lonelygal
JF-Expert Member
- Apr 11, 2017
- 208
- 166
Sikuwahi kujua kama mapenzi yanaweza jeruhi kiasi hiki aisee, kiasi cha kuona dunia imesimama. Nilikuwa tu nasikia na kusoma tu kama hadithi. Dah mtu uliyempa Moyo wako kwa dhati kabisa yeye anakuchukulia poa khaaa sijui inawezekanaje jamani.
Hata siamini Mungu tu anipe nguvu niweze muondoa akilini ili nisonge mbele. Maana nampenda sana hadi nashindwa kuelewa sababu tu. Usithubutu kukutwa na hali hii katika maisha yako, ni uzoefu mchungu mno.
Hivi huwa kuna uwezekano kuwa na uhusiano halafu mmoja wenu awe tu malaika asimkosee mwenzie kabisa? Akimkosea mwenzie kosa tu dogo mawasiliano yanakatika? Lakini wakati huo yeye anakukosea sana tu na unamsamehe bila kujali kwa vile tu unampenda?
Kama unajua hauko serious kwanini sasa usababishe shida kwa mwenzio kiasi hiki jamani? Kwanini jamani drama hizi. Sina majibu sahihi nina maumivu makali mno! Njooni mnisaidie nitokeje hapa please.
Mmmh ama kweli kuishi kwingi kuona mengi, nimeamini hata kivuli chako chaweza kukusaliti siku moja. Nimeamua kusema huku labda naweza pata nafuu kwa kutoa nyongo hii ila siyo rahisi kabisa.
Naombeni nasaha zenu
Hata siamini Mungu tu anipe nguvu niweze muondoa akilini ili nisonge mbele. Maana nampenda sana hadi nashindwa kuelewa sababu tu. Usithubutu kukutwa na hali hii katika maisha yako, ni uzoefu mchungu mno.
Hivi huwa kuna uwezekano kuwa na uhusiano halafu mmoja wenu awe tu malaika asimkosee mwenzie kabisa? Akimkosea mwenzie kosa tu dogo mawasiliano yanakatika? Lakini wakati huo yeye anakukosea sana tu na unamsamehe bila kujali kwa vile tu unampenda?
Kama unajua hauko serious kwanini sasa usababishe shida kwa mwenzio kiasi hiki jamani? Kwanini jamani drama hizi. Sina majibu sahihi nina maumivu makali mno! Njooni mnisaidie nitokeje hapa please.
Mmmh ama kweli kuishi kwingi kuona mengi, nimeamini hata kivuli chako chaweza kukusaliti siku moja. Nimeamua kusema huku labda naweza pata nafuu kwa kutoa nyongo hii ila siyo rahisi kabisa.
Naombeni nasaha zenu