Ushauri: Nisaidieni namna Bora ya kutibu tatizo linalomuandama mama yangu

Nimesoma huu uzi, from my lower understanding of Psychology naweza kuelezea hivi.

Kuna tatizo maarufu sana kwa watu wazima, linaitwa PARANOIA, ni tatizo la kiakili yaani "Hali ya juu ya kujishuku", hii hutokea kwa watu wazima wafuatao;

1. Wale ambao walifeli baadhi ya mambo katika maisha yao, na watu wengine wakawa wanajua 'Failures' zao. Mara nyingi hawa, huwa wanawindwa na mawazo ya majuto "Hallucinations" ambapo anahisi kama watu wengine pia wanamsema kama yeye anavyojuta. Hii inapelekea mtu kuona hakuna sababu ya kuendelea kuishi, kwa sababu maisha ni muingiliano (Interaction) kama unahisi wanaokuzunguka wanakusengenya, kuna haja gani kuishi? Ni rahisi mtu kutaka kujitoa uhai.

2. Wale wenye magonjwa ya kudumu; kwa uzoefu wangu, watu hawa pamoja na walemavu ni makundi yanayoongoza kuwa na shida hii (Paranoia); kwa kuwa hujitofautisha na wengine, hivyo husisi wametengwa, japo huenda ikawa kweli ama yeye ndiye akawa amejitenga (Self Isolation), ndio maana, ARVs hazikutosha kutatua shida yake kiafya, matibabu ya kihisia ni salama zaidi na ya kudumu, tunatibu hisia kupitia Muingiliano, ndio mana nikutoe kidogo kwenye mada, kama mkeo upo nae mbali, muingiliano hushuka, hisia hupotea, mapenzi pia yanakufa. Nagusia tu

Sasa basi, kitendo cha watoto wake wa kuzaa kuwa mbali, kunachochea kushuka kwa muingiliano, kushuka kwa hisia, hivyo kupoteza tumaini. No hope, no reason to live.

Kwa nini hasa asingizie wengine?

Turudi hapo hapo kwenye somo la Saikolojia, umeona hilo kundi namba moja? Yani watu wenye failures za maisha, sasa nikwambie hakuna anayekubali failures kirahisi ndungu yangu, ni hivi.

Timu ya mpira inaweza kucheza Fyongo, ikafungwa, ila haitakosa wa kumlaumu, naomba uelewe ni "Wa Kumlaumu" maana yake ni mtu, aidha refa, mchezaji ama hata kocha. Ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye majuto, akianza kuyakataa, kitaalamu tunasema ana "Play, victim side" yaani yeye hujiweka kama mhanga wa shida anayopitia, ila mtu fulani ndiye lazima awe sababu.

Katika pita pita yako, uliwahi kusikia mzee yeyote anayeshinda kwenye vijiwe vya kahawa huko akasimulia historia yake ya shule akasema alikuwa wa mwisho darasani? Hapana, imekuwaje leo kawa hivo? Atamtafuta wa kumtupia lawama. Kitendo hiki, kwa kingereza kinajulikana kama PROJECTION DEFENSIVE MECHANISM

Ni nini haswa?

Ni hali ya kujilinda kutoka kwenye makosa/majuto ama lawama, kwa kumuona mwengine kama sababu ya shida yako.

Je mama yako anayo?
Jibu ni NDIO, anahisi kutengwa, jiulize, aseme anataka kuuliwa kwa lipi? Kitendo cha kuhisi kutengwa kinamfanya ajihisi kama mnasema/mnamsimanga/ ama mnamuonea kinyaa, hilo ndio PARANOIA bwana , anatumia njia ya Projection, ili siku kwa bahati mbaya (Siombei) akiaga dunia, msije mkazungumzia hali yake (UKIMWI) bali ugomvi wake na mtu fulani, kwa sababy ikiwa hivo, ni aibu, kama ujuavyo ugonjwa wenyewe kwenye jamii yetu unavyochukuliwa.

MFANYE NINI?
Kabla ya kuhangaika na Watabibu wa akili, ninyi ndio mnapaswa kuwa watabibu wa kwanza (Kumbuka ulisema hali yake kabla hamjaondoka) kaeni na mama yenu, ikiwa mna familia zenu, fanyeni ratiba ya kila siku moja ya wiki muwepo woote, mkae nae, mle nae, stori n.k. hakikisha hamzungumzii masuala yenye kutia huzuni huko, sio mnaanza stori za marehemu bibi yenu wa Kibaigwa, hapana, ni mwendo wa kujichekelesha.

Halafu; kama ulivyotuletea ombi hili la ushauri, utuletee na mrejesho baada ya kufanya hivi.

Mwl. Diwani
Asante mkuu ntajitahidi kufanya hvyo na kuhakikishia ntaleta mrejesho hali yake ikitengamaa
 
Pole sana mkuu, kwa dalili za mama anaonesha dalili za ugonjwa wa akili.
Ana dalili kama hizi
•persecutory delusion- kuwa na imani kwamba kuna watu wanataka kumdhuru bila ya kuwa na ushahidi au maelezo ya kueleweka kwa namna gani wanataka kumdhuru.
•suicidal ideation-mawazo ya kutaka kujiua.
•disorganized speech- kuongea vitu havieleweki ambavyo haviendani na muktadha.
•kukosa usingizi.
Mkuu kwa hayo machache ni dalili za ugonjwa wa akili ambapo yawezekana akawa na either magonjwa ya psychosis(HIV associated/induced psychosis) au magonjwa ya mood disorders.
Nakushauri ufike hospital yoyote hasa ile ya rufaa kwenye kitengo cha magonjwa ya akili utapata msaada mkuu.
 
Pole kwa kuuguza,
Ni vyema kufika hospitali na kuhusisha vitengo viwili:

1: Afya ya akili(kuangalia hali yake kwa undani, yawezekana kuna zaidi ya ulichokiona binafsi).

2: Kitengo cha CTC(kuangalia hali yake ya ugonjwa vs aina ya dawa anazotumia kama zaweza kuhusika).

3: Mama asiwe/asibatizwe jina kuwa ni kichaa bali tatizo la afya ya akili na wanaomzunguka, hasa ndugu. Itamsaidia kujikubali.

4: Mwenendo wa kimaisha: kuishi peke yake au anaoishi nao wanashirikiana nae kwa kiasi gani na wanampa ushirikiano kwa kiasi gani. Kwa umri wake, anajihusisha na nini? Ushiriki wake katika masuala ya dini vs jamii.
Kiukweli anaishi na dada yangu na dada ananiambia wanampa ushirikiano mzuri tu pamoja na hali waliyokua nayo lakini wanajitahidi kumuelewa na kuishi nae hivyo hvyo
Mimi ndo Niko mbali nae napanga niandae likizo nikawaone na nijumuike nao Kwa pamoja

Na pia uwa naongea nae mama na ananiambia anataka amuone mjukuu wake mana tangu mke wangu amejifungua sijapata nafasi ya kumpeleka mtoto akamuone.....

Na mimi nikiwa naongea nae kwenye simu huwezi amini unaweza ukahisi Hana tatizo kabisa ila zikipita siku kadhaa tu utasikia Kuna jambo huko ameshalifanya mpaka linakua linawaogopesha watu anaokaa nao
 
Hivyo vidonge alitakiwa apewe kwa nguvu au kwa Siri hata kwenye juisi ilimuradi muhakikishe anatumia hizo dawa huwa zinawapa usingizi wanapata muda wa kupumzika, mpaka anapona.
Daah tutajitahidi ndugu yangu ila ni changamoto akibaini Kuna vitu mmemchanganyia anakua na hofu anahisi mmepanga njama za kumuua,na hapo hata umueleweshe Kwa upole namna Gani hakuelewi kabisa
 
Hataki siku hizi kwenda mwanzon alikua anaenda mwenyewe ila tulipoanza kuona hii hali uwa tunaenda tunamfatia dawa tunamletea nyumban
Kumchukulia dawa inatakiwa iwe kwa dharura tu!

Mpelekeni hospitali mkawaeleze wataalam wa afya jinsi anavyobehave, ni tatizo dogo watalishughulikia.

Nyie kama watu wake wa karibu mna jukumu kubwa sana la kumfariji na kumfanya ajihisi ni mwenye thamani sana!!

Mwisho, nina mashaka kama hata hizo dawa anazitumia Kwa usahihi ikiwa tu kwenda clinic hataki..
 
Nadhani pia upweke ulichangia hasa kama mlikuacha akiishi peke yake kwa muda mrefu.
Jaribuni kumuweka karibu na kumuweka karibu na Mungu kutokana na imani yake.
Pia kama inawezekana hana shida zaidi ya hiyo achangamane na wamama wenzie kama ni Kanisani au Msikitini ili asiwe mpweke kama ni maombi au shughuli nyingine za kidini hasa mtaani.
Pia kama hapo anapoishi Kuna majirani wa umri wake jaribu kuwaweka karibu nae ili ajichanganye na watu itampunguzia mawazo ila tu angalia wale wenye busara na pia uwaeleze tatizo lake ila usiwaeleze ugonjwa wake haitapendeza ili wajuie wanadeal na mtu wa aina gani pia waweze kumsaidia ajisikie amani.
Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu.
 
Mungu amfanyie Mama yetu wepesi ila muwe mnajitahidi hata kumpigia simu kila baada ya masaa kadhaa.Vilevile kama mtampeleka Mirembe inaweza kuwa bora zaidi na msisahau kumpelela kwenye maombi!
Mkuu tunajitahidi sana Kila tuwezalo kuhakikisha mama afya yake inatengamaa
Na juzi tu hapa nilimuomba dada anitumie picha yake what's up nimuone alivyo
Aisee niliamsha mzozo wa hatari akadai nataka kupanga njama yaaaan mkuu sijui nikwambie nn mungu amponye mama ni mateso Kwa kweli
 
Kule kwa mamamdogo kulikuwa sehemu sahihi sana endapo mamamdogo angechukua jukumu la kumshirikisha kanisani muda wote awapo huko ili naye azoeane na kujenga urafiki na watu wengine. Kanisani angesali, kuimba(muhimu katika kutuliza na kuburudusha akili) na angeshiriki kwenye shughuri za kinamama.
Hata hivyo jaribuni sana kutomuacha nyumbani kwa muda mrefu, mchukueni kwenye matembezi ya marakwamara.
Kisa cha mamdogo kuogopa ni kwamba alimuona mamdogo ni kama adui yake japo alikua akimchukua na kumpeleka kwenye maombi mara Kwa mara lakini Kuna siku alitaka kujinyonga akiwa ndani kitu ambacho kilimfanya mamdogo kuogopa kukaa nae
 
Pole sana mkuu, kwa dalili za mama anaonesha dalili za ugonjwa wa akili.
Ana dalili kama hizi
•persecutory delusion- kuwa na imani kwamba kuna watu wanataka kumdhuru bila ya kuwa na ushahidi au maelezo ya kueleweka kwa namna gani wanataka kumdhuru.
•suicidal ideation-mawazo ya kutaka kujiua.
•disorganized speech- kuongea vitu havieleweki ambavyo haviendani na muktadha.
•kukosa usingizi.
Mkuu kwa hayo machache ni dalili za ugonjwa wa akili ambapo yawezekana akawa na either magonjwa ya psychosis(HIV associated/induced psychosis) au magonjwa ya mood disorders.
Nakushauri ufike hospital yoyote hasa ile ya rufaa kwenye kitengo cha magonjwa ya akili utapata msaada mkuu.
Asante mkuu nashukuru Kwa ushauri wako
 
Pole hizo ni effect za matumizi ya mda mrefu wa madawa. Waoneeni madaktari wanao msaada wa kupunguza madhara ya madaw hayo. Changamoto itakuwa kwa mgonjwa kukubali kutumia Ili apone, ukaribu na ufariji ni muhimu zaidi, pili mwambie sister asichoke asiyajali maneno yake still Hakuna thamani kubwa duniani kama kumtunza mama. Msiogope msikate tamaa pambaneni hadi sent ya mwisho hadi mda wa mwisho.Ili Nguvu ya maombi itende Kazi ni lazima anaombewa airuhusu iingie ndani mwake ndipo ufanya kazi.
Dili ni chanzo cha tatizo yaani side effects za hizo dawa kwanza atakaa SAwa.
 
Back
Top Bottom