Je, Kuna sababu ya lazima kwa mwanaume uliyezaa na mchepuko kuchukua huyo mtoto kumleta kwa Mke?

Weakman

JF-Expert Member
Jul 23, 2021
861
1,384
Wazee tufundishane hapa!

Kwenye maisha yetu Kama waume hii inatokea Mara nyingi tu. Mzee penzi limenoga kwa mchepuko, mara tu mimba hii hapa.

Wengine wanakataa ujauzito na mahusiano yanakufa!

Wengine wanaamua kuondoa mimba fasta, ili maisha yaendelee!

Wengine wanalea ujauzito na mtoto kwa Siri!
Lakini hata hivyo dunia Haina Siri, mwisho wa siku katoto kanatambaa, Mara kanatembea, ohooo hakoo kanaingia darasa la kwanza!
Mke amepata taarifa ya uwepo wa mtoto wa pembeni, Mara ooh katoto kameletwa ndani ya nyumba!

Hapa ndipo naleta hoja yangu!
Nini ulazima wa kumleta mtoto huyu ndani ya nyumba ya mke?

Hivi mama yake ameshindwa kumlea kweli, akipewa sapoti zote na baba husika?

Unamleta kwa mkeo apate Nini chenye ulazima wa kibinadamu atakachokikosa
kwenye makazi ya mama yake?

Je, baba utashindwa kumpa huduma za chakula, mavazi, tiba na Elimu akiwa mikononi mwa mama yake?

Mfano mume aliyeoa wake wawili au watatu ambao wanaishi makazi tofauti, mbona anawalea watoto wake wote wakiwa makazi tofauti na hadhi ya baba inabaki palepale?

Naomba mwenye kujua Jambo hili atamke, sababu Mimi naona hii haijakaa poa!

Hata baba yetu Daudi, yule mfalme mkuu tunayemuenzi kwa kuifanya taasisi ya michepuko kuwa na heshima, hakuwa na desturi ya kuchukuwa watoto wa mwanamke huyu na kuwapeleka kwa mwanamke yule!
Mwanamke azae, alee na kukuza watoto wake aliowazaa akisapotiwa kwa asilimia zote na baba mzazi!

Naomba kuwasilisha!
 
Wazee tufundishane hapa!

Kwenye maisha yetu Kama waume hii inatokea Mara nyingi tu. Mzee penzi limenoga kwa mchepuko, mara tu mimba hii hapa.

Wengine wanakataa ujauzito na mahusiano yanakufa!

Wengine wanaamua kuondoa mimba fasta, ili maisha yaendelee!

Wengine wanalea ujauzito na mtoto kwa Siri!
Lakini hata hivyo dunia Haina Siri, mwisho wa siku katoto kanatambaa, Mara kanatembea, ohooo hakoo kanaingia darasa la kwanza!
Mke amepata taarifa ya uwepo wa mtoto wa pembeni, Mara ooh katoto kameletwa ndani ya nyumba!

Hapa ndipo naleta hoja yangu!
Nini ulazima wa kumleta mtoto huyu ndani ya nyumba ya mke?

Hivi mama yake ameshindwa kumlea kweli, akipewa sapoti zote na baba husika?

Unamleta kwa mkeo apate Nini chenye ulazima wa kibinadamu atakachokikosa
kwenye makazi ya mama yake?

Je, baba utashindwa kumpa huduma za chakula, mavazi, tiba na Elimu akiwa mikononi mwa mama yake?

Mfano mume aliyeoa wake wawili au watatu ambao wanaishi makazi tofauti, mbona anawalea watoto wake wote wakiwa makazi tofauti na hadhi ya baba inabaki palepale?

Naomba mwenye kujua Jambo hili atamke, sababu Mimi naona hii haijakaa poa!

Hata baba yetu Daudi, yule mfalme mkuu tunayemuenzi kwa kuifanya taasisi ya michepuko kuwa na heshima, hakuwa na desturi ya kuchukuwa watoto wa mwanamke huyu na kuwapeleka kwa mwanamke yule!
Mwanamke azae, alee na kukuza watoto wake aliowazaa akisapotiwa kwa asilimia zote na baba mzazi!

Naomba kuwasilisha!
Hata baba yetu Daudi, yule mfalme mkuu tunayemuenzi kwa kuifanya taasisi ya michepuko kuwa na heshima, hakuwa na desturi ya kuchukuwa watoto wa mwanamke huyu na kuwapeleka kwa mwanamke yule!
Mwanamke azae, alee na kukuza watoto wake aliowazaa akisapotiwa kwa asilimia zote na baba mzazi!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lengo ni akuharibie kwa mkeo wa ndoa,

Imani yake "mkeo akijua umezaa nje, atakasirika na atadai talaka, aondoke zake ili apate nafasi aolewe yeye"

Sahv kina mama mijengo wamejanjaruka Sana, Anampokea Mtoto wako na maisha ya ndoa yanaendelea Kama hamna kilichotokea.

Utashangaa baada ya MDA mfupi,
anakushtaki ustawi ili umrudishie Mtoto wake.

Maana kitendo tu Cha kukurudisha Mtoto,
Mawasiliano na mirija yote ya pesa toka kwako inakua Imekata rasmi. Hii kitu inaumiza sana.

Hapa ndo MICHEPUKO UCHANGANYIKIWA SANA
 
Ni ego tu ila ukweli mwanao kumpeleka kwako akae kwa mama wa kambo ni hatari kwa afya yake japo wewe unaona sawa .

Wanaume wengi wanaona ile mtoto kama atakuja kuwakataa baadae ,ila ukweli bora umuache kwa mama yake kwa sababu baba wa kambo(mwanaume) hawezi kutesa mtoto kama mama wa kambo (mwanamke) wanakuwa na roho mbay sana.

Honestly ,tukife mahali tuangalie faida ya mtoto kuliko faida zetu sisi wazazi...
Muache tu kwa mama ake akae hata milele ,we jitafutie tu ili mtoto aishi vizuri
 
wengi hukwepa gharama na usumbufu wa mchepuko kiasi cha kuhatarisha ndoa... hivyo huona bora lawama kuliko fedheha​
 
Hakuna sababu Wala ulazima wa kufanya hivyo. Mtoto siyo ATM, mtoto siyo mbuzi useme utachinja unywe supu.

Mtoto ni liability!
 
Ni ego tu ila ukweli mwanao kumpeleka kwako akae kwa mama wa kambo ni hatari kwa afya yake japo wewe unaona sawa .

Wanaume wengi wanaona ile mtoto kama atakuja kuwakataa baadae ,ila ukweli bora umuache kwa mama yake kwa sababu baba wa kambo(mwanaume) hawezi kutesa mtoto kama mama wa kambo (mwanamke) wanakuwa na roho mbay sana.

Honestly ,tukife mahali tuangalie faida ya mtoto kuliko faida zetu sisi wazazi...
Muache tu kwa mama ake akae hata milele ,we jitafutie tu ili mtoto aishi vizuri
Safi sana
 
Back
Top Bottom