MATHIAS KABYEMERA
JF-Expert Member
- Mar 7, 2013
- 1,793
- 573
huyu jamaa sijui ana elimu ya dunia gani. Post zake ni hizi hizi tu! mara ndoto mara uchawi! Naumuogopaga balaa
Kwanini
Ndoto nyevu zina mengi ndani yake4. Ndoto nyevu na kuota unafanya mapenzi mpaka unatoa manii kabisa, hii mara nyingi huwatokea wale wenye kuleta nyodo kwa wanawake na kujisikia kulikopitiliza.
Mh mbn km siamini hivi
Msaada tofauti ya mchawi na mshirikinaNi imani zenye uhalisia kuna kundi kubwa sana la watoto wachawi na washirikina.. Tena mahiri hasa Jiulize katika umri ule kajifunza au kafunzwa saa ngapi? Tena yuko daraja la juu! Kumbuka Uchawi na ushirikina pia vina madaraja
Ndoto nyevu zina mengi ndani yake
-ushirikina
-kufanya mapenzi na majini na mapepo
-ugwadu
- ndoto za kawaida
Mungu wangu hii ni real jitahidi kujipakaza ndimu na kuogea chumvi hayo ni majini ukiyazoea hutatamani mwanamke
naomba unitag na mieKuna mada yake hili nikiipata takutag. . ni lazima wawe na kasoro kwakuwa ule si uumbaji wa Mungu... Nadhani ile mada inaitwa watoto wa kuzimu

Mojawapo wa vizazi vya duniani ni kizazi cha wachawi washirika na walozi. Hii ni jamii inayofanya kila mbinu kujitanua na kujijengea himaya kubwa na yenye nguvu zaidi duniani.
Kwenye ulimwengu wa kishirikina, mchawi mzuri na wa uhakika si yule wa kurithishwa au kufunzwa duniani (kwenye post zilizopita tumeona kuna vyuo vya kishirikina) hawa wanakuwa si halisi hawa wana damu na makandokando ya kiimani na starehe za kidunia, kwahiyo wachawi hufanya kila aina ya mbinu kupata kizazi chao kisichochakachuliwa kwa njia zifuatazo:-
1. Kutumia wanawake wanaojiuza, vyovyote ufanyavyo ukifanya naye ngono kwa kondom au bila kondom lazima manii zako utaziacha. Kujiokoa na hili tumia kondom kisha ukimaliza kufanya dhambi zako katupe chooni usikubali yeye ndio afanye hiyo kazi itakula kwako.
2. Kutumia mahawara na nyumba ndogo wanaopenda kwenda kwa waganga. Yeye atatumwa manii zako ili atengenezewe dawa kumbe ndio watu wanazichukua wakafanyie yao.
3. Kupenda kujichua, mara nyingi hii watu hufanyia bafuni kule nako watu huweka mtego yao na kuchukua malighafi. Na hii mara nyingi ni kwa wale watu wazima.
4. Ndoto nyevu na kuota unafanya mapenzi mpaka unatoa manii kabisa, hii mara nyingi huwatokea wale wenye kuleta nyodo kwa wanawake na kujisikia kulikopitiliza.
Manii hizi huchanganywa na madawa na kwa njia za kishirikina huwekewa wanawake wenye mimba changa au mimba zinazotunga na kulea mimba ya kichawi mpaka mtoto anazaliwa akiwa mchawi. Mtoto wa namna hii huwa agent tangu kuzaliwa kwahiyo hata ahubiriweje hawezi kubadilika.
Jiepushe na haya kwa:
1. Kuwa na mwenza mmoja mwaminifu
2. Kuhifadhi manii zako vizuri kwa namna yoyote ile na kwa hali yoyote ile, hakikisha haziangukii mikononi mwa yeyote
3. Kuepuka uwezavyo kufanya masturbation na kufanya mapenzi na watu usiowafahamu
Kwa njia hii utasaidia mno kudhoofisha kizazi cha kichawi na kishirikina


, mkuu umetoa changamoto 4, umekuja na suluhu 3, hiyo suluhu 1 imepotelea wapi, hasa hiyo inayohusiana na changamoto ya 4?