Radio Producer
JF-Expert Member
- Feb 4, 2011
- 728
- 320
Heshima mbele wakuu,
Kwenu TBC na Mkurugenzi TBC.
Kwanza kabisa, mimi Radio Producer nawapa pole kwa majukumu mengi na magumu mnayoyapitia katika suala zima la kuifanya TBc isonge mbele. Kiukweli mimi napenda sana kutoa ushauri kwenye media houses mbali mbali. Natoa ushauri kuhusu programming, production, follow-up na mengine! Kwa elimu niliyonayo nimeona ninaweza kuwashauri au kutoa maoni yangu kwa TBC. Kama ninavyoelewa umuhimu wa FEEDBACK katika fani hii nina imani pia kuwa mtayapokea maoni na ushauri wangu! Hapa chini ndiyo ushauri wangu ulivyokaa:-
1. Programming
Ukweli ni kwamba mna vipindi vingi sasa na ni vizuri sana na vinasaidia sana. Nikifuatilia kote kote TBC1, TBC Taifa, TBC fm hata TBC2 ukweli mnajitahidi sana katika suala la vipindi kwa ujumla. Vipindi vyenu vina heshima, vinajali kanuni zote za uaandaaji wa vipindi na kwamba vinaweza kuangaliwa na watu wa umri tofauti tofauti.
Tatizo au changamoto mliyonayo kwenye programming iko upande wa NEWS.
Mnakosa kitu BALANCE, kiukweli hapa mna matatizo makubwa sana. Kwasasa hamfuati kabisa kanuni za uandishi wa habari ila mmejiingiza kwenye siasa. Hata habari zenu zote zimekuwa za kisiasa siasa tu! Juzi juzi nilikuwa naongea na moja ya wanafunzi waliofukuzwa UDOM, akaniambia "ninashangaa sana TBC walitoa madai tofauti na yale ambayo sisi tulikuwa tunayadai wakati wa mgomo, yaani tulishangaa kuona hivyo" Je, hivi nyinyi sources zenu za news mbona zimekuwa za upendeleo sana siku hizi? Hivi kwanini mpaka mbadilishe habari? mnaibadilisha ili kudanganya umma? kwa hili mmepotea njia kabisa!
2. Credibility
Jueni kabisa kwamba vyombo vya habari vinaongozwa na hiki kitu credibility. Sasa nyinyi mmepoteza sana credibility yenu kwa watu! Yaani kila mtu siku hizi ukifika wakati wa news ukiweka TBC anakwambia na wewe ni magamba? weka ITV au Star TV bwana. Yaani sijui kitengo chenu cha ufuatiliaji kinafuatilia kweli juu ya hili? Kama watu wanakwepa kuangalia news zenu kweli kabisa hamuoni kuwa mmepoteza credibility?
Jilinganishe na TV zingine za nchi zingine, Angalieni hata ya wenzenu KCB1 iko tofauti mno na nyie. angalieni TV za nchi zingine mjifunze. Mmekuwa mnaficha ukweli na kutetea uovu hivi ndivyo ilivyo kwenye media kweli? Nyinyi ndiyo mnatakiwa myafichue maovu lakini leo ndo imekuwa kinyume. Ndiyo maana Jerry Muro yalimkuta hayo, kwa sababu hampendi ukweli.
MAMBO YA KUZINGATIA.
1. Jiondoeni kwenye siasa, wekeni news balance ziwe wazi kwa watu wote.
2. Acheni kutetea chama tawala, simamieni haki katika nchi yetu, komboeni maisha ya wanyonge kwa kuionyesha jamii ukweli halisi.
3. Fuateni kanuni za uandishi wa habari, achenikujifanya hamzijui.
4. Jengeni kuaminika (credibility) kwa watanzania wote.
5. Shida yenu kubwa ni hapo tu BALANCE ya NEWS na matukio mbali mbali.
Asanteni kwa kunielewa.
Radio Producer.
Kwenu TBC na Mkurugenzi TBC.
Kwanza kabisa, mimi Radio Producer nawapa pole kwa majukumu mengi na magumu mnayoyapitia katika suala zima la kuifanya TBc isonge mbele. Kiukweli mimi napenda sana kutoa ushauri kwenye media houses mbali mbali. Natoa ushauri kuhusu programming, production, follow-up na mengine! Kwa elimu niliyonayo nimeona ninaweza kuwashauri au kutoa maoni yangu kwa TBC. Kama ninavyoelewa umuhimu wa FEEDBACK katika fani hii nina imani pia kuwa mtayapokea maoni na ushauri wangu! Hapa chini ndiyo ushauri wangu ulivyokaa:-
1. Programming
Ukweli ni kwamba mna vipindi vingi sasa na ni vizuri sana na vinasaidia sana. Nikifuatilia kote kote TBC1, TBC Taifa, TBC fm hata TBC2 ukweli mnajitahidi sana katika suala la vipindi kwa ujumla. Vipindi vyenu vina heshima, vinajali kanuni zote za uaandaaji wa vipindi na kwamba vinaweza kuangaliwa na watu wa umri tofauti tofauti.
Tatizo au changamoto mliyonayo kwenye programming iko upande wa NEWS.
Mnakosa kitu BALANCE, kiukweli hapa mna matatizo makubwa sana. Kwasasa hamfuati kabisa kanuni za uandishi wa habari ila mmejiingiza kwenye siasa. Hata habari zenu zote zimekuwa za kisiasa siasa tu! Juzi juzi nilikuwa naongea na moja ya wanafunzi waliofukuzwa UDOM, akaniambia "ninashangaa sana TBC walitoa madai tofauti na yale ambayo sisi tulikuwa tunayadai wakati wa mgomo, yaani tulishangaa kuona hivyo" Je, hivi nyinyi sources zenu za news mbona zimekuwa za upendeleo sana siku hizi? Hivi kwanini mpaka mbadilishe habari? mnaibadilisha ili kudanganya umma? kwa hili mmepotea njia kabisa!
2. Credibility
Jueni kabisa kwamba vyombo vya habari vinaongozwa na hiki kitu credibility. Sasa nyinyi mmepoteza sana credibility yenu kwa watu! Yaani kila mtu siku hizi ukifika wakati wa news ukiweka TBC anakwambia na wewe ni magamba? weka ITV au Star TV bwana. Yaani sijui kitengo chenu cha ufuatiliaji kinafuatilia kweli juu ya hili? Kama watu wanakwepa kuangalia news zenu kweli kabisa hamuoni kuwa mmepoteza credibility?
Jilinganishe na TV zingine za nchi zingine, Angalieni hata ya wenzenu KCB1 iko tofauti mno na nyie. angalieni TV za nchi zingine mjifunze. Mmekuwa mnaficha ukweli na kutetea uovu hivi ndivyo ilivyo kwenye media kweli? Nyinyi ndiyo mnatakiwa myafichue maovu lakini leo ndo imekuwa kinyume. Ndiyo maana Jerry Muro yalimkuta hayo, kwa sababu hampendi ukweli.
MAMBO YA KUZINGATIA.
1. Jiondoeni kwenye siasa, wekeni news balance ziwe wazi kwa watu wote.
2. Acheni kutetea chama tawala, simamieni haki katika nchi yetu, komboeni maisha ya wanyonge kwa kuionyesha jamii ukweli halisi.
3. Fuateni kanuni za uandishi wa habari, achenikujifanya hamzijui.
4. Jengeni kuaminika (credibility) kwa watanzania wote.
5. Shida yenu kubwa ni hapo tu BALANCE ya NEWS na matukio mbali mbali.
Asanteni kwa kunielewa.
Radio Producer.