That is not the main reason, there is the truth within yourself, kama ulikulia makuuzi ya kukulalamikia kila mala, wazazi, kaka zako, dada zako, yaani kila kitu kitakuwa lawama tu. Kila jambo unaliangalia kwa négativité, maana katika kukua kwako hukupewa mtazamo chanya. kadri unavyokuwa unakuwa unapoteza ile nguvu chanya maana unachoambiwa utotoni ni negative tu. Hali hiyo inakupelekea kuwa na nguvu hasi, mwoga mwoga, hasira zisizo na kichwa wala miguu, chunguza watu waoga wengi ni wanakuwa na hasira sana wakichukia. Na hizo nguvu zinakufata popote, darasani unakuwa unaogopa kuongea, ukingoja daladala zinapita tu zote zimejaa, ila unashangaa mbele kidogo inasimama inabeba abiria, ukiwa kwenye foleni ya chalupa kinaisha kabala wewe hujapata.
Hata hizo negativite zigeuze positive, jifunze kushukuru kuliko kuhukum
Anza kuangalia mambo kwa mtazamo chanya, anza kujichanganya na watu wa rika mbalimbali, ongea mbele za watu hata kama utachekwa lakini ndio mwanzo wa kujifunza public speech.
Kinyume cha Love ni Chuki-Anza kujipenda, jikubari mwenyewe, penda vile ulivyo, kama uko kafupi, mrefu, mweusi tii au mweupe pee.,,..jikubari utaona nuru usoni kwako na maisha ya uwoga yatatoka taratibu. Na ukiweza kujipenda menyewe na kushukuru Mungu vile amekuumba, utaona unaweza wapenda wengine, namaanisha kupenda sio kujipendekeza, jipende na ujiheshim, utaheshim na kupenda jirani na marafiki na dunia kwa ujumla.