sepema
JF-Expert Member
- Jun 13, 2019
- 591
- 1,000
Wakuu salaam,
Mara kadhaa mama amekuwa akimtuhumu mzee kujihusisha kimahusiano na mama fulani ambae ni shemeji yake. Mama amejaribu kufanya jitihada za kuwaachanisha kwa njia ya mazungumzo lakini wamegoma kuachana kabisa.
Mara ya mwisho mama kajaribu kumweleza mume wa huyo mchepuko kila kitu ila cha ajabu mzee yule kaamua kumtetea mkewe kuwa hana hizo tabia na hawezi kutoka kimapenzi na mzee wangu.
Upo ushahidi wakutosha kuwa mzee anatoka na huyo mama. Baada ya kuvumilia kwa miaka mingi mama ameamua anipigie simu kunishirikisha jambo hilo. Amenambia ameamua kunishirikisha mimi kwani ni kijana wake mkubwa na kwa hali ilivyo anaweza kupoteza maisha kwa pressure hivyo niangalie nini naweza kufanya.
Nimefikiria kumchukua bimkubwa niishi nae ila nahofia familia itajigawa. Ndugu wa mzee wameongea lakini mzee habadiliki kabisa, ndio kwaanza anachochea makaa kwenye treni. Nimefikiria kumvaa baba nimweleze kuhusu hilo tatizo nakwamba aache mara moja ila nahofia reaction yake. Wakuu; huu msala na utatua vipi ili ninusuru hii ndoa ya wazee wangu ambayo imedumu kwa zaidi ya miaka 30 Sasa.
Mwisho: Ukihisi huwezi kuchangia naomba usome nakupita. Kama itakulazimu kuchangia kwa kutukana, naomba hayo matusi yaelekee kwangu ila sio kwa wazazi.
Wasalaam!
Mara kadhaa mama amekuwa akimtuhumu mzee kujihusisha kimahusiano na mama fulani ambae ni shemeji yake. Mama amejaribu kufanya jitihada za kuwaachanisha kwa njia ya mazungumzo lakini wamegoma kuachana kabisa.
Mara ya mwisho mama kajaribu kumweleza mume wa huyo mchepuko kila kitu ila cha ajabu mzee yule kaamua kumtetea mkewe kuwa hana hizo tabia na hawezi kutoka kimapenzi na mzee wangu.
Upo ushahidi wakutosha kuwa mzee anatoka na huyo mama. Baada ya kuvumilia kwa miaka mingi mama ameamua anipigie simu kunishirikisha jambo hilo. Amenambia ameamua kunishirikisha mimi kwani ni kijana wake mkubwa na kwa hali ilivyo anaweza kupoteza maisha kwa pressure hivyo niangalie nini naweza kufanya.
Nimefikiria kumchukua bimkubwa niishi nae ila nahofia familia itajigawa. Ndugu wa mzee wameongea lakini mzee habadiliki kabisa, ndio kwaanza anachochea makaa kwenye treni. Nimefikiria kumvaa baba nimweleze kuhusu hilo tatizo nakwamba aache mara moja ila nahofia reaction yake. Wakuu; huu msala na utatua vipi ili ninusuru hii ndoa ya wazee wangu ambayo imedumu kwa zaidi ya miaka 30 Sasa.
Mwisho: Ukihisi huwezi kuchangia naomba usome nakupita. Kama itakulazimu kuchangia kwa kutukana, naomba hayo matusi yaelekee kwangu ila sio kwa wazazi.
Wasalaam!