Elungata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 40,343
- 33,487
hahaha,..huo ndo mpango mzima,mengine ni mahangaiko na mahangaiko ya wanadamu.Nendeni kanisani au kwa shehe baada ya hapo mnasepa zenu hotelini. haki ya nani hata laki mbili hazifik
hahaha,..huo ndo mpango mzima,mengine ni mahangaiko na mahangaiko ya wanadamu.Nendeni kanisani au kwa shehe baada ya hapo mnasepa zenu hotelini. haki ya nani hata laki mbili hazifik
Tafuta resort/hotel/baa yenye garden, kisha fanya yafuatayo...
1. Nunua nyama ya ng'ombe kilo 30 --- sh 180,000
2. Nunua bia/soda chupa 2 kila mtu --- sh 200,000
3. Nunua ndizi mzuzu --- sh 50,000
4. Nunua keki --- sh 100,000
5. Nunua shampeni chupa 10 --- sh 100,000
6. Tafuta mtu mwenye mziki --- sh 200,000
7. Kama huna rafiki mwenye v.camera, kodisha --- 200,000
8. Tafuta mchoma nyama na jiko na mkaa --- 70000
Jumla 1,000,000/=
Achana na mambo ya Mc, Tarumbeta wala mapambo. Usiweke jukwaa, viti visipangwe, itakuwa kama cocktail party... Kadi za mwaliko tengeneza mwenyewe, au fanya kwa sms... Marafiki zako uwataarifu kuwa mtu akifika ukumbini, kama anaweza achangie kununua kinywaji chochote..., kama ni chupa moja hya, kama ni kreti haya... Marafiki zako wataimba, watawarushia maua, watajenga tunnel kwa mikono yao nyie mtapita chini yake n.k, ili mradi itakuwa shamrashamra. Mtakata hiyo keki, na mtahakikisha mmewalisha wote, shampeni kumi zitafunguliwa na watu tofauti na zitaongeza shmrashamra, nyama za kuchoma na ndizi zitakuwepo mda wote jikoni, mtu anaenda kujichukulia anavyotaka, vinywaji vitasambazwa kwenye meza moja, mtu anajichukulia anavyotaka, ndugu jamaa na marafiki watakuwa na wasaa wa kuongea chochote wanachojisikia kuongea (kusiwe na formality), mtacheza sana mziki... nk...
Natamani ningekuwa na uwezo wa kukutumia mkanda wa arusi yangu ilivyokuwa simple, but ilipendeza...
Watu 40...laki si pesa
milioni si mtajii?
Harus ya milioni kweli au watu 100 tu mkuu?
Kama ni ivo sawa.
Na life ili la kidigital kila kitu bei juu
simple zipo but sio milion arusi kweli.
Kwanza mdogo wangu; hongera kwa hatua ulofikia ya kukubali kuungana na mwenzi wako kuwa mwili mmoja.
Ushauri wangu uko vipi;
Kwanza usikubali kufanya mambo ambayo yatakuingiza hasara na kukufanya uanze maisha mapya kwa kulipa madeni yasiyo ya lazima. Horodhesha marafiki zako wa karibu (naamini wanaweza kufika 40/50); Mwambie na mwenzako afanye hivyo hivyo; mtapata horodha ya watu wasiopungua 100. Kati ya hao mia waite 50 kwenye kikao kidogo na uwaeleze unataka kufanya nini; usikubali kupokea michango ya ufadhili kutoka pembeni; watumie marafiki zako wa karibu tu.
Mtakaa na kupanga bajeti ambayo nakushauri izingatie mambo yafuatayo:-
Tafuta hotel ambayo watakupa ukumbi free. Utafanikiwa kwa kufanya utafiti wa kwa siku mauzo yake ni Tshs. ngapi?
Hapo hapo hotelini kanunue kila kitu pale kwa bei mtakayokubaliana. Hotel nyingi siku hizi zina mziki mzuri tu; si wa kelele wala wa kuserebuka.
Gharama za usafiri kwa maharusi, mavazi n.k hizo mjigharimie wenyewe.
Ndani ya marafiki zako / mume wako - hapatakosa mtu anayeweza kuendesha sherehe ndogo hiyo.
Nakuhakikishia utatumia gharama kidogo na sherehe itafana sana; ila kumbuka baada ya harusi yenu utalaumiwa na wengi kwa kutokuwashirikisha kwenye sherehe hiyo. .
Ukitaka nikupatie bajeti ya kimahesabu niko tayari.
Habarini za majukumu wana JF
Ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya, jamani mimi ninakaribia kuolewa, ila kutokana na hali ya maisha tumekubaliana na mwenzangu tufanye harusi ya gharama ndogo.
Nimeamua kuomba ushauri wa jinsi ya kufanya sherehe hiyo kwa gharama ndogo sana, kwanzia mavazi mpaka chakula nisaidien wana jukwaa.
Karibuni.
Habarini za majukumu wana JF
Ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya, jamani mimi ninakaribia kuolewa, ila kutokana na hali ya maisha tumekubaliana na mwenzangu tufanye harusi ya gharama ndogo.
Nimeamua kuomba ushauri wa jinsi ya kufanya sherehe hiyo kwa gharama ndogo sana, kwanzia mavazi mpaka chakula nisaidien wana jukwaa.
Karibuni.
hatupati feedbackHabarini za majukumu wana JF
Ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya, jamani mimi ninakaribia kuolewa, ila kutokana na hali ya maisha tumekubaliana na mwenzangu tufanye harusi ya gharama ndogo.
Nimeamua kuomba ushauri wa jinsi ya kufanya sherehe hiyo kwa gharama ndogo sana, kwanzia mavazi mpaka chakula nisaidien wana jukwaa.
Karibuni.
Kama unaishi mjini huwezi kuepuka gharama maana ndoa ni ya kwako na mwenza wako ila sherehe ni ya wazazi wenu,ndugu,jamaa na marafiki,huwa ikifika hapo ni vigumu sana kuepuka gharama ila kama utapunguza uwepo wa niliowataja hapo inawezekana ikapungua kidogo sana kitu ambacho hakiwezi kubadili unachokihitaji.