Ushawahi pitia kama hii single father?

Ushawahi pitia kama hii single father?

Ni ngumu kwa sana kwa mama wa kambo kumpenda mtoto asiye wake. Hii kitu sikia tu kwa wengine. Tena mbaya zaidi ukute huyo mama wa kufikia hana mtoto. Naanza kukuelewa mkuu. Story saingine ikiwa nusu ni rahisi mtu kuhukumu

Mara nyingi inatokea ikiwa mwanaume hana maokoto
Ukiwa na maokoto mwanamke atakupenda na kizazi chako chote
 
Wakati bado unajitafuta mlee mtoto kwa misingi mizuri ya kimaadili na kimila hakiisha unamuasa kila upatapo nafasi kuhusiana na maisha hasa kujiheshimu na bidii, lakini yote ya yote mpe msingi wa dini hii itamsaidia hata kama atakuja kukengeuka huko mbeleni basi awe na msingi wa dini utakaomsaidia kujikwamua

Sijajua we ni imani gani ila Biblia inasema mlee mtoto katika njia impasayo nae hataiacha hata atakapokuwa mzee

Kila la heri
 
Brother hauna mzazi yoyote ambaye yuko hai ?
Kama bibi yake yuko hai jaribu kumpeleka akapate maradhi mazuri, huyo mtoto una mduhurumu vitu vya msingi baadae atakuja kukulahumu huyo 🥹
Wapo lkn nimewaambia subilin kwa sasa sina changamoto ambayo binafsi ninaona nimtoe dogo ila kama kunamabadiliko yakitokea nitafanya hivyo tunaishi vizuli kabisaa kwa furaha na amani tele
 
Mkuu ulianza kukaa naye akiwa na miaka mingapi?
 
Hakikisha yupo huru kukueleza kama atakutana na changamoto huko nje.

NB: Hiyo bond uliyotengeneza na bintiyo ni ngumu mno kuishi na mke na mkawa kama mlivyo sasa labda umpeleke mahali.

Mama wa kambo akija,kazi ya kwanza itakuwa ni kukufitinisha naye sasa utachagua nani abaki.
 
Mama yake yupo hai lkn hana makazi maalum, mama yake tulitengana miaka mingi iliopita binti akiwa mdogo baadae nikaja owa mwanamke mwingine, kutoka na maisha alikuwa anaishi kwa mama yake ilibidi nimchukue dogo nikae nae, baada kama miaka 4 ya kuishi mke niliekuwa nae amesema eidha aondoke yeye au mtoto arudi kwa mama yake,

Mama yake ni muhangaikaji leo yupo Dar anaweza kaa miezi miwili kesho ukasikia yupo Mbeya ,

Kiukweli mm nimekataa kumtoa mtoto ili nibaki na mwanamke kupitia hili mwanamke akaamua arudi kwao nimebaki na mtoto , kama ww unafanyaje??
Baki na mwanao.
 
Good life lakini it is better ukawa na dada wa Kazi hapo nyumbani kwa ajili ya kufanya shughuli mbili tatu hapo nyumbani .
 
Habarii hivi ushawahi kupitia hii

Ninaishi na bint wa miaka nane mimi ndio mama nyumbani tupo .

Usiku ninapika chai naiyacha kwenye chupa, asubui mm huwa ninawai kutoka kabla yake namuacha amelala wala simuamshi.

Akiamka anafagia wanja na kuosha vyombo, anakunywa chai na kwenda shule.

Ikiwa yeye atawai kurudi shule kabla ya mm anakula na kwenda sehem nyingine ambayo ni kwa ajili ya masomo ya jioni.

Ikiwa mm nitawai kurudi nitapika chakula cha mchana,

Ikiwa yeye atawai kurudi kuna mazingila nimemtengenezea aweze kula,

Vitu vya muhimu nilivyofanya,

Nina sim ndogo nimeacha ndani ambayo nimejiunga halichachi kwa maana muda wowote anaweza kupiga, nimemuandikia namba,za watu wa karibu ikiwa na dhalula awapigie nimewka funguo nje ili ikitokea amepoteza funguo au aliondoka na kuniacha mm nyimbani akasahau kubeba funguo akija aweze kufungua mlango

Nimeacha pesa ya dhalula ikiwa nimesahau kuacha pesa ya vitafunwa asubui akachukue pale anunue vitafunwa.

Changamoto ninazopitia ni ndogo sana lkn ninamshuku mungu nipo salama na bint yangu na maisha yanasonga,

Nawakaribisha mp kama kuna mwanamke amevutiwa na hii familia aje kuwa mtu wa 3, karibu mp


Unajiweza sana, usikaribishe matatizo Nyumbani kwako. Kama una ndugu binti mkubwa hata wa kumsaidia kusoma course kama cherehani, mlete amchangamshe Dogo, Mambo ya kuoa waachie Vijana wa kinondoni maana hawanaga mda na malezi ya watoto.
 
Kijana wa miaka 7 naishi nae geto mwaka wa pilii huu .
Nataman kuwekaa picha hapa ninazopiga naye Kila cku tukiwa zetu geto ,tukipika,tukifua,tukiangalia mpira yaan n full burudanii,,

Changamoto niliyonayo n yy ajuagi muda maalumu wa kusomaa anaweza shtuka usingizi saa Saba usiku akawasha taa akaanza kusomaa vitabu vyake mpk achoke ,ss mm akishawasha taa tu usingizi kwisha NAMI kumkataza kutokusoma nashindwa najisemeaga labda akisomaa muda huu ndio anaelewa zaidii

Kiukwel n msela wangu ,n rfk pia n mshikaji...
Dah hongera mkuu,Kwa ishu ya kuamka kusoma inabidi uzoee tu,good stuff.
 
Boss,wewe una tatizo,Mazingira unayolea huyo mtoto ni mazingira hatari sana,kwa umri wake.Kama una ndugu au rafiki ambaye ana stable family mpeleke, Au mpeleke kwa bibi mzaa baba au hata mjomba au shangazi.

Maana naona kuo umeshindwa na kwa namna fulani huwamudu wanawake.Utamuharibu mwanao kuwa makini usijemfanya Mke na wewe ukawa ndio abuser number one.
 
Kimkakati sana hili bandiko.

Ila sijaona ni wakati gani unafuatilia maendeleo yake Mkuu, kama mzunguko wa maisha yenu upo hiv ulivyoelezea huyo binti yupo kwenye mazingira hatarishi sana tofauti na vile unavyoweza kufikiri.

Huyo binti muda wowote anaweza kuwa mhanga wa ukatili na wala wewe usifahamu/kujua au ukaja kujua ikiwa ushachelewa.

Mtengenezee mazingira rafiki kwa umri wake Mkuu. Usimpore utoto wake ili tu wewe uweze kuishi kwa amani, kuna hatua muhimu sana hasa ikizingatiwa huyo ni mtoto wa kike. Anahitaji kuandaliwa vyema aje kuwa mama wa wanawe pia.

Ni ngumu kwa wengi kuelewa hili swala.
Umeongea kama mwanaume na baba🤛
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom