Afande Beka kwenye ofisi ya karibu na mwembe ili nilipe 150,000/=. sikkufanikiwa kumuona afande Beka. Nikapewa namba nimpigie askari anisaidie kuitoa pikipiki. Akaniambia bila laki na nusu pikipiki huitoi, nikamwambia laki na nusu ninayo. Akaniambia nisubiri baada ya nusu saa kwa sababu yupo mbali.
Baada ya nusu saa akanipigia simu nipeleke pesa. Nikaenda nikampa keshi 150000. Nikapelekwa kwa Afande Beka nikaaandikiwa kimemo, pikipiki nikapewa. SIUKUPEWA RISITI. NILIPOULIZA RISITI NIKAULIZWA KWANI PIKIPIKI YAKO HUJAPATA? NIKAISHIWA POZI IKABIDI NIWE MPOLE.
SEHEMU YA PILI.
Mwezi November. Picha linaanzia mataa ya kamata. Nikiwa nimesimama ktk mataa mara paap funguo zimechomlewa. Kama kawaida. Tukaenda kuwekwa kwenye karandinga karibu na roundabaout ya kuelekea sentro na mbagala. Ilipofika jioni aliletwa jamaa mmoja anashushiwa kipigo cha hatari. Alishushia sitiki za kufamtu. Kumbe yule jamaaalikua mwanajeshi ila yeye alikuwa abiria alivyoona wamerukia ufungua wa bodaboda aliyekuwa amemubeba alihisi kutaka kusababishiwa ajari, ikabidi awape adabu kidogo asikari duuh baada ya hapo walikusanyika kama wote walimshushia kipigo cha mbwa mwizi pamoja na kuwaonesha kitambulisho kama afisa wa jeshi hawakumuelewa, walimpa kipigo hadi akawa anatoa chozi kwa uchungu. Siku hiyo kama kawaida tukapelekwa central, usiku huo zilipigwa simu nyingi sana zikilenga kusaidia huyo mjeshi bila mafanikio. Siku hiyo tulikaa pale tukachuliwa maelezo hadi usiku wa saa 6. Baadae tulipelekwa mahabusu wote ,tukapekuliwa tukaingizwa chini lakini yule mjeshi alibaki kaunta tulikuja ambiwa kesho yake kuwa aliachiwa.
Kama kawaida utaratibu wa kutoka ulikuwa uleule. Nililipa 150,000/=BILA RISITI, BILA KUANDIKIWA MAKOSA MATANO ILI IENDANE NA PESA ILIYOLIPWA YA MAKOSA 5, ILA SIKU HIYO NILIANDIKIWA KOSA LA KUPITA MWENDO KASI WAKATI NIMEKAMATIWA MATAA YA KAMATA NIKIWA NATOKA POSTA.
SEHEMU YA TATU.
Baada ya pale baadhi ya madereva bodaboda walivyoona nakamatwa kizembe walinishauri nisiwe nasimama kwenye mataa. Wao huwa hawasimami kwe mataa kwa kuogopa kudandiwa na askari bila sababu za msingi. Nikaona hii imekaa poa sana. Na mimi sasa nikawa siheshimu mataa, nikiona upenyo tu napenya. Laikini hili halijanisaidia kwa sababu sasa hivi hawa askari wamejaa kila mtaa. Naambiwa wanatumia shirikishi na baadhi ya madereva bodaboda kukamata wenzao. Unaweza ukawa unatembea mara ghafla inabinywa clutch. Kwa style hii ya hovyo nimekamatwa mara 2 na mara zote hizi nilianguka chini kwa sababu ya kung'ang'aniwa clutch.
Kuna mbinu nyingine wanakublock na bajaji au na pikipiki kiasi kwamba wanaweza kukusababishia ajari. Hii mbinu nadhani imeanza baada ya kuona hatusimami tena kwenye mataa.
Picha linaanzia february. Nimekamatwa mara 5 toka february hadi jana. Kama kawaida mkamataji anaweza kukuliza kwanza una bei gani, mkimalizana anakuachia. Mara nyingi ukiwa na elfu 50, 30, 20 ya papo kwa papo unaachiwa. Kama huna pesa ya papo kwa papo ndo unafikishwa kwa pilato. Kwa afande Beka.
Angalau sasa hivi wamepunguza bei. Pale sasa hivi unaambiwa lipia makosa mawili yaani 60,000/=. Bila hiyo pesa huachiwi na chombo kinabaki polisi. NAWAONEA HURUMA BODABODA WANAOCHUKULIWA PESA ZAO BILA HURUMA KUWA WENGINE WANAENDESHA FAMILIA ZAO KWA KAZI YA BODABODA. Bodaboda na waendesha pikipiki wengine hapo mjini huo ndo mtindo wa kisasa. HII ADHA MADEREVA PIKIPIKI TUNAIPATA KWA SABABU YA TAMKO LA MH MKUU WA MKOA PAUL MAKONDA.Unaweza kuwa na Kila kitu lakini ukifika pale unapigwa biti na maasikari pale utadhani umeua. Hupewi pikipiki ukaendelee na shughuli bila kulipia faini. Husikilizwi hata kidogo. Hii ni tofauti na gari unaandikiwa bill hata kama huna pesa kwa wakati huo unalipia baadae. HII HALI YA VITISHO, KUWEKWA NDANI , NA KULAZIMISHWA KULIPIA FAINI YA PAPO KWA PAPO NDO INAONGEZA RUSHWA NA HATUPEWI RISITI. PESA ZOTE ZINAISHIA PALE KWA AFANDE BAKARI BADALA YA KULIPA KWA CONTROL NAMBA AU KWA MHASIBU.
BODABODA NA MADEREVA WENGINE WA PIKIPIKI HASA WA DAR-ES-SALAAM NAO WANA FAMILIA. HUU UONEVU WA KUPIGWA FAINI KUBWAKUBWA UNAWAONGEZEA STRESS ZA MAISHA. MUDA UTAONGEA.
Hapa ndo hapo nawaona bodaboda hawana kitu kesho utawakuta na mitisheti ya mboga mboga akat imetomea centroHalafu bodaboda mnaunga juhudi wanasiasa wkt wa uchaguzi kwa mafuta ya buku 5!!
Makonda huyo huyo akiwaita mnajaza mibendela ya chama kama vibaka!
Sent using Jamii Forums mobile app
Wkat anagawa vyumba vya kulala nlikua naangalia draft watu wanacheza so siku pewa chumba.
Jidanganye siku nmekamatwa nalala central alikamatwa mwanajeshi kabebwa kwenye pikipiki na yy wakamuunganisha. Sasa akawa anawaambia yy ni mwanajeshi kwa kujiamini mzee kilichompata ni siri yangu ila akili ilimkaa sawa. Akapewa kesi ya kumpiga askariPole sn Kiongozi
Kwakua unatumia pikipiki kwa lengo la kuleta ufanisi ktk kazi yako tena kihalali Naomba nianzie kwa ushauli huu:
1. Tumia pikipiki tofauti na bodaboda (Click, XL, XLR and alike)
2. Gundua majina ya Askari, No za kazi na No za simu vyote weka hapa.
3. Usiogope kutumia silaa nyepesi inapolazimu. Km mtu anachezea maisha yako Kwnn unaeshimu ya kwake!
Kwa hiyo kwa awamu hii ya jiwe wanajeshi hawana nguvu???Jidanganye siku nmekamatwa nalala central alikamatwa mwanajeshi kabebwa kwenye pikipiki na yy wakamuunganisha. Sasa akawa anawaambia yy ni mwanajeshi kwa kujiamini mzee kilichompata ni siri yangu ila akili ilimkaa sawa. Akapewa kesi ya kumpiga askari
Sent using Jamii Forums mobile app
kenge awa m walinichomolea funguo kumbe pkpk nshaiunga direct ile anasogea atua moja tu akuamn nilvyo pepea[emoji16]
Sent using Jamii Forums mobile app
Dua la kuku halimpati mwewe!Polisi Tanzania ni kati ya Jeshi ambalo sina Imani nalo hata kidogo, mwezi wa 11 walikula 150,000 yangu kwa kosa la kubambika.
Ila najua hao waliogawana hiyo pesa yangu hawatakaa wapate amani ya moyo na matendo hayo.
Kama kuna polisi yumo humu na amesoma hizi comments mjue mnafanya dhuruma ambayo laana yake haitakaa iishie kwenu, itakula hadi watoto na wajukuu wenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nyie hasikari, siku mkikaria misumarri ndiyo mtapata hakirri.👮🔫🔫🔫Dua la kuku halimpati mwewe!
Tunakula hela zenu na laana haitupati.
Tumemuua Mwangosi, muuza magazeti huko Morog. Akwilina na wengi wengineo ndiyo kwanza tunanenepa, we subiri kama tutalaanika.
Sent using Jamii Forums mobile app