Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
Ingawa nipo safarini kuelekea Arusha katika Mkutano wa nusu mwaka wa TLS,nimewiwa kumshauri jambo Mbunge wa Geita Vijijini,Ndugu Joseph Kasheku 'Msukuma'. Ushauri wangu unafuatia kadhia iliyompata ya kukamatwa na kushtakiwa kwa kuhujumu miundombinu ya maji
Ndugu Msukuma amekuwa na juhudi za kumsema na 'kumtisha' Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Geita,kabla na baada ya kukamatwa kwake. Amekuwa akimzungumzia RPC wa Geita kana kwamba ni raia wa kawaida anayeweza kumsema kisiasa atakavyo. Pia,Msukuma,kwa uelewa wangu,analenga 'kumchongea' RPC wa Geita kwa wateule wake.
Nataka kumpa taarifa Msukuma,na kumshauri. Kwanza,polisi si raia. Polisi hawana chama. Polisi ni chombo cha dola;chombo cha Serikali na wananchi kwa ujumla. Polisi wanapaswa kuheshimiwa kwakuwa wanafanya kazi kubwa kwa ulinzi wetu na ulinzi wa mali zetu. Msukuma anapaswa kuwaheshimu polisi na kuwaweka mbali na mikwara yake ya kisiasa.
Serikali ni yetu sote. CCM si watanzania wote na hivyo Msukuma asitambie. Kwakuwa tayari jambo lake liko mahakamani,anapaswa kunyamaza kimya na kushughulika na jambo lake. Kumsema na kumtisha RPC hakutamsaidia. Anaowategemea wamsaidie kichama wako kimya kwakuwa wameona kuwa Msukuma hana hoja!
Ndugu Msukuma amekuwa na juhudi za kumsema na 'kumtisha' Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Geita,kabla na baada ya kukamatwa kwake. Amekuwa akimzungumzia RPC wa Geita kana kwamba ni raia wa kawaida anayeweza kumsema kisiasa atakavyo. Pia,Msukuma,kwa uelewa wangu,analenga 'kumchongea' RPC wa Geita kwa wateule wake.
Nataka kumpa taarifa Msukuma,na kumshauri. Kwanza,polisi si raia. Polisi hawana chama. Polisi ni chombo cha dola;chombo cha Serikali na wananchi kwa ujumla. Polisi wanapaswa kuheshimiwa kwakuwa wanafanya kazi kubwa kwa ulinzi wetu na ulinzi wa mali zetu. Msukuma anapaswa kuwaheshimu polisi na kuwaweka mbali na mikwara yake ya kisiasa.
Serikali ni yetu sote. CCM si watanzania wote na hivyo Msukuma asitambie. Kwakuwa tayari jambo lake liko mahakamani,anapaswa kunyamaza kimya na kushughulika na jambo lake. Kumsema na kumtisha RPC hakutamsaidia. Anaowategemea wamsaidie kichama wako kimya kwakuwa wameona kuwa Msukuma hana hoja!