lee Vladimir cleef
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 9,154
- 33,367
Ewe mkulima usifurahie mfanyakazi kutoongezwa mshahara,kwani mtumishi wa sekta yeyote ni mteja wa mazao yako,asipoongezwa hutauza mazao yako kikamilifu.
Ewe mfanyabiashara,usifurahi kwa mtumishi kutoongezwa mshahara ,asipoongezwa ,hatanunua bidhaa dukani mwako ,asiponunua ,hutapata pesa za kutosha kuendesha maisha yako,naye mzalishaji kiwandani hatazalisha bidhaa kwa wingi.
Nawe mtumishi usifurahie mkulima asipolipwa malipo yake kikamilifu,asipolipwa hatalima mazao zaidi,hivyo kupelekea bidhaa kupungua masokoni na kufanya bei kupanda.
Pia ewe mfanyakazi usifurahie mfanyabiashara kubugudhiwa,akibugudhiwa huacha kufanya biashara,huondoka ,hivyo husababisha bidhaa kuadimika,zikiwa chache bidhaa,bei hupanda,matokeo yake maisha huwa magumu sio kwa mfanyakazi tu,bali pia kwa mkulima na mfanyabiashara.
Madhara yake ni nini?
Madhara yake ni mifarakano,
Tuungane wafanyakazi,wakulima na wafanyabiashara kudai haki zetu,tusifurahie matatizo ya mmoja wetu.
Wenye akili wamenielewa.
Ewe mfanyabiashara,usifurahi kwa mtumishi kutoongezwa mshahara ,asipoongezwa ,hatanunua bidhaa dukani mwako ,asiponunua ,hutapata pesa za kutosha kuendesha maisha yako,naye mzalishaji kiwandani hatazalisha bidhaa kwa wingi.
Nawe mtumishi usifurahie mkulima asipolipwa malipo yake kikamilifu,asipolipwa hatalima mazao zaidi,hivyo kupelekea bidhaa kupungua masokoni na kufanya bei kupanda.
Pia ewe mfanyakazi usifurahie mfanyabiashara kubugudhiwa,akibugudhiwa huacha kufanya biashara,huondoka ,hivyo husababisha bidhaa kuadimika,zikiwa chache bidhaa,bei hupanda,matokeo yake maisha huwa magumu sio kwa mfanyakazi tu,bali pia kwa mkulima na mfanyabiashara.
Madhara yake ni nini?
Madhara yake ni mifarakano,
Tuungane wafanyakazi,wakulima na wafanyabiashara kudai haki zetu,tusifurahie matatizo ya mmoja wetu.
Wenye akili wamenielewa.