USHAURI TAFADHALI: Nime-fall kwa x-kicheche. Je atatulia?

USHAURI TAFADHALI: Nime-fall kwa x-kicheche. Je atatulia?

Me370

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2008
Posts
985
Reaction score
293
Ndugu zangu yapata miezi kama mi 3.5 hivi iliyopita nimeopoa bonge la mpenz. Mzuri ana mvuto wa nguvu na mkali kwenye kila idara hadi story zinapanda mwanzo mwisho. Financially independent e.t.c

Issue kubwa niliyonayo ni kuwa mpenz mwenyewe ni kicheche. Yaani ana historia ya kupitiwa na wanaume wengi huko nyuma. Hili halifichiki kwani mimi nalijua na yeye pia anajua kuwa najua. Kinachonikosesha usingizi jamani ni kuwa huyu mtoto kiukweli nampenda lakini je kweli anaweza tulia? Tabia yake ya nyuma inanifanya nisiamini lolote analoniambia yaani najihisi ni mmoja katika orodha ya wengi watakaofuata.

Matatizo mengine ni kuwa kanizidi karibia kila kitu. I mean nikijiangalia kwenye kioo najiona mbaya tuuuuuu alaf nikimuangalia mwenzangu kila ninapokua naye najiona kabisa hatuendani ingawa yeye anasema ananipenda then again wangapi wamesha ambiwa wanapendwa na huyu b4 me.

Mfano Juzi (Saturday) nlienda naye kwenye harusi ya mfanyakazi mwenzangu nikamtambulisha kama mpenz kwa watu ninaofanya nao kazi. Workmates wangu wote wakaanza kunimwagia misifa jinsi mtoto alivyo bomba. Karibia kila anayenijua (ikiwemo walio ma handsome zaidi yangu) wakawa wananiuliza nimempataje n.k. Boss wangu ndo kabisaa kaja na mkewe lakini wakati wa kucheza akaja mnyanyua mpenz wangu wakawa wanacheza huku wanapiga story na kucheka kwa furaha.

Yaani hata tukitoka Out najikuta tunatumia Gari yake (Nzuri kuliko yangu na ina A/c) kitu ambacho yeye anapenda. Mshahara wake ni zaidi ya ule wangu hadi nyumba tunazokaa yake nzuri zaidi. I keep asking myself will this relationship work?

Kinachonifanya ni hang-on hadi now ni kuwa amenitambulisha hadi kwa wazazi wake na baadhi ya marafiki kama mchumba wake. Ila Dingi mwenyewe alionekana hana time na mchumba wa binti yake. Mama yake naye anaongea naye kama dada yake.

Jamani embu nishaurini ni inferiority complex zangu tuu zinanisumbua ama niumalize tu huu uhusiano? Nimesha present concerns zangu kwake. Yeye akakimbilia kunikabidhi funguo za nyumbani kwake na kusema naruhusiwa kwenda hata saa nane za usiku. Bro alinishauri nimlazimishe anikabidhi simu yake. Nlivyomwambia tu akanipa hakubisha hata kidogo na hivi ninavyoandika hapa ninayo na imekuwa ikiita majina ya kike tuuu toka asubuhi ya leo (sijaipokea). Nime double check kwenye tigo pesa baadhi ya No zinaonekana legit. Kiufupi yuko tayari kufanya ninavyotaka hata gari kasema atapanda langu ingawa kimeo.

Nipo njia panda kumpenda nampenda sana lakini najihisi ntaumia zaidi huko mbele........... Mtu wa aina hii anaweza kweli kuwa a good wife? Niambie nimepotea au ndo penyewe?




 
Mmh, wewe ana mpango wa kukuufanya mme, ukishaoa anaendelea. kuchit kwa amani.

Oa tu, afterall wanawaaake wengi wanachit tu.
 
Me nilidhani unataka pongezi kwa kumaliza darasa la saba wiki iliyopita. Kuna mtu humu amewah kusema mwanamke haaminiwi kama mungu
 
Huu ni mwanzo tu ndugu, huenda kweli kaamua kubadilika na kutulia. Huenda hapo awali hakuwa amepata watu sahihi waliompa sababu za kuamini katika ndoa...

Nina mfano mmoja wa mwanamke kama huyo ambaye naye alipoamua kutulia aliacha yote nyuma na kuwa mtu mwema...

Kazi kubwa uliyonayo ni kumuaminisha huyo mwanamke kuwa wewe ndiye chaguo lake sahihi...
Fanya mambo yatakayo msuta kila atakapojaribu kuwaza kucheat.
 
Inaonekana hujiamini kaka, huyo ni wako na inaonekana yupo tayari kuacha yote ya nyuma.
 
Huyo amecheza hadi kachoka,kwa hiyo kaona huu ni muda wa kutulia ili
ajenge familia.Hii ni kwa sababu ya age go.
 
Mkuu mimi nadhani cha msingi songa nae mbele wewe ni mwanaume haina haja ya kuwa na uoga kwani yaliyopita sio issue maadam umejua alipotoka basi unatakiwa kumuongoza aendako na ukapata thawabu tele.Pia fanya unachoona/moyo wako unavyokutuma kama alivyoongea mdau mmoja hapo juu.Sometime inabidi kufukia na kusonga mbele maana ukiangalia ya Bata huwezi kula nyama yake tamu.
 
You can turn her to be a perfect wife, kikubwa love her to the maximum, care her tremendously , once she realize that he had beeen totally loved, she ll forget all her 2.5 million boy friends and the family will grow.
 
Wanaume bwana mnachekesha, mkipendwa mnajistukia. Nataka nikutie moyo kuwa kuna wakati ucheche wa mwanamke unasababishwa na nyie wanaume.

Mwanamke anakuwa anatafuta mwanaume wa kutulia naye lakini kila anayekuwa naye anamuacha, hivyo inapelekea kuwa na mahusiano na watu wengi lakini si kicheche kama wengi amb
avyo mngemwita. Anakuwa hajapata atakaye mpenda kwa dhati.

Hata huyo wako naamini amefika wakati anahitaji kutulia na mpenzi ambaye ni wewe. Kama umempenda wewe muoe. Hakuna miss perfect.
 
  • Ndugu Me370 kwani una umri gani?, Yawezekana umri wako ikawa ni sababu ya kutokujiamini kwa huyu mrembo akupendaye.
  • Mwanamke akiamua kutulia basi hutulia kweli, zuli zaidi unafahamu historia yake ya nyuma na yeye anatambua kwamba unajua.
  • Jiamini. Hakuna aliye mkamilifu.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom